Kombe la Cecafa Senior Challenge 2009

Maximo Maximo Maximo Maximo! ndivyo ulivyokua unashangiliwa ushindi wa Zanzibar! Hii ikiashiriwa kuwa sasa watz wamemchoka mwalimu huyu! katika muda wa miaka minne ameshindwa kuwa na kikosi cha kwanza kwa muda mrefu!
 
Ile freekick ilikuwa kali hata Maximo angekuwa kipa bado angefungwa tu huo ndo ukewli!
 
Eei nilikuwa nimalizie Xmass ndio niibuke tena hapa JF ,lakini ulipangalo silo alilokuekea Mwenyezi Mungu,ni baada ya kusikia Zanzibar imetoa kipigo cha paka mwizi.
Yaani huku kwetu tunamsemo unasema kupuruzia na pale mwanzo tuliwapuruzia angalau mpate kuvuka na hamkuwa na fadhila ,maana kumbe hata nchi mnayowakilisha haipo ,sielewi mmetokea nchi gani ,yaani mmeingia katika mashindano ya watu kinyemelanyemela na kutaka kujifanya mnajua kucheza kuliko watu wenye nchi zao.
Sasa hata ushindi wa tatu mmeukosa na mnarudi mlikotoka sijui mmetoka wapi.Nasikia ni kutoka Tanzania ila nijuavyo Tanzania ni Muungano wa nchi mbili moja ikiwa ipo na ingine imefulia tokea miaka ya sitiini.
Hivyo ile haki ya nyie kushiriki katika kombe hilo hamna kabisa na ushindi mliopata ungeweza hata kukatiwa rufaa ,isipokuwa huruma tu ndio zimewakumba kama waliotoka kwenye mafuriko.
Mara ingine msishiriki katika mashindano ya watu wenye nchi zao ambazo zipo hai na zitaendelea kuwepo.Kwanza ni aibu kushiriki mnadusa katika mambo ambayo nyie hayawahusu.
Zanzibar imetoa somo kubwa sana na itabidi kwanza mujiulize Zanzibar imeifunga nchi gani ? Ndio muweze kujibu hii hoja kama haitoshi muulizeni Pinda hivi nyie mukiwakilisha nchi gani na katika kugombea mshindi wa tatu ni nchi gani iliwafunga ,Je hii ni nchi ? Mbona imetufunga nje ya mipaka ya Tanzania na wewe ulisema si nchi nje ya mipaka ? Lazima atakwambieni Kikwete ndie aliesema hivyo.
 
teh teh teh, soka la bongo ndio lilivyo...
 
Kwa hiyo sisi wa Tanganyika ndiyo unatuita "Machogo"? Nini maana ya neno hili? kama hutamind kutufahamisha.
 
There was a time niliandika kwenye gazeti la Mwananchi kuelezea ni kwanini watanzania hufika mahali fulani wanaamua kuizomea Kili Stars. Na nikaelezea ni kwanini Maximo hafai kufundisha timu yetu ya taifa, lakini baadhi ya watanzania walinishutumu kwamba nimemtukana mwalimu wao, mteule wa rais. Napata shida sana ninapoona kwamba yale ambayo niliandika watanzania wakanipinga, hivi leo yanaitafuna nchi. Kwa ujumla, Maximo si Mwalimu anayepaswa kuifundisha Taifa stars. Tunatumia pesa nyingi za walipa kodi kumlipa mshahara mnono, hatuoni chochote. Angekuwa Simba au Yanga angeshafukuzwa siku nyingi. Sijui huyu Kikwete alikula kiapo gani na Maximo. Tunaweza kumnyima kura Kikwete kwa ajili ya upuuzi huu. Amfukuzie mbali, tutafute kocha mwingine.
 
Yah sie huku Zenji tunandaa mishumaa ya kuwapokea mashujaa wetu kwa kutoa kichapo
 

heheheheeeeeeeeeeeee

nimefurahi sana na kijembe hiki kinachoakisi uzito wa baadhi ya akili kuelewa mambo!

kwa kukusaidia mkuu, sio nchi zilizoshindana na kama zingekuwa nchi, zanziba isingeruhusiwa kushiriki. zilizoshingana ni timu zinazoidhinishwa na vyama wanachama wa cecafa!

muhidini ndolanga alikuwa mwerevu sana wa mambo ya soka ndoio maana akina kapuya na uprofesa wao walichemsha. walikuwa na akili kama hizi wakifikiri fat ilikuwa idara ya serikali umbe kilikuwa chama kilichundwa na wadau, kikiwa huru na kwa uhuru kiliomba uanachama katika chama kingine huru cha fifa na kukubaliwa hivyo serikali haina uhalali wa kuingilia mambo ya soka kama serikali, bali inaweza kushauri tu kama wadau wengine.

