Koffi Olomide ndio msanii bora wa muda wote kutoka Congo

Koffi Olomide ndio msanii bora wa muda wote kutoka Congo

Inaitwa Maggie, ilikuwa ni moja ya hit song iliyofanywa na Koffi Papaa Mopao akishirikiana na kundi lake la Quartier Latin na ndo ilibeba jina la album iliyotoka 1994.

Koffi ni moja ya wasanii ninao wahusudu sana ktk anga za music duniani. Tangu nipo vidudu (nursery) mpaka leo hii nipo kazini huyu mzee bado anatoa pini tu na zote ni moto!!!


Sent using Jamii Forums mobile app
Magie ilitoka nadhan1992, na 1994 ni albamu ya V12 ikiwa na wimbo kama Andrada.
Kiujumla Koffi Olomide kadumu sana kwenye muziki akiwa juu, albamu zake kama Loi, Rondpoint aliyowadis Zaiko, Attetant, Force de Frape, Effrakataa, Affaire de etate(kwangu mm ndiyo albamu bora ya muda wote ya Koffi inanyimbo kali sana), Monde arabe (2nd best albam) na Danger de Mort.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wewe furahia tu mziki wa Koffi. Kwa sisi wa enzi hizo tunajua huwezi kuwaweka chungu kimoja hao ulio wataja na Luambo. Franco Luambo Makiadi ni habari nyingine kabisa-ukiongelea muziki wake unaongelea muziki wa TP OK Jazz huenda ikawa bendi bora zaidi kutokea CONGO na Africa kwa ujumla. Hiyo ndio bendi ya Vicky Longomba, Poete Lutumba Simaro, Commandant de Bord Josky Kiambikuta, Ntessa Dalienst, Ndombe Pepe, Sam Mangwana, Madilu System, Djo Mpoy, Kiwakana Aime, Checain Lola Djangi kukutajia wachache. Miaka ya 1980 kwa mfano TP OK Jazz ilikuwa na wapiga solo (5) Franco, Papa Noel, Thierry Mantuika Kobi, Gerry Dialungana Kasia, Dizzy Mandeku-sikiliza nyimbo za wakati huo au wasome hao jamaa kwani wote ni who is who kwenye muziki wa Zaire. Luambo ni mwanamuziki wa kwanza kujengewa SANAMU "monument" huko CONGO miaka 26 bada ya kufariki na kufanyiwa international conference ya kujadili muziki wake. Luambo ana kitu inaitwa "OK Jazz School of Music". Kabla ya Tchacho ujuwe kulikuwa na Rhumba Odemba ambayo bado ipo ndani na nje ya Congo. Kuhusu gitaa ya Franco check hii youtube na pia google "Syran Mbenza & Ensemble Rumba Kongo: Immortal Franco: Africa's Unrivalled Guitar Legend" Kuhusu maisha ya Franco check hiki "Congo Colossus: The Life and Legacy of Franco & OK Jazz Paperback – January 4, 1994 by Graeme Ewens (Author)"
Wikipedia wanasema "

François Luambo Luanzo Makiadi (6 July 1938 – 12 October 1989) was a major figure in 20th-century Congolese music, and African music in general. He is widely referred to as Franco Luambo or, simply, Franco. Known for his mastery of rumba, he was nicknamed the "Sorcerer of the Guitar" for his seemingly effortless fluid playing. As a founder of the seminal group OK Jazz, he is counted as one of the originators of the modern Congolese sound." Sikatai Koffi yuko vizuri sana lakini ukimuweka yeye na Luambo ni sawa na mzee Mwinyi alivyosema "Nyerere ni Kilimanjaro na yeye ni kichuguu". Mkuu furahia Tchacho.
Luambo ni 2nd generation na Koffi ni 3rd Generation ya Music wa Congo, hapo vionjo lazima viwe tofauti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tuweke record sawa, Ferre gola hajatolewa na Koffi, Fere ni zao la Werrason. Ferre ameenda QLI akiwa tayari na heshim yake nzuri tu kuliko fally... nyumbo kama Vita Imana tayari zilikuwa zimeshamfanya imjue Herve ni nani...
Papaa Mopao,, kiukweli huyu jamaa anastahili sifa zake.
Toka nimeanza kuifahamu albamu yake 'Maggie' na kundi la Quartier Latin enzi nikiwa nimeanza shule ya msingi miaka ya 1995 mpaka leo hii bado jamaa yupo ktk ubora wake ule ule.

