Makamu Mwenyekiti wa CCM, Komredi Abdulrahaman Kinana amewataka wabunge kuwa wakali na mambo ya wananchi na kuiwajibisha Serikali.
Kauli hii ya Mzee Kinana inatafsiri gani katika kipindi hiki ambacho Bunge linatupiwa lawama na wananchi kwa kupitisha tozo za simu, tozo katika miamala ya kibenki pamoja na kubariki mipango mbalimbali ya Serikali iliyosababisha hali tulionayo sasa.
Pia usimamizi mbovu wa wabunge katika kuibana Serikali na kusababisha wananchi kukabiliwa na mfumko mkubwa wa bei za bidhaa kutokana na wabunge kushindwa kuiwajibisha Serikali.