sasa wewe mzenji, ni kuwa zanziba si nchi, ilijinyonga yenyewe tangu 1964, hiyo ilyoshiriki mashindano si timu ya taiifa ni timu ya mkoa wenye uanachama wa cecafa! kuhusu kushinda ama kutoshinda, siku zote ni dakika 90 ndizo huamua! hujasikia mabingwa wa ligi kuu ya nchi ya tz yanga imefungwa na timu ya daraja la kwanza tmk united? hiyo ndo soka, hakuna cha ajabu.

asiyekubali kushindwa si mshindani, hongereni sana wakubwaaaaaaaaa kwa ushindi ila mtuombee tuepushwe na mwalmu wa nidhamu(discipline master) wa timu yetu, maximo. mtuombee angalau nasi tupate mwalimu wa mpira hata kama ni mzawa. maximo alituzuga kuwa amekuja kufundisha mpira, kumbe amekuja kufundisha nidhamu! na jk anavyomtetea, nadhani naye ameishakuwa mwanamtandao!!!!!!!!

Mungu ibariki tanzania
 
Habari za uhakika nilizopata hivi punde leo Maximo ameweza kuiandikia timu ya taifa historia nyingine
ya kufungwa na Zanzibar!
Kila siku nilikuwa namtetea MAKIZIMO, lakini kwa kufungwa na hawa rojorojo ITS TIME FOR HIM 2 GOOOOO.Aondoke now more than later,uwezo wake umeishia hapa,tunataka kocha mwingine wa kuendeleza alipoishia.
PERTITION:
MAXIMO MUST GOOO NOW!!!!!!!PLZZZZZZZ!
 
Nyinyi hamzijui fitina za wa "upande wa pili wa Muungano". Hata mapinduzi yenyewe yalipatika kwa fitina!. Hapakuwa na mtu mwenye nguvu ya kupingana na Utawala wa Usultan enzi hizo kama si fitina!, Kinyekitile na majimaji cha mtoto kule,.....ni Mchezo ulikwisha chezwa Kiembe samaki one wiki b4 na leo ililikuwa kiini macho tu! KaMa hata mguu pande na sawa ni legeza, soka wapi na wapi??
 

Tenda watu wataona majisifu weka kando.(mtaka unda haneni)
 
Tovuti ahsante kwa kumjibu Bubu,hilo ni jina la utani katika mambo ya kisiasa na kimichezo kwani si mlituita vibua mlipotufunga mmesahau kama usitukane wakunga na uzazi ungalipo sasa tumewazalisha ila ndio hivyo.

Mgombea Ubunge kama utasafiria dau hilo ubunge utaukosa ,unasema timu haya tuchukulie timu, hizo timu zinatoka nchi gani ? Je kuna uwezekano wa kuishirikisha au kushiriki kwa Simba au Yanga .JKU au Jamhuri katika mashindano hayo naona lipo kombe la washindi na Zenji nao wanatoa yao ? Hata kwenye kombe la dunia Zenji nao wanashiriki fitina zenu ndio ziliwaharibia lakini kwa kisago hiki naona ujumbe utakuwa umefika FIFA.
Hapa nahitaji mumuulize Pinda mmefungwa na nchi gani ?
 

Furahia ushindi wako ndugu lakini acha chuki,sie ndugu hata iweje.huu ulikuwa mchezo na kama unavyojua katika soka kila kitu kinawezekana,hakuna haja ya kuitana machoko wala nini.HONGERA KWA USHINDI NA WEKA CHUKI PEMBENI.........
 

we mzenji mbona huelewi? hakuna nchi mwanachama wa fifa, caf, cecafa wala uefa. wanacham huko ni vyama vya michezo tu, full stop. chukulia mfano wa muungano wa uingereza, ennland, scotland na ireland wote wana uanachama fifa na uefa. ndio maana hata siku moja huwezi kusikia timu a united kingdom imefuzu kucheza fainali za kombe la dunia, au euro, siku zote utasikia england, scotlandau ireland zimefuzu!!!!

hilo swali ni dogo sana kwa mkubwa pinda, kama hujanielewa basi labda maximo ndiye wa kujibu zaidi
 
Kwa hiyo sisi wa Tanganyika ndiyo unatuita "Machogo"? Nini maana ya neno hili? kama hutamind kutufahamisha.


Mbona hilo jina lakiutani na lipo miaka mingi tu kwa ufahamu wangu mimi tokea miaka ya 70 tena lilikuwa linatumika sana ni hivi miaka ya karubuni ndio limepoteza umarufu wake sawa na kuwaita wazanzibari mayakhe au majina mengine amabyo yalikuwa yanatumika kiutani sio jina jipya ua vyenginevyo ,inaoneka Babu ataka kusema wewe ni mgeni wa Dar wala usibishane .au umezaliwa wakati wa mzee Ruksa.
 
maximo amekuwa mswahili nae siku hizi. Pamoja na kuwa mcheza sinema pia ni mwalimu wa nidhamu.

Poleni sana Wabara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…