Kombe la dunia ndo lilelile la miaka yote?

Kombe la dunia ndo lilelile la miaka yote?

mussa victor

Senior Member
Joined
Jul 12, 2015
Posts
116
Reaction score
163
wakuu naomba mnitoe matongotongo hivi lile kombe la dunia ndio lile lile miaka yote au huwa wanatengeneza baada ya miaka 04 maana jana nilimuona nahodha wa ujerumani mmoja ya washindi wa kombe la dunia 2014 akikabidhi kombe hilo kwa ufaransa hapa ndipo nilichanganyikiwa je kombe ndio hilo linazunguka mnakaa kaa nalo kwa muda baada ya 4 years mnaliachia? maana mbona sisi bongo mfano simba makombe yake yote yapo msimbazi. Please mnidadafulie
 
Nimesoma kwenye mitandao maana swali lako nami limenifanya niwe mdadisi:
Kwa jinsi nilivyoelewa, vikombe hivi toka kombe la dunia limeanza ni 2 tu vimetumika.
Zamani kabisa toka kombe laanza mpaka miaka ya 1970 walikuwa wanatumia kombe tofauti na la sasa. Waliliita Jules Rimet Cup. Kimuonekano kilikuwa pia tofauti na hiki cha sasa. Kikombe hiki kilichukuliwa na brazil moja kwa moja kwa sheria za zamani kwamba ukishinda mara 3 unakichukua moja kwa moja. Kikombe hiki kikiwa huko makumbusho ya brazil kiliibiwa ikabidi watengeneze cha bandia na kukiweka makumbusho.

Baada ya hapo lililopo sasa ndio lilianza tumika. Mpaka 2006 bingwa alikuwa akikabidhiwa anakaa nacho mpaka mashindano yajayo. Ila siku hizi wamebadilisha, bingwa anakabidhiwa uwanjani kombe original, ila akiondoka uwanjani anatengenezewa replica, yaani kopi ya lile origina. Lenyewe linakuwa gold bronze plated.

CHECK LINK HII, KWA MENGINE ZAIDI. .
 
safi mkuu mm nilikuwa sijui chochote though nishabiki ndaki wa mpira
 
Back
Top Bottom