Kodi ya majengo ya ghorofa ni dhulma, haikubaliki

Kodi ya majengo ya ghorofa ni dhulma, haikubaliki

Gulwa

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2008
Posts
10,597
Reaction score
16,394
Mimi nina Kajumba kangu huku uswahilini, kwa sababu ya ufinyu wa eneo nilijiongeza nikawekwa kaghorofa. Sasa serikali inanitaka nilipe elfu 15 kila mwezi. Yupo jirani yangu aliwanunua watu na kupata eneo kubwa, kuliwekea Uzio na kushusha mjengo wa kisasa wa nguvu.

Thamani ya jengo la jirani inaweza kuwa mara tano ya kaghorofa kangu, yeye atakuwa analipa buku jero kwa mwezi!

Sasa nawauliza hawa wataalam wetu wa kodi wametumia kigezo gani cha kutuadhibu wenye ghorofa? Kujenga ghorofa ni ishara ya utajiri na nyumba ya chini ni umaskini?

Nina mashaka na mfumo wa elimu wetu, huenda unazalisha wajinga zaidi
 
Kwa ujumla wake tu kodi ya majengo ni wizi. Maana umenunua ardhi kwa hela yako, umenunua vifaa vya ujenzi kwa hela yako (na hivyo vifaa tayari vimeshatozwa kodi za kila aina), unajenga nyumba kwa hela yako!
Sasa kwa nini ulipe tena kodi ya majengo kila mwezi!! Huu ni wizi.

Kama serikali inapenda kutoza kodi za majengo, ijenge nyumba zake nchi nzima na kuwapangisha watu wenye uhitaji. Ila siyo kuibiana mchana kweupe kupitia hizi sheria zao za kipuuzi.
 
Kwa ujumla wake tu kodi ya majengo ni wizi. Maana umenunua ardhi kwa hela yako, umenunua vifaa vya ujenzi kwa hela yako (na hivyo vifaa tayari vimeshatozwa kodi za kila aina), unajenga nyumba kwa hela yako!
Sasa kwa nini ulipe tena kodi ya majengo kila mwezi!! Huu ni wizi.

Kama serikali inapenda kutoza kodi za majengo, ijenge nyumba zake na kuwapangusha watu. Ila siyo kuibiana mchana kweupe kupitia hizi sheria zao za kipuuzi.
Upo sahihi
 
Umeandika kweli tupu.Matajiri wengi hawajengi ghorofa,nyumba ya kuishi.Wanapenda nyumba za chini ns za uhakika.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
... duh! Kwamba maskini ndio huporomosha maghorofa? Vyovyote vile, kwa mtazamo wa kitanzania hakuna maskini mwenye ghorofa ingawa ni kweli kwamba sio kila tajiri ana ghorofa.
 
Kigezo kikubwa tunachotumia wakadiria majengo ni ngazi, Kama kwenda kulala usiku lazima upande ngazi basi lazima 15 inakuhusu mkuu. Hata Kama unalala juu ya kontena chief.
ghorofa.jpg
 
Back
Top Bottom