Kocha wa simba awaka asema siwezi kumtumia Mo Ibrahim,hana nidhamu na simba sio timu ya sikukuu

py thon

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
2,476
Reaction score
4,448
“ MO amekuwa na tabia ya kutokuja mazoezini akiwa na sababu nyingi kila mara jambo ambalo linaathiri kiwango chake na hivyo sitaweza kumtumia. Simba sio timu ya sikukuu ambayo unaamua leo uje kesho usije . Mchezaji mwenye weledi sahihi na kazi yako huwezi kuacha kuyapa kipaumbele mazoezi ya mwalimu wako, masilahi ya timu na kipaji chako” alisema Pierre kwa ukali.

 
Kuna sababu zinazopelekea hapa ukali hautakiwi dogo akalishwe chini atafunguka tu
 
Hao ndio wachezaji wa bongo au afrika hawajitambui wakisifiwa na kuandikwa tu na magazeti vichwa Vina viimba. Nakumbuka mashabiki WA simba wakati WA Omog walikuwa wanamtetea Sana mo hapangwi. Kumbe mtoro na mvivu WA mazoezi. Mimi ni simba kulia lkn sikubaliani na ujinga wa WAchezaji na mashabiki. Hugo afukuzwe tu ana maringo san
 
Wanamuonea tu yule Mganda huwa anajipa likizo na anapangwa kila mechi
Yule ni mfalme ana sauti kwenye timu kuliko hata Manara! Kama mzungu hajipendi ajaribu kumgusa! Awe mgonjwa, awe mtoro lazima acheze!
 
hapo ndio tunaona tatizo la management za timu zetu, meneja anafanya nini kumsaidia mchezaji
viongozi kama katibu anafanya nini kumrekebisha mchezaji
Wakala wake anafanya nini kumsaidia mteja wake au yeye anasubiri mkataba uishe ndio ajitokeze kumpiga bei
 
Yule ni mfalme ana sauti kwenye timu kuliko hata Manara! Kama mzungu hajipendi ajaribu kumgusa! Awe mgonjwa, awe mtoro lazima acheze!

Lakin pia ufalme wake hajaupata bure, mganda anaonesha utofaut mkubwa sana akiwa uwanja. Kwa kifup soka la bongo hakuna wa kumfananisha nae.
 
Namfahau Mo ( nimecheza nae na pia tulisoma wote o'level) ni moja kati ya wachezaj wenye nidhamu ya hali ya juu... Somethng is wrong here!
 
Namfahau Mo ( nimecheza nae na pia tulisoma wote o'level) ni moja kati ya wachezaj wenye nidhamu ya hali ya juu... Somethng is wrong here!

Hata mimi nina wasiwasi kuna kitu hakiko sawa. Jamaa anaonekana ni mwenye nidhamu kabisaa.
 
Unamchukia sana Okwi.. kwa nini? mtu ambaye haiingii darasani ila mitihani ikija anafaulu kitu ambacho ndo lengo la mwalimu huwezi mfananisha na mpuuzi mmoja ambaye ana akili ya wastani ila hatak kujibiidisha kusoma matokeo yake anafail. mpumbavu atasema mbona mwanafunzi flani yeye akienda likizo anachelewa kurudi darasani. kumbe huyu akiwa likizo huwa anasoma sana tu. akirudi hata ukimwambia test kesho anafanya anafaulu. huyu pumbavu anachelewa kurudi kumbe anakuwa huko akibet na kunywa viroba... ujinga kabisa. okwi alionywa na akajirekebisha na akaanza kuperform vizuri tu. TUACHENI KUMCHUKIA OKWI.

Wanamuonea tu yule Mganda huwa anajipa likizo na anapangwa kila mechi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…