Kocha wa Yanga SC akumbushwe hili kuhusu TP Mazembe

Kocha wa Yanga SC akumbushwe hili kuhusu TP Mazembe

Hukumbuki hata afisa habari wao alipata kusema kuwa Yanga ina Wachezaji Quality na thamani kubwa kuliko Al Hilal

Wanajipumbaza sana.
3/4 ya kikosi chao ni wacongo ambao wametokea team ya As Vita ambayo ilikuwa ina tawaliwa na haohao Mazembe, kisha mpumbavu mmoja anasema Yanga ina kikosi kizuri kuliko
mazembe.
 
Kocha wa Yanga akumbushwe kwamba TP Mazembe siku zote wanacheza mpira wa kujiami sio ugenini au nyumbani kwa hiyo akija na mpira wake ule wa kutafuta possession na kushindwa kupeleka mashambulizi mbele hatutoboi hakika hivi

Yanga tuna wachezaji wazuri kuliko Mazembe ila Mazembe wanajiamini kuliko sisi. Kwa hiyo basi ili kuwaweza mazembe ni lazima tucheze mpira wa long pass ili kuzuia mazembe wasiwe wanapanda saana
Na tutumie washambuliaji watatu Mzize, mayele, na msonda. Tuachane na kisinda, na moloko tucheze na Centre forwards watatu

Dawa ya moto moto tu ni speed kwenda mbele bila ivo hakika tutalamba makaa ya moto
Kwamba long pass???!!!
 
Kisindaa na maroko hawafaii kuchezaa yanga , na yanga Haina mpishi wa magori mfano Simba tunajuaa wapishi wa magori ni chama anaasist 12++ na tibazongizaa anamagori na assist......... tukijaaa yanga fei hayupo yupoo Jesus moroko ndo mpikajii/mtengenezaji wa magori afu anaasist 3 tuh afu uyoo ndotunaamtegemeaaa kwenye match za kimataifa inasikitishaa Sanaaa [emoji1787]
Hahahaha
 
Central forward bila mawinga lazima wawe na uwezo wa kukaa na mpira, kufungua au kuvunja ukuta! Yanga mna typical strikers mtawapa mzigo tu.

Simba washambuliaji wetu wote wanaweza kucheza role tofauti, Boko anaweza kutokea pembeni, Phiri, Baleke, Kibu, Kiyombo, Chama, Saido wote wanaweza ku switch position ndani ya game kuleta matokeo.

Yanga lazima mcheze na mawinga aina ya Bernard Morrison na Farid wawasaidie. Pia mnajitaji kiungo mbunifu kurahisisha kazi kwenye mashambulizi. Feitoto hayupo msogezeni Aucho mbele awe huru then Bangala awe kiungo mkabaji. Mtapata balance nzuri.

Bila Morrison aliyefiti hiyo game itakuwa ngumu sana kwenu.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Thread ilipaswa kuishia hapa.
 
Timu za Tanzania wikiend hii ni vilio vizito.
 
Eti Yanga ina wachezaji wazuri kuliko Tp mazembe!
Akili zenu huwa mnazivua au hamnazo kabisa?

Au mlipodanganywa na injinia Hersi kuwa aliwapiku Mazembe kwa Musonda mkajiona wakubwa siyo?

Mazembe bado ni dume la simba lililozeeka kamwe halitakuwa nyau.

Ni timu inayoweza kupata matokeo chanya popote bila kujali ugenini.
 
Asimpange kisinda kabisaa, huyu mtu na Morrison sijui injinia alikunjea uji wa wapi hadi kushawishika kuwarudisha. Kisinda anakimbia tuu hovyo mpaka usawa wa goli kashaapita saa nyingi bado anakimbia tuu
 
Yanga Wana wachezaji wazuri kuliko mazembe ..kisinda?,moloko?kibwana,job? Hauko serious wewe.
Kikosi cha bil 4 ufananishe na kikosi cha mil 600?
Aliyewadanganya watanzania kupima ubora wa kikosi kwa kuangalia thamani ya kikosi atafute auwawe.Watz 89% ni wacha-mbuzi feki
 
Huu ulimwengu haujawahi kuisha vituko nimecheka sana aliposema et uto ina wachezaji waruzi kuliko Mazembe.
Wachezaji hao ni wapi sijaona labda wapo wengine tofauti na wale tunaowajua.
Yupo mwanariadha anakimbia mpaka anataka kutoka nje ya uwanja ogopa anawazidi mpaka mbio linesman,mwingine beki kanenepeana trako kama lote.
Bado unaendelea kucheka au sasa hvi unalia?
 
Eti Yanga ina wachezaji wazuri kuliko Tp mazembe!
Akili zenu huwa mnazivua au hamnazo kabisa?

Au mlipodanganywa na injinia Hersi kuwa aliwapiku Mazembe kwa Musonda mkajiona wakubwa siyo?

Mazembe bado ni dume la simba lililozeeka kamwe halitakuwa nyau.

Ni timu inayoweza kupata matokeo chanya popote bila kujali ugenini.
Tuchambue kwa mizania mpira Wala hauhitaj jazba timu uliyoibeza imefanya maaajabu na timu uliyoiamin imeduwazwa

Tuache mpira uongeee mbona kocha wenu anafalsafa nzuri tu ya acha boli litembeee

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom