Kodtec Speaker systems

Ha ha sidhani kama ni hio ambayo naisemea hapo πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚! Hio nayoisemea hapo imekaa vizuri sana yani. Ina mvuto flani wa kibabe.

Hio ya pichani hukuipata?
 
Kwa bi mkubwa alitaka radio tukaenda mchukulia ilikuwa laki na nusu 2013 hadi sasa haijawahi kufa na iko njema sana yani for the price na mdundo unaotoka ni nzuri sana


Haina Bluetooth ila ile hata exchange na toleo jipya tena iwe mpya na BT juu sitaki...

Huwa inatetemesha vioo vyote hadi nje chooni ukiacha mlango wazi bati la toi lina vibrate
 
Me huwa naangalia thamani na pesa na ninachokipata ,,

Mfano ile seapiano kwa bei la laki na nusu kwa sauti ile ..spika la bass watts 80 inch 8 ....

Ukiwaza mahesabu ya kutengeneza wewe itakucost zaidi ila unapata vyote just plug in and play kwa laki na nusu ni pesa ndogo sana huu unaenda mwaka wa nane ...na ilikuwa inapiga mziki muda mrefu sana hadi sink lake linachemka ila hakuna kinachoharibika


Svs nimeshasikia sehemu ila sijajua kwann wanauza ghali vile labda zinatoka nchi ya mbali sana sijui ila kwa 1.3M ni pesa nyiΓ±gi sana kwa sauti ile tena ni sub tu spika ukatafute mwenyewe za sauti...hio pesa nikifanya custom yangu naweza pata zaidi ya hicho tena ikawa ni tetemeko kabisa
 
Kila mtu na anavyotumia kichwa chake, mimi binafsi sijafikia level ya kununua subwoofer 1.3M! For the price labda niwe nimepata full set of speakers na AMP ya kudrive hizo speakers. Atleast 5.1 System ya adabu 😁😁😁!

Sea Piano ni brand imara kwa wale wanaotaka mziki kwenye tight budget. You will never get full range sound dynamics in it ila atleast lina mziki uliobalance kwa wasikilizaji wa kawaida.
 
Hahahah mie sikufichi, we pita kwenye stores zao Pale Mlimani City hakikisha una playlist yako freshi then Omba kutestiwa hiko kinu [emoji23][emoji23][emoji23] kwanza. Bank hazipo mbali pale utaenda tu mwenyewe kaka kuchomoa noti!
Mkuu kwa A.Town(Arusha) naupata wapi huu mkito heavy?
 
Tuma picha basi tuione mkubwa
 

Kuna kipindi nilikua mkoa flani nikawa sina radio one day nilienda sehemu nikakuta ka sub kadogo ila kana sauti ambayo haiendani na size yake...nikacheki model ilikuwa aborder 3119BT nikaenda mjin tafuta nikakosa nikakuta 3119BH muuzaji akanambia hii ni update ya ile BT ..nikachukua

Ina sauti nzuri iliochujika huwezi amin ina sound poa sana kuliko lg HT ya 300w ...kuna mtu alikua anayo hata nyimbo zikipigwa kwenye tv hazivutii ila kwenye ile ki aboda na bei yake ati 95k kipindi ile 2017 ndo Ilikuwa bei hio ni hatari...udogo wake sauti yake pale niliwapongeza wakat nanunua sikutegemea nilikuwa najua itakuwa kama vile vi sub vya elf 70
 
Mkuu naona umeamua kuwa wakala wa kodtec music maana naona unafanya promo kwa nguvu sana.

Kusema ukweli hapo hamna mziki zaidi ya kelele tu, yaani ni sawa na Sea Piano baada ya mwaka au miezi itaanza kukoroma.
Ipi sasa inafaa ? kama na sea piano inaiponda ?, tushauriane maana nataka kwenda kununua moja.
 
Yah unajua kuna mambo mawili. Kuna RMS wattage na Peak Power wattage.
Ni sawa na gari inaweza kuwa na RPM mpaka 8 ila region inayotumika ni 1-6 ila ukifloor Accelerator inaweza ikafika 8 mara moja kisha ikarudi 2...3...4...mpaka 6. Ndio namna hio hio ambapo redio zinafanya sasa wauzaji wanapendaga kuweka ile Peak Power Output kwenye Advertisement ila kimsingi sio kwamba mziki unakuwa na output hio.
Real 1000Watts za RMS pengine utakuwa unafanania na mziki kama wa Fiesta Ule. Mara nyingi miziki ya P.A ndio inagonga hio figure.
Kwa hometheatre hizi kupata real value chukua ile namba ya kwenye box gawanya kwa 4 ndio utapata Watts in RMS. Mfano uhalisia wa 1200watts ni kama 300Watts RMS.
Sasa kwa kale kadude ka LG 300watts ni P.M.P.O. inamaana gawa kwa 4 utapata Real Power ya speaker zote ni jumla ya 75watts hapo ukianza kugawa kwa 5 tena utakuta kale ka woofer ka LG kana almost 20watts of Real Power.(RMS)

Ila Ma subwoofer ya kichina yana RMS value, kwahio unakuta likiandikwa 150 watts ni za uhakika...Sub inakula 100watts satellite speakers 25w X 2!

Ndio maana unakuta subs la kichina lina watts 60 tu ila linapiga kuliko 300watts za LG.
 
Yeah kale ka box cha lg HT ya 300w inalingana na kale cha aboda na zina share spika size hio sub
 
Extrovert
Embu pata wasaa tafuta na hili dude la zamani kidogo hapo mlimani au kokote unakojua


 
Hili nilishalisikia dundo lake kipindi ndio namaliza form four nina mwanangu kwao walikuwa nalo tukawa tunajiachia nalo na mangoma ya kina Lil Weni πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…!

Mshindo wake unangurumisha bati na makabati ya vioo πŸ˜…
 
Hili nilishalisikia dundo lake kipindi ndio namaliza form four nina mwanangu kwao walikuwa nalo tukawa tunajiachia nalo na mangoma ya kina Lil Weni πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…!

Mshindo wake unangurumisha bati na makabati ya vioo πŸ˜…
Ili ukiweka ngoma za shaggy hakika huo si mchezo hahaha, naruka na madogo dansoooo au Madanso hahaha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…