Kundi lake la Quartier Latin ambalo liliasisiwa kitambo hicho 1986 limetoa wasanii wengi sn wanaofanya vizuri kama Fally Ipupa, Ferre Golla nk ambao kwa sasa hawapo tena kundini, ila cha kufurahisha zaidi ni ule upendo na ushirikiano wanaoendelea kuoneshana baina yao kwa mfano mwaka 2016 Fally Ipupa aliorganize tamasha la 30th Annivessary ya lililokuwa kundi lao la Quartier Latin wasanii wengi waliopitia kundi hilo akiwemo the founder himself Papaa Mopao alishiriki vizuri sana.

Ila Koffi Olomide Ngoma zake za miaka ya hivi karibuni 'Abracadabra' na 'Danger De Mort' nazikubali sana!!
 
tuweke record sawa, Ferre gola hajatolewa na Koffi, Fere ni zao la Werrason. Ferre ameenda QLI akiwa tayari na heshim yake nzuri tu kuliko fally... nyumbo kama Vita Imana tayari zilikuwa zimeshamfanya imjue Herve ni nani...
Tuweke sawa record Mkuu, Ferre Gola ni zao la Wenge Musica na sio Werrason.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Leo acha niseme ukweli wakuu,watu wanapenda kutompa mtu sifa zake mpaka afe.
Toka kizazi cha kina Lwambo mpaka sasa kina ferre na fally hakuna msanii wa kumlinganisha na koffi kimuziki apo Congo.Sema watu wanapenda kutukuza vitu vya kale kama kwenye mpira wanavyompaisha Pele na Maradonna wakati messi na Ronaldo wamefanya mengi makubwa tu.

Sasa basi hata kwenye mziki,utasikia sijui Madilu,Papa wemba sijui nani.Ndio wametoa nyimbo kali sana lakini hakuna aliefanya consistency ya nyimbo nyingi kuwa juu kama koffi.
Hata huyo Werrason bado anapaishwa tu kwa nyimbo chache ukifananisha na Koffi.

Tukubali tu wakuu hakuna kama Koffi kwenye muziki wa boringo.
Hapana si kweli kabisa huyu hata Pepe Kalle hamkuti kabisa kabiaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kweli koffi olomide papa fololo hana mpinzani.hao kina franco,pepe kale,papa wemba hawamfikii kidogo labda kama utakua umeamua kubisha.kipaji cha koffi toka dunia iumbwe hakuna aliyekifikia kwa upande wa sekta yake.ultimutum ni moja ya nyimbo bora,akadabra,tsou tsou,selfie aisee huyu jaamaa aishi miaka mingi kila nyimbo yake kali nikisema niorodheshe nitakesha.mopao mokonzi,papa mourinyo,quarda kora man namkubali sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo acha niseme ukweli wakuu,watu wanapenda kutompa mtu sifa zake mpaka afe.
Toka kizazi cha kina Lwambo mpaka sasa kina ferre na fally hakuna msanii wa kumlinganisha na koffi kimuziki apo Congo.Sema watu wanapenda kutukuza vitu vya kale kama kwenye mpira wanavyompaisha Pele na Maradonna wakati messi na Ronaldo wamefanya mengi makubwa tu.

Sasa basi hata kwenye mziki,utasikia sijui Madilu,Papa wemba sijui nani.Ndio wametoa nyimbo kali sana lakini hakuna aliefanya consistency ya nyimbo nyingi kuwa juu kama koffi.
Hata huyo Werrason bado anapaishwa tu kwa nyimbo chache ukifananisha na Koffi.

Tukubali tu wakuu hakuna kama Koffi kwenye muziki wa boringo.
From NOBLESSE OBLIDGE to XXXX.
 
Luambo ni 2nd generation na Koffi ni 3rd Generation ya Music wa Congo, hapo vionjo lazima viwe tofauti

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu afadhali wewe umeliweka hili kwa njia tofauti, lakini kuna mtu humu alimlinganisha Franco-Le Grand Maitre Franco tena akuita mkulima-yaani akimlinganisha na Koffi anaona Franco ni mkulima tu. Haya ni matusi makubwa na ndio nikamjibu hivyo. Wadogo zetu saa nyingine wanazidisha mahaba.
 
