Kocha Noureddine Al-Nabi atua Yanga

Kocha Noureddine Al-Nabi atua Yanga

Shadow7

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2020
Posts
24,606
Reaction score
39,289
Mabingwa wa Kihistoria, Timu ya Wananchi, Vijana wa Jangwani na Vinara wa Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara Young African Sports Club wanadaiwa kumpa mikoba Kocha, Nasreddine Nabi iliyoachwa na mtangulizi wake Cedric Kaze.

al-merrikh-sc-sack-their-head-coach-nasreddine-nabi_1sis85jid9ne12rtd1sn1rpiq.jpg


Nasreddine Nabi aliyekuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya El Merreikh atachukua nafasi hiyo ambayo kwa sasa inakaimiwa na Juma Mwambusi.

Kwa mujibu wa tetesi zilizopo ni kuwa Kocha huyo Mpya wa yanga anatarajiwa Kuwasili rasmi Nchini hapo kesho siku ya Jumanne akiwa na benchi lake la ufundi.

Kocha huyo raia wa Tunisia ni muumini wa mfumo wa 4-1-4-1 na anauzoefu na soka la Afrika.
 
Kha yaani utopolo wameshindwa ata kumuachia mwambusi amalizie ligi?
Mbona wanampiga danadana mzee wa watu hivi
 
Kila siku usemi wa Simba next level unajionyesha, tumechukua kocha Sudan nao wameiga tena timu ileile, sasa hivi wanataka kuajili mtaalamu wa video kumbe Senzo alikuwa mweupe anangoja Babra aanze na yeye aige
 
Mabingwa wa kihistoria Tanzania, Dar wa Salaam Young Africans maarufu kwa jina la Yanga leo wamemtambulisha, Nasreddine Nabi raia wa Tunisia kuwa kocha wao mpya

Nabi ambaye anakuja kuchukua mikoba iliyowachwa na kocha aliyetimuliwa Kaze kutoka nchini Burundi


Screenshot_20210420-170603~3.jpg
 
Kocha anaweza kua mzuri lakini wachezaji wenyewe wako wapi?
 
Back
Top Bottom