Kongamano la akina Butiku na wenzie - kijiwe cha malalamiko

Hivi kuna ubaya gani katika kulalamika? Kuna ubaya gani kwa mtu kama Mzee Butiku na Warioba kumwambia Rais JK kwamba awe jasiri na kufanya maamuzi magumu hasa katika kusafisha CCM na Serikali yake. Kwamba Rais wetu amezungukwa na wafanyabiashara ambao wamemfanya mateka wao. Hivi kuna mtu mwenye akili timamu ambaye halioni hili? Kwamba anachotakiwa kufanya Rais JK ni kuwatema (to purge) hao ili CCM na Serikali virudi katika msitari. Nani asiyejua kwamba Serikali inashindwa kutekeleza kikamilifu maamuzi ya Bunge kuhusu Richmond kwa sababu ya hao wafanyabiashara waliomzunguka Rais wetu?

Kuna ubaya gani katika Mzee Butiku kutwambia kwamba watu wale wale waliogawa pesa kwa vijana wa CCM katika mchakato wa urais 1995(sio 2005) zilizotoka nje ya nchi bado wapo na walianzisha mtandao ambao ulimwingiza Jk Urais 2005 na kumtaka hauvunje? La sivyo kuna hatari huko mbele tuendako. Haya sio malalamiko bali ni WOSIA. Kama watanzania tuna utashi wa kusikiliza wosia huu na kukubali au kuukataa.

Binafisi mimi namliganisha mzee Butiku kama nabii. Kazi ya nabii ni kuhubiri na kutahadhalisha na manabii wengi walitahadhalisha lakini hawakusikilizwa matokeo yake majanga yakawapata hasa waisrael. Na sisi kama tusipomsikiliza huyu mzee na kumbeza eti alikuwa anamtaka Salim awe rais na hivyo apumzike akale pensheni ole wetu! Wenye masikio na wasikie.
 

Asante mkuu hapo umenena
 

Mkuu hapa mwendo mdundo tu kwani kila mtu anafahamu kuna mtu ilibidi aitwe Jumanne baada ya kwenda Iran kupewa cha kupewa
Sasa unganisha dot nani ana asili ya Iran kwenye inner circle ?
 
Sikubaliani kabisa na hiyo point ya kuwasema wale wazee ni spent forces. Usijenge point kuwapinga tu kwa kuwa ni wazee. Pinga point walizotoa.
Kuhusu JK kuwa ni wa dot com... mhh. The guy is not young!!
 
Labda sijamwelewa, alitaka Lowasa akaribishwe azungumze kwenye kongamano la kumbukumbu ya Mwaalimu? Ili aseme nini?

Ha ha ha kichekesho!!!!
 
Wakati mwingine huwa nashindwa kuelewa kama mtu kama huyu haoni kwamba TZ tuna tatizo?. Hivi ni nini hasa kinachomfanya muhusika aone ukweli unaosemwa juu ya uongozi katika nchi yetu unahitaji marekebisho. Eeeh Mungu tusaidie kwani yaelekea tuna safari ndefu.
 

Kwa jinsi ninavyoona Watz hawataki criticisms, wanataka sifa tu. Sijui wengine tumelelewaje? Mfano, washiriki wangeenda kwenye kongamano na kila mmoja kusifia jinsi madini yanavyonuifa taifa na kila Mtanzania anavyosonga mbele, hakuna rushwa/ufisadi na nchi yetu ni ya kidemokrasia na utawala bora (inaongoza Afrika), nk watu wengi wangewasifia sana. Lakini mimi najaribu kutumia hekima niliyojifunza kwamba hata kama kitu kinachosemwa ni upumbavu, kinakufunza kitu fulani.

Binafsi, naona kila aliyechangia amejitahidi kusema kilicho moyoni mwake na sisi tunaodai tunajua mstakabali wa taifa letu, mbona hatuuleti hapa JF tuuone. Ila wengine wakichangia tunasema hiki na kile na kisichokuwepo pia. Tuna shida sana!
 
Mkuu hapa mwendo mdundo tu kwani kila mtu anafahamu kuna mtu ilibidi aitwe Jumanne baada ya kwenda Iran kupewa cha kupewa
Sasa unganisha dot nani ana asili ya Iran kwenye inner circle ?


Ndie alikuwa kinara wa G55 mpaka Mwl.JKN akataka kuwarudishia card ya CCM pale Dodoma, Leo hii amejirudi na kuwa kundi la kupinga Ufisadi yeye na mke wake kule bungeni


 

Mbona nawe unalialia tu!

