Boomslang kwa kiswahili ni?Yuko na mwanasayansi mmoja mmarekani mwenye asili ya ujerumani alikuwa anamchezea Boomslang mdogo akang'atwa alipoulizwa kama asaidiwe matibabu akasema nyoka huyo ni mdogo kwa hiyo hana madhara...alikufa usiku wake.
Nyoka wa kwenye miembe.Boomslang kwa kiswahili ni?
Huyo black mamba ndio koboko ni lugha tu hiyoYeah, wewe unamjua, watu wanachanganya na black mamba sijui kobra, tofauti kabisa, huyu jamaa kwanza hana rangi nyeusi, ni mweupe fulani hivi, ana singa kichwani na akitoa mlio unaweza fikiri ni jogoo, anasafiri kama helcopta, ana shabaha, ana lenga kichwani tu, akikugonga dakika tano nyingi tuna zika, tumewaua wengi kijijini, mkigundua sehemu kuna koboko, tulikuwa tunajitwisha uji wa moto kwenye sufuria, akikuona lazima akurukie kichwani, anajizamishwa kwenye uji wa moto anakufa.
Khaaa...nisingependa kukutana na aina ya nyoka yoyote maishani mwangu!Nyoka wa kwenye miembe.
Koboko akikukimbiza kama kuna mteremko huwa ana tabia ya kung'ata mkia wake halafu anakuwa kama gurudumu kubwa la baiskeli dakika moja tu aanakufikia.Khaaa...nisingependa kukutana na aina ya nyoka yoyote maishani mwangu!
Kitu nilichojifunza kuhusu koboko ukikutana nae polini okota tofali au jiwe lolote kisha liweke kichwani haraka haraka hivyo akija kugonga kichwani atagonga jiwe au tofali .NIKIKUTANA NAYE BARABARANI NIFANYEJE JAMENI????? MAANA NINA TABIA YA KUFUKUZA NYOKA KWA MAWE AU GONGO.🙁
Wewe jamaa ndie koboko mwenyewe nini ? Maana ulivyocheza na huu uziKoboko akikukimbiza kama kuna mteremko huwa ana tabia ya kung'ata mkia wake halafu anakuwa kama gurudumu kubwa la baiskeli dakika moja tu aanakufikia.
Hamna vivutio hapo, kuna shida tuMkuu hutaki vivutio vya wa talii[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Kwa kweli Koboko huwa napenda stori zake kwa mbali tu ila huwa nikisikia kaonekana mahala na ni mkubwa wa kukomaa huwa nakula kona.Wewe jamaa ndie koboko mwenyewe nini ? Maana ulivyocheza na huu uzi
Koboko anagonga popote pale hili la kusema anatafuta kichwa tu sio kweli labda akiwa kwenye mti na wewe unapitaKitu nilichojifunza kuhusu koboko ukikutana nae polini okota tofali au jiwe lolote kisha liweke kichwani haraka haraka hivyo akija kugonga kichwani atagonga jiwe au tofali .
Kama hakuna tofali okota mti au tumia gongo uanze kupambana nae ukiona amekurukia kichwani au anakuja mpige na gongo kumzuia asigonge utasoni na wakati unapambana nae usiwe muoga yaani wee hakikisha unalinda kichwa chako tuu na katika mapambano yako hakikisha unamtaja mungu wako akusaidiee koboko akuone huruma akusamehee maana yule mdudu huwa hawezi kusalender katika mapambano
Hili halina ushahidi Reptiles hawana vinyweleo.ana singa kichwani na akitoa mlio unaweza fikiri ni jogoo,
Kweli Mwenyez Mungu kila upande kaweka maaajabu yake, tembo wanaomboleza km binadamu, tembo analia kwa uchunguWe!
Tembo kwa visasi usimtanie kabisa.
Kuna Daktari Mzungu wa wanyama pori alkuepo pale mikumi,
naskia aliwahi kuuawa na Tembo kikatili sana.
Jamaa naskia alikuta kitoto cha Tembo kiko hoi bin taabani peke yake pirini kimepona pona kuuwawa na Simba.
Basi jamaa akaita gari kikapakiwa na kupelekwa camp kwa matibabu.
Kilipopata nafuu,
Na kuweza kusimama na kutembea.
Majamaa wakaona ni vema kikarudishwa tu porini kiendelee na maisha yake.
Basi wakakipakia Tena kukirudisha porini.
Wakashauriana na wenzie kua NI vema kikapelekwa walipo jirani na Tembo wenzie kwa ajili ya Usalama wake zaidi.
Basi,
kikafikishwa na kuwekwa kama mita 500 kutoka walipo Tembo wenzie.
