Mkuu naona unamshusha Franco kwa style fulani hivi. Kundi hilo la moto unalo lizungumzia ni kazi halisi ya Francois Luambo na Victor Longomba walilijenga toka chini. Pili Mobutu alikuwa FANATIC wa OK Jazz hapo aliposhika madaraka 1965 Franco na OK Jazz walikuwa wameshajipanga na kufahamika hata nje ya Congo (East, Central and West Africa). Sisi tulicheza sana kitu inaitwa Polo na Bolingo ya Bougie enzi hizo. Mobutu alichofanya kwa sababu alikuwa FANATIC wa Luambo alimwambia tukiwa pamoja utafika mbali.
Sina nia ya kumshusha Koffi hivyo sitamzungumzia sana ninachosema ni hiki hawa "Franco na Koffi" si watu wa kulinganishwa, Franco alikuwa a Musical Genious.