Baada ya hii mechi sitarajii kama huyu jamaa ataendelea kuwepo.
Ni mpuuzi sana
Labda nikuambie kitu kimoja,
Kuna Mpira biriani, ufundi mwingi, pasi nyingi, mchezo umetulia, watu wanatandaza Samba uwanjani, kampa kampa tena, Barcelona ya Pep Guardiola watu wanapiga mpaka pasi 800+.
v/s
Mpira kukamiana, ukishika tu mpira mpinzani huyu hapa, kiatu mtu, weka ugoko niweke jiwe, heri mshambuliaji upite mpira ubaki au mpira upite mshambuliaji abaki, ulipo tupo miaka yetu tuliita "Bundesliga".
Mpira wa jana kua na faulo zote zile ni wazi uliegemea kwenye aina ya pili hapo juu. Kuna wachezaji wanamudu mifumo yote miwili na wengine kama Chama ni wazuri mfumo mmoja, ule wa kwanza.
Ndio maana hata kiwanja kikibadilika tu kikawa kama vile vya mikoani vyenye features zote za mabonde, milima, mito, tambarare basi chama hutomuona aking'ara sababu ye ni mzoefu zaidi wa ule mfumo wa kwanza.
Watu walikamiana sana, Chama yuko Kwa Mkapa, Uwanja safi sawa lakini asingeweza ku shine kwa mchezo wa jana. Kuhusu BM3 huyu ni kama alishakua Ms Jazba hivi