Konde Gang yawaaga rasmi Killy na Cheed

Slowly

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
10,589
Reaction score
35,268
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize amedhibitisha kuondoka kwa wasanii wake wawili Killy pamoja na Cheed.




Kufuatia tangazo hili, Cheed pamoja na Killy wamefuta post zote katika kurasa zao za Instagram.

Kwa upande wa Killy namkubali sana, nashauri aende wasafi. Anauwezo mkubwa sana wa utunzi wa mashairi, ila promo inamuangusha.

Ni wewe ft harmonize utabaki kuwa wimbo wangu pendwa.
 
Mungu awayangulie ameen inshalh 😆😆😆
 
Nami naunga mkono hoja, Kelly aende wasafi........si mwanachama wa hilo genge lkn aende pale atafanikiwa. Huyu bosi dogo wa kimakonde kila siku yupo na kajala.....watatayarishwa myda gani?!!!!!!
 
Kusimamia msanii mpaka anafika level ya kutambulika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania si swala dogo.

Inahitajika moyo, uvumilivu, kujitoa na uwekezaji mkubwa mno. Nawaonea huruma kwani wametoka ila still brand zao ziko vilevile. Hapa ndipo Mondi anapopewa heshima yake.

Killy anaweza kusurvive ila Cheed ni wa kawaida ila sijui huko mbele ya safari anaweza kuwa bora.
 
Madogo wa hovyo wasio na identity, walipokuwa KING’S wote walisaundi EEYOOO kama Kiba…. walipohamia Konde Gang wakasaundi kooh kooh oyaa oyooh wote kama Chinga!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…