Basi wakaona kimesimama tuli na wenzie wanaanza kukifata
Wenzie wakawa kama wanakifariji na kama wanacheza hivi
Mda so mrefu wakaona kimelala chini, jamaa wakahisi labda ndo michezo yenyewe.
Baada ya hapo,
Tembo wenzie wakaanza kutoa sauti kubwa sana.
Yule dokta akawaambia wenzie kua,
Inawezekana hali ya kile kitoto ni mbaya zaidi.
Huo ni mlio wa huzuni kwa tembo kulia vile.
Ni vema wakasogea na kuangalia zaidi,
Jamaa wakasogeza gari karibu mpk kufkua km mita 200 hv.
Ghafla Jamaa wakawaona tembo wakichimba shimo pana.
Yule Dokta akawadokeza wenzie kua,
"Bila shaka kile kitoto cha tembo kitakua kimefariki, hayo yatakua ni maadalizi ya mazishi"
Basi dokta akawasihi,
"Ni vema tutoke hapa HARAKA sana, tembo huwa hawataki kabisa bugudha wakati wa mazishi"
Wale jamaa wakang'ang'ania eti wanataka waendelee kuona mpaka mwisho jinsi Tembo wanavyofanya mazishi.
Basi jamaa wakanogewa kuendelea kuangalia lile tukio.
Basi mwenzao mmoja, akachomoa kamera ili kupiga picha.
Aisee;
Ile jamaa alipopiga picha moja tu, ule mwanga wa flash ukawapiga wale tembo.
Ghafla waliona tembo wawili WAKUBWA wakiwageukiwa na kuja kwa kasi ya ajabu.
Yaan ile hata gari kubwa waliokua nayo (mitsubishi fuso) haijawaka, wale tembo waliipiga kwa nguvu ikayumba.
Wakaipiga Tena, ikapinduka.
Ghafla wakaona washafika tembo kama 5 hivi.
Wakaendelea kuipiga, gari ikaanza ku-roll mpaka kwenye kwenye mfereji wa maji.
Basi ilkua kila aliepata upenyo, ni kukimbia tu. Mpaka silaha zao walisahau kwny gari lile.
Jamaa wenzie walioweza kutoroka, kwa mbali walimuona aliebaki pale ni dokta.
Na keshatolewa nje ya gari anakimbizwa na Tembo wawili
Na kwa sababu, eneo LA camp halikua mbali, jamaa wakakimbilia camp kuchukua silaha kumsaidia dokta.
Wanarudi tu,
Wakakuta tembo washaondoka na dokta ndo keshauwawa tayar na kazikwa kwnye shimo fupi Jirani na kile kitoto cha tembo na kufukiwa kwa majani&matawi ya miti.
Waliitoa maiti ya dokta kwenye shimo ikiwa imevunjwa vunjwa viungo vyote.
Na ikiwa haina mkono mmoja.
DAH; JAMAA WALIUMIA SANA.
WAKAJILAUMU SANA KWANINI HAWAKUFATA USHAURI WA DOKTA KUA WAONDOKE ENEO LILE HARAKA SANA.
WAKAMLAUMU SANA MWENZAO ALOPIGAILE PICHA YENYE FLASHI NA KUWAAMSHA GHADHABU TEMBO.
WAKAWAZA KUA ,
HUENDA TEMBO WALIFANYA KISASI WAKIHISI YULE DOKTA NDO KASABABISHA KIFO CHA MWENZAO.
INAWEZEKANA NDO MAANA WALIPOMUUA WALIENDA KUMZIKA JIRANI NA KITOTO CHAO
Dah, Jamaa wote waliumia sana.
( Hii stori nlisimuliwa na Mzee Mose, alkuaga askali wanyama pori pale Mikumi. Kwa sasa amestaafu)
Hahhhahahha, we jamaaaaHuko South afrika wakati wa utawala wa makaburu walikua wanachukua mayai yake yakishatotolewa wanawafuga kidogo halafu usiku wanaenda kuwaachia kwenye maeneo ya weusi cha ajabu wale koboko walikuwa ni wapole mpaka leo koboko ni wengi kwenye miji yao.
Tembo ni walezi wazuri sana wameshawahi kuonekana wakiwachapa watoto wao ili kuwatia adabu.Kweli Mwenyez Mungu kila upande kaweka maaajabu yake, tembo wanaomboleza km binadamu, tembo analia kwa uchungu
Mbona hawa wadudu warefu sana, yaaan nikitazma hapoView attachment 769338
Kitu hicho kilichokomaa kinawinda.
Hao huwa wanapatikana mapori makubwa.Mbona hawa wadudu warefu sana, yaaan nikitazma hapo
Wanaweza kufikia mara nne ya kima cha binadamuMbona hawa wadudu warefu sana, yaaan nikitazma hapo