How sure are you kwamba Lowassa hakualikwa? Kama Sumaye aliweza kualikwa why not Lowassa. Kweli wakati mwingine inauma.

Vyovyote utakavyoukandia uongozi wa Mwalimu Nyerere you are waisting your breath and time! Mwalimu was the greatest in Africa and is an idol of Tanzanians today and tomorrow!

Hoja yako ya upendeleo imenikumbusha habari niliyowahi kuisikia kwa kusoma kwenye magazeti ama kwenye radio kwamba wakati mmoja Mwalimu (Mkatoliki) alishutumiwa kwamba anapendelea Wakatoliki, amejaza wakatoliki kwenye baraza lake la Mawaziri. Poor man, he was very innocent na wala hakuelewa kwamba mawaziri waliokuwa kwenye Baraza wanatoka kwenye madhehebu gani. Ikabidi amtume msaidizi wake Miss Joan Wicken (sio Butiku) amfanyie utafiti kujua ni Wakatoliki wangapi wako kwenye cabinet ile. Ikagundulika kwamba walikuwa wawili tu na Mwalimu wa tatu!!

Unataka kuniambia akina Samuel Sitta, Mzee Lusinde, Bomani, Malecela, Sokoine, Salim, Kaduma, Kawawa, Makweta, ....(Mawaziri) .... akina Siyovelwa, Natepe, Shindika, Mzenna, Mahiga, Kitine - (Usalama wa Taifa hao) ... akina Nkembo, Apiyo, Mulokozi Ernest na Bernard, Makatibu wakuu wa enzi hizo za Nyerere - the list is very long ya maafisa wa ngazi ya juu Serikalini enzi hizo je hao wote walikuwa true northerners! Mantiki ya kuwa na Wakurya jeshini inaeleweka - ni wapiganaji kwa kuzaliwa! Usingeliweza kumteua mkwezi wa minazi kwa Mkuu wa Majeshi!

Acheni uzushi usiokuwa na mantiki!
 

Mkubwa,

Mimi naona huo ndio msimamo wako na kwa hiyo you are entitled to your own opinions.

Ila tu fikiria kwa upande mwingine wa shilingi kuwa WE HAVE CREATED OUR OWN MONSTERS FROM DAY ONE MFUMO WETU WA UENDESHAJI NCHI ULIPOANZISHWA.Hapa nazungumzia enzi za Nyerere na awamu zilizofuatia.Tunayoyaona sasa yamezaliwa huko nyuma!Ukweli unabaki kuwa KAMWE HATUTAWEZA KUBADILI MFUMO WA SASA BILA YA SACRIFICE.Wengi tunakataa kukubali hili.Ukitaka yote haya yabadilike,everything MUST change!Tutaendelea kulia lia tu hapa.Tanzania ina uwezo kabisa wa kuwa moja ya nchi nzuri sana kiutawala KAMA mfumo mzima utaondolewa sasa hivi na watu wakajua kuwa THAT CHANGE IS CRUCIAL kwenye mustakabali mzima wa nchi!

Nawasilisha!
 

Msimamo wa ndugu ni wake lakini tuko wengi tunaoelewa matatizo ya enzi za Butiku na kuathiriwa na mfumo wa kiutawala uliokuwepo.Ni kweli enzi hzo Butiku alikuwa very powerful,jeshi lilkuwa chii ya mtu wa Butiama pia,BOT ilikuwa na mtu wa Tarime na hakuna ubishi kuwa ukabila ulikuwa mbele.

Kuwapo kwa makongamano kama hilo la Nyerere foundation ambayo huko nyuma hayakuruhusiwa ni ishara kuwa uendeshaji wa Serikali uko wazi sana kuliko nyakati zote zilizopita.

Hali kama hii ambayo kila mtu yuko huru kukosoa ilikuwa nadra enzi za Mwalimu na hata zile zilizofuatia.

Demokrasia imekuwa sana wakati wa JK na nina imani kuwa mfumo wa utawala utabadilika bila vitendo vya utumiaji nguvu.Mfano ni ule wa maridhiano kati ya Karume na Seif,bila hata kutumia wapatanishi kutoka nje.

Kila siku tunajionea hamasa za watu na contribution za kisiasa ambazo zina mwelekeo wa kukuza demokrasia.Kwa maoni yangu naona hata uchaguzi huu unaokuja tutaona mabadiliko makubwa bungeni.

Sacrifice ili mfumo ubadilike kwa maana ya kuchukua sheria mkononi hazifai ila mapambano ya kutafuta katiba mpya ili kubadili mfumo uliopo kwa kuwashirikisha wananchi kunaweza kuleta mabadiliko yanayotakiwa na wengi.

