Kodi ya Fremu alipe directly mmiliki wa Frem na sio mpangaji

Osei Tz

Member
Joined
Sep 20, 2018
Posts
96
Reaction score
79
Ukifungua biashara ukienda TRA ili wakokotoe kiasi cha kodi unachopaswa kulipa lazima wakuulize umepanga frem ya bei gan, Ile thaman ya frem kwa mwaka wanakokotoa asilimia ambazo ndio kodi ambayo kimsingi ilibidi ilipwe na mmilik wa frem au Jengo.

Pointi ni kwamba wamilik wa majengo au frem hawajawah na hawana huo utamaduni wa kumrudishia mpangaji ile hela alielipa.

Na wengi wetu tunaokodi hizi frem hua tunakua hatuna idea kama mweny frem anatakiw kulipa kodi kama income tax ambayo kimsingi hua anabebeshwa mpangaji (mjasiliamali).

Matokeo yake wajasiriamali wanaanza kuichukukia TRA kwamba wanawapangia kiasi kikubwa cha kodi ambacho hakilingani na mitaji yao, kumbe kalipishwa had income tax ya baba mweny frem.

Kwa mazingira haya wamiliki wengi wa frem hawalipi kodi kabisa wakati wanapata kipato kikubwa.

Ushauri: TRA iangalie namna ambayo itaondoa hii kero kwa wapangaji wa frem, kila mtu atimize majukum yake ya kulipa kodi, na sio mtu mwingine achukue jukum la mtu mwingine la kumlipia kodi.
Yeyote anaeingiza kipato alipe kodi yeye kama yeye vinginevyo TRA watakua wanakwepa majukumu yao.
 
Nadhani unazungumzia with holding tax (kodi ya zuio) ambayo ni asilimia 10 ya kodi ya pango. Uko sahihi kabisa kwamba anayetakiwa kulipa ni mwenye fremu, yaani kama umemlipa 1 million kodi basi anatakiwa apeleke tra 100,000.
 
Tumia akili kidogo tu. Kama kodi ni laki 1, basi tambua, kama angelipa hiyo kodi unayosema, kodi ya pango atakufanyia 120k. Ni akili ndogo tu, ni yale yale tu, kodi aliyokupangishia tayari inapunguzo ili uweze kutumia hilo punguzo kulipa kodi ya withholding.

Kama unaona wenye nyumba wanaenjoy, jenga zako.
 
Kunywa mbege chibuku 1 mwambie na akwii akupatie ugoro wa buku vyote nalipia mimi
 
Hili ndilo tatizo, yaani kutetea ujinga na kutopenda kusimamia sheria. Mfano kodi za fremu maeneo mengi zinafahamika, kama ni laki moja na unalipa kwa miezi 6 hiyo ni laki 6. Inatakiwa wewe umlipe hiyo laki 6 na yeye kwenye hiyo laki 6 atoe elfu 60 apekeke TRA. Sijawahi kujua ni kwa nini TRA huwa hawafuatilii jambo hili.
 
Huyo mwenye fremu kaweka kodi hiyo akijia wewe ndio utalipa withholdong. Kama ikatokea akadaiwa yeye directly , bila shaka atapandishabkodi kufidia hilo ongezeko, sasa inakuwa hakuna ukichokwepa. Nilichoandika umekielewa nadhani.., leta hoja kama unayo.
 
Hayo ni ya kwako, sheria haisemi hivyo. Logic ya kawaida kabisa ni kwamba wewe mwenye nyumba ndiye mlipa kodi kwa sababu umepata new income. Mbona kwenye mapato mengine kama mishahara hausemi anayelipa salary ndiye alipe income tax?? Wewe uliyelipa kodi ya fremu unalipaje withholding tax wakati hujazalisha chochote?
 
Ulichosema hakuna aliyekibisha. Sasa swali ni je, nilichokisema umekielewa?
 
Mkuu hii hoja yako haizuii TRA kwenda kudai wenyewe ushuru kwa mwenye flem badala ya kumkaba mkodishaji

Hata akiongeza pango bado nitakuwa na hiari nipangishe kwa bei aliyoitaka au niende sehemu nyingine alimradi withholding tax wamshike mpangishaji sio mpangaji ni uonevu

Halafu kingine unakuta wameweka viwango vyao kabisa vya kukokotoa withholding tax mfano wanakwambia ili uweze kupigiwa hesabu lazima pango lianzia 50k hata kama flem umekubaliana na mwenye nyumba umlipe 30k huu ni uonevu

Ndio maana kuwa mfanyabiashara bongo ni kama kutangaza vita na serikali yaani wao ndio wanakupangia kama vile mtaji wamekupa wao upuuzi tu
 
Hayo uliyoyasema sidhani kama kuna mtu ameyapinga. Ila swali ni je, nilichokisema umekielewa?
 
Sawa tutalipa sisi,ila badala ya laki kwa mwezi,itakuwa laki na ishirini, kufidia withholding tax
 
Kodi adaiwe muhusika hiyo ndio haki kuhusu kwamba eti mwenye nyumba ataongeza pango hiyo ni hiari ya mpangaji either apange au atafute sehemu ingine yenye unafuu

Siku zote biashara ni ushindani wewe ukipandisha fremu zako eti kisa unatozwa 10% ya pango wengine wanashusha na wanakubaliana na uhalisia

Mantiki ni kuwa mfanyabiashara asilazimishwe kulipa withholding tax ambayo haimuhusu TRA waende wenyewe wakadai ushuru kwa mwenye fremu
 
Ulichokisema hakuna aliyebisha. Swali ni je, nilichokisema hakina mantiki?
 
Atakusumbua huyo mweupe kichwani,hao ndio wapangaji ambao wakinunua umeme pia wanataka ile kodi ya jengo buku jero alipe mwenye nyumba, nna mpangaji wangu mmoja anajifanya mchumi kutwa kuniuliza nitamfidia vipi kodi ya jengo ya kila mwezi, nimemuambia ngojea mkataba ukaribie mwisho tutajua
 
Mzee ungeitisha maandamano kupinga ilo!
 
Mfano mdogo ni wasajili wa laini za mitandao mwanzo laini walikuwa wanauziwa sh 100 na walikuwa wanazisajili bure mteja anaweka vocha

Wakaja kuuziwa lain moja mia tano (500) wakatishia kupandisha bei kuiza buku na vocha mteja ajiwekee ya buku ili kumaintain faida

Matokeo yake laini imeendelea kuuzwa jero na bado wanasajili bure na vocha wanawaekea bure

Wewe ukilinga na fremu zako wengine wanawabembeleza wafanyabiashara kwa kuwapa ofa
 
Sawa, tuishie hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…