Mkuu wewe furahia tu mziki wa Koffi. Kwa sisi wa enzi hizo tunajua huwezi kuwaweka chungu kimoja hao ulio wataja na Luambo. Franco Luambo Makiadi ni habari nyingine kabisa-ukiongelea muziki wake unaongelea muziki wa TP OK Jazz huenda ikawa bendi bora zaidi kutokea CONGO na Africa kwa ujumla. Hiyo ndio bendi ya Vicky Longomba, Poete Lutumba Simaro, Commandant de Bord Josky Kiambikuta, Ntessa Dalienst, Ndombe Pepe, Sam Mangwana, Madilu System, Djo Mpoy, Kiwakana Aime, Checain Lola Djangi kukutajia wachache. Miaka ya 1980 kwa mfano TP OK Jazz ilikuwa na wapiga solo (5) Franco, Papa Noel, Thierry Mantuika Kobi, Gerry Dialungana Kasia, Dizzy Mandeku-sikiliza nyimbo za wakati huo au wasome hao jamaa kwani wote ni who is who kwenye muziki wa Zaire. Luambo ni mwanamuziki wa kwanza kujengewa SANAMU "monument" huko CONGO miaka 26 bada ya kufariki na kufanyiwa international conference ya kujadili muziki wake. Luambo ana kitu inaitwa "OK Jazz School of Music". Kabla ya Tchacho ujuwe kulikuwa na Rhumba Odemba ambayo bado ipo ndani na nje ya Congo. Kuhusu gitaa ya Franco check hii youtube na pia google "Syran Mbenza & Ensemble Rumba Kongo: Immortal Franco: Africa's Unrivalled Guitar Legend" Kuhusu maisha ya Franco check hiki "Congo Colossus: The Life and Legacy of Franco & OK Jazz Paperback – January 4, 1994 by Graeme Ewens (Author)"
Wikipedia wanasema "
François Luambo Luanzo Makiadi (6 July 1938 – 12 October 1989) was a major figure in 20th-century
Congolese music, and
African music in general. He is widely referred to as
Franco Luambo or, simply,
Franco. Known for his mastery of
rumba, he was nicknamed the "Sorcerer of the Guitar" for his seemingly effortless fluid playing. As a founder of the seminal group
OK Jazz, he is counted as one of the originators of the modern Congolese sound."
Sikatai Koffi yuko vizuri sana lakini ukimuweka yeye na Luambo ni sawa na mzee Mwinyi alivyosema "Nyerere ni Kilimanjaro na yeye ni kichuguu". Mkuu furahia Tchacho.