Nimesajiliwa baadhi ya wachezaji ambao sikuwataka mfano Makambo. Walisema wanamleta makambo atakuwa na Ajibu walicheza pamoja lakini niliona mtandaoni huyo Ajibu nae amesalia katika club yake ya Simba sasa sijui itakuwaje.
Kambi ya Morocco tumekuja ila hotel ya kwanza ilikuwa mbali na viwanja vya mazoezi nikaikataa hii ya pili ndiyo tumefikia umbali kutoka casablanca mpaka kambini ni kilometa kama 300 lakini tunapambana kujiweka sawa.
Jana kikosi kilisafiri ndege moja na wachezaji wa Simba wawili (Ndemla na Duncan) wenzetu waliposhuka walionganisha ndege mpaka ilipo kambi yao sisi tulichukuliwa na basi kitendo hiki sikukipenda ni kuwachosha wachezaji inaonesha jinsi gani watu wa logistics kwenye klabu hawapo vizuri.
Nilicha maagizo swala Sarpong na Saido walimalize kwa sababu hakuwa kwenye mipango yangu msimu huu mpya nashangaa sisi tulitangulia morocco kabla ya timu kufika kutoke Tanzania lakini nikashangaa kuwaona bado wapo nyota hao bado wapo kikosi wameshindwa kuvunja mikataba yao sina jinsi mimi ni mwalimu na kufundisha ndiyo kazi nitafundi ila napata wakati mgumu kwenye muunganiko wa mfumo kiuchezaji".
Maneno ya kocha wa yanga