Mzalendo_Mkweli
JF-Expert Member
- Jan 30, 2012
- 2,025
- 1,270
Habari wana JF,
Kuna gari langu la Suzuki Carry niliagiza toka Japani mwezi May mwaka huu na nikaliweka barabarani baada ya kwisha kulipia kodi zote. Hivi majuzi gari langu lilikamatwa na watu wa TRA wakishirikiana na Majembe Auction (Wazee wa kazi) wakidai sijalikatia kodi ya mapato. Wazee wa Majembe waliweka katika yard yao na siku iliyofuata nilireport TRA Chang'ombe kupewa maelezo ya kina ambapo niliambiwa natakiwa nilipe shs 450,000 kama kodi ya mapato ya gari na dereva kwa mwaka.Baada ya mvutano mrefu nililipa kodi husika katika Bank wanayotumia na kuwaletea nakala ya stakabadhi husika halafu wakatoa notice ya gari langu kuachiwa. Katika hii Scenario naomba mnitoe ushamba kidogo kwa kunijibia maswali yafuatayo:-
1. Hii ya kodi mpya ya mapato mbona nijawahi kuiona au kuisikia kupitia Government Notice (Gazeti)
2. Hivi mtu akiwa na Suzuri carry yake nyumbani kwa ajili ya shughuli ya kifamilia anatakiwaje kulipa kodi ya mapato?
3. Kama hii kodi tajwa ni halali, je kuna yeyote aliye na ufahamu mpana utufumbue macho wengi wetu?
4. Idd mbaraka kwa wahusika wote
Nawakilisha
Kuna gari langu la Suzuki Carry niliagiza toka Japani mwezi May mwaka huu na nikaliweka barabarani baada ya kwisha kulipia kodi zote. Hivi majuzi gari langu lilikamatwa na watu wa TRA wakishirikiana na Majembe Auction (Wazee wa kazi) wakidai sijalikatia kodi ya mapato. Wazee wa Majembe waliweka katika yard yao na siku iliyofuata nilireport TRA Chang'ombe kupewa maelezo ya kina ambapo niliambiwa natakiwa nilipe shs 450,000 kama kodi ya mapato ya gari na dereva kwa mwaka.Baada ya mvutano mrefu nililipa kodi husika katika Bank wanayotumia na kuwaletea nakala ya stakabadhi husika halafu wakatoa notice ya gari langu kuachiwa. Katika hii Scenario naomba mnitoe ushamba kidogo kwa kunijibia maswali yafuatayo:-
1. Hii ya kodi mpya ya mapato mbona nijawahi kuiona au kuisikia kupitia Government Notice (Gazeti)
2. Hivi mtu akiwa na Suzuri carry yake nyumbani kwa ajili ya shughuli ya kifamilia anatakiwaje kulipa kodi ya mapato?
3. Kama hii kodi tajwa ni halali, je kuna yeyote aliye na ufahamu mpana utufumbue macho wengi wetu?
4. Idd mbaraka kwa wahusika wote
Nawakilisha