Mkuu, utaumiza kichwa bure kuelimisha UTOPOLO! Wao, wana jibu lao tayari!Kama kushinda nyumbani tu, kwa hivi karibuni haya matokeo nayo yalikuwa nyumbani?
Vita Club, 0-1 Simba SC,
Jwaneng Galaxy 0-2 Simba SC.
Plateau United 0-1 Simba SC.
Huu ndo utani ambao tulikuwa nao toka zamani..!guvu moya kanji bai awaite wachezaji na kuwapa vitisho. ushindi utaibuka mkubwa tu
Maoni yangu kuhusu mtanange huu ni kwamba Pablo ujuzi ni ndogo kwa hilo uliloliona.Mashabiki wa Simba SC na Wadau wa soka, upi uchambuzi wako kuelekea kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya RS Berkane, utakaofanyika Jumapili ya March 13 kundi D kwenye dimba la Benjamin Mkapa.
Unadhani Kocha Pablo Franco Martin aingie na mpango, au mbinu ipi kuhakikisha anapata ushindi kwenye mchezo huu, ambapo Simba SC walipoteza kwenye mchezo wa kwanza ugenini kwa mabao mawili kwa bila.
Kwangu..Simba SC wanatakiwa kuanza kwa kupress kwenye mstari wa juu [High Press] hii itasaidia Back Line ya RS Berkane kutokuwa Comfortable na mpira hivyo pressing ya Simba SC itanza kufanikiwa kwa haraka zaidi kutokana Kasi ya Sakho kulia na Movement nyingi za Banda kushoto, kwasababu RS Berkane kuna uwezekano wa kupress mstari wa kati [Mid Block].
Na hapo inatakiwa kiungo wa chini awe na akili ya haraka kutoa msaada pembeni, na katika sehemu ambayo Simba SC inatakiwa kuwa makini na kufanyiwa kazi sana kwenye mazoezi ni mipira ya kutengwa (Set Pieces) mabao mawili kwa RS Berkane yalipatikana kwa njia hiyo.
Utabiri wangu Kikosini;
1.Manula.
2.Kapombe.
3.Hussein.
4.Onyango.
5.Inonga.
6.Mkude.
7.Sahko.
8.Mzamir.
9.Kagere.
10.Bwalya.
11.Banda.
Akiba;
Kakolaya, Israel, Nyoni, Wawa, Lwanga, Kanoute, Bocco, Kibu, Jimmyson, Morrison.
Yapi maoni yako kuhusu mtanange huu.
..Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana..[/b]
Huu ndo mtazamo au uchambuzi tunataka, hivyo hatuna budi kuheshimu maoni kama haya.1. Manula
2. Kapombe
3. Zimbwe
4. Onyango
5. Inonga
6. Mkude
7.Sakho
8.Mzamiru
9.Kagere
10. Kibu
11. Efua Moriss
Sub: Kakolanya, Gadiel, Nyoni, Mwenda, Bocco, Jimson, Mhilu, Bwalya na Lwanga.
N:B
Timu icheze jihadi iache ujinga wa kupiga backpass 600 na square passes 500.
Tucheze mipira mingi ya kwenda mbele tena kwa kasi kubwa kama ya kipindi kile tunacheza na Kaizer Chiefs au As Vita club hapo Lupaso stadium.
Tucheze mpira wa kasi na kukaba wote huku tukianzia mashambulizi juu kuliko chini.
Pia Kocha ana kaujinga flani kanakofanana na kocha wa PSG kakuchelewa kufanya sub kwa mchezaji aliyeboronga au ambeye mpira umemkataa siku hiyo.
Aache kuwaanzisha Banda na Bwalya hawa hawana nguvu wala kasi inayotosheleza kupambana na Waarabu. Huwa wanachelewesha au kupoteza mipara kwa wepesi ukiwafanyia pressing.
Mwisho japo si kwa umhimu:
"Kamati ya roho mbaya iongeze mashambulizi ya mabomu nje na ndani kwa dakika zote 90 + kuliko yale ya Russia dhidi ya Ukraine."
Mbinu hii ingetumika wale river wangepigwa nje ndaniTutumie zile zile mbinu zetu za kuspray hewa ya kuwalekeza mwili