Mkuu afadhali wewe umeliweka hili kwa njia tofauti, lakini kuna mtu humu alimlinganisha Franco-Le Grand Maitre Franco tena akuita mkulima-yaani akimlinganisha na Koffi anaona Franco ni mkulima tu. Haya ni matusi makubwa na ndio nikamjibu hivyo. Wadogo zetu saa nyingine wanazidisha mahaba.

Watu watambue kuwa Franco pamoja na kuwa walikuwa na kundi moto vilevile Rais Mobutu Seseseko Wazabanga alimbeba sana katika kumfanya afahamike mataifani. Ukirudi kwa Koffi Olomide nae alipigana sana kusimama kivyake mkumbuke kuwa miaka ya zamani ilikuwa ngumu kwa kijana mdogo usimame peke yako na kutengeneza kikundi cha muziki, na ndo maana ukiangalia sana wanamuziki wengi walikuwa hawampendi Koffi, na yeye alilitambua hilo, hata matamasha yake kadhaa ulaya na Zaire enzi zile yalihujumiwa sana, lakini hakukata tamaa na akasimama na hadi leo anatisha. Koffi Olomide anakubalika sana nje ya Congo
 
Mkuu afadhali wewe umeliweka hili kwa njia tofauti, lakini kuna mtu humu alimlinganisha Franco-Le Grand Maitre Franco tena akuita mkulima-yaani akimlinganisha na Koffi anaona Franco ni mkulima tu. Haya ni matusi makubwa na ndio nikamjibu hivyo. Wadogo zetu saa nyingine wanazidisha mahaba.
Mkuu usitumie nguvu nyingi kubishana na hivi vitoto vya miaka ya 90. Yani mtu anasikiliza masebene ya koffi olomide akiwa bar halafu anadiriki kuja huku na kumfananisha na Franco!?!! Seriously??? HAYA NI MATUSI MABAYA SANA.
Mungu na awasamehe bure.
Koffi olomide ni msanii mkali sana dunia hii lakini kwa Franco haifikii hata 0.000001 level zake ni za kina hao Jb mpiana, sijui ferre Gola na yule mfanyakazi wake wa zamani aitwae Ipupa.
Mtu akiendelea kumdharau Franco namporomoshea matusi mazito sana hadharani.
 
Watu watambue kuwa Franco pamoja na kuwa walikuwa na kundi moto vilevile Rais Mobutu Seseseko Wazabanga alimbeba sana katika kumfanya afahamike mataifani. Ukirudi kwa Koffi Olomide nae alipigana sana kusimama kivyake mkumbuke kuwa miaka ya zamani ilikuwa ngumu kwa kijana mdogo usimame peke yako na kutengeneza kikundi cha muziki, na ndo maana ukiangalia sana wanamuziki wengi walikuwa hawampendi Koffi, na yeye alilitambua hilo, hata matamasha yake kadhaa ulaya na Zaire enzi zile yalihujumiwa sana, lakini hakukata tamaa na akasimama na hadi leo anatisha. Koffi Olomide anakubalika sana nje ya Congo
Mkuu naona unamshusha Franco kwa style fulani hivi. Kundi hilo la moto unalo lizungumzia ni kazi halisi ya Francois Luambo na Victor Longomba walilijenga toka chini. Pili Mobutu alikuwa FANATIC wa OK Jazz hapo aliposhika madaraka 1965 Franco na OK Jazz walikuwa wameshajipanga na kufahamika hata nje ya Congo (East, Central and West Africa). Sisi tulicheza sana kitu inaitwa Polo na Bolingo ya Bougie enzi hizo. Mobutu alichofanya kwa sababu alikuwa FANATIC wa Luambo alimwambia tukiwa pamoja utafika mbali.
Sina nia ya kumshusha Koffi hivyo sitamzungumzia sana ninachosema ni hiki hawa "Franco na Koffi" si watu wa kulinganishwa, Franco alikuwa a Musical Genious.
 
Back
Top Bottom