Ni jukumu la vyama vya siasa kudai katiba mpya kwa kuwaamsha wananchi kifikra.
 
Let's look at this piece in the true toe-to-toe Bluray tradition.

Amen.
 
Kama Serukumba na Masha ndio viongozi watarajiwa wa kizazi kijacho naomba Mungu ainusuru Tanzania.
 
Tatizo la akina Butiku wanadhani Nyerere Foundation ni kuhutubia maadili ya mwalim tu, hapana, they have to go further.

Mfano, ile foundation ingekua hata inatoa scholrships hata tano kwa elim ya juu Tanzania kuna tatizo gani?

Foundation ingekua inaandaa makongamano ya ukimwi, kansa, na hata haya mauaji ya albino, kuna tatizo gani?

Foundation inauwezao wa kutafta funds si lazima itegeemee 100 percent serikalini, kama kuna watu tu huko edinberg wameweza kuomba Mwali Nyerere scholarships kuwa offered, kwanini akina Salim washindwe?

Kuna mambo mengi jamaa wanatakiwa kufanya, lakini tatizo lao wao wanadhani kazi yao ni kuikosoa tu serikali. Sisemi kuwa serikali isikosolewe, hapana, nachojaribu kusema jamaa hawaitendei haki na hawafanyi kazi ipasavyo Mwalim Nyerere Foumdation. KIMEKUWA KAMA KIJIWE CHA MAJUNGU, ni kweli kabisa au ni KAMA ANOTHER POLITICAL PARTY.
 
Marigwe
Member
Join Date: Fri Nov 2009
Posts: 18
Thanks: 0
Thanked 14 Times in 8 Posts

Kabla ya kongamano hilo kukutana, nilikuwa nimejaa na matumaini kwa kijana Nape Nnauye nikawa nimeamua kama mkazi wa Ubungo, kumpigia kura ya maoni kwa ajili ya jimbo la Ukonga.

Marigwe hajatuambia kwa nini alikuwa na matumaini na Nnauye.


Anachanganya ku-criticize na kujiona bora. Sio lazima critic awe bora ya yule anayekuwa criticized. Sote tunaweza kuwa katika quagmire ya kutojua jibu la hesabu, lakini hili halimaanishi kwamba wewe ukitoa jibu lisilo kweli nitashindwa kujua.

Kwa mfano, naweza nisijue jibu la hesabu ya kujumlisha, lakini nikajua kwamba namba zinazojumlishwa zote ni even, na ukijumlisha namba even utapata jibu even, kwa hiyo hata kabla sijajua jibu lenyewe, ukiniletea jibu lililo odd, nitajua kwamba jibu si sahihi.

Critics wa Kikwete hata kama hawana uwezo wa kuongoza nchi wanaweza kujua jinsi gani hatutakiwi kuendesha nchi. Let us not try to silence a much needed force of dissent.

Ukimpa Nnape aongoze hataweza. Mimi nayasema haya from experience.

OK, hebu tusikilize experience gani hii?

Tunaemjua Jackson Makwetta enzi zake kabla hajawa Mbunge akifundisha IDM naye alikuwa hivi hivi kama akina Baregu na huyu kijana Nnape. Leo Makwetta ana miaka 30 ndani ya jimbo Njombe kaskazini wapiga kura hata kumuona hawataki. Hilo la kwanza.

Sasa experience yako na Makwetta unaenda kumvika Nnauye wapi na wapi? Isn't this a case of a dilapidated comparison?


Kama wazee wanaongelea performance ya rais, how can that not be about mustakabali wa taifa? Au mnataka mpaka awe Nyerere anawatungia watu vitabu na kuwasema ndiyo muone statesmanship, akifanya mwingine bila muhuri wa Nyerere ni nostalgic jealousy?

Na wakaamua kumchapa Lowasa lakini hawakuwa na ujasiri wa kumtaja hata kwa jina.

Hujaeleza umejuaje ni Lowassa wakati hakutajwa jina, unatupa shaka na uwezo wako wa kujieleza.

Basi wangemwalika ahudhurie. Sisi tunaoijua historia ya nchi yetu tunafahamu kuwa hao wazee ndiyo walioweka msingi mbovu wa utawala kiasi kwamba leo akina JK wanahangaika.

Kwamba wazee wameweka misingi mibovu kwa wajuvi halina mjadala kama mvuto wa dunia, lakini JK anahangaikaje? JK amekuwa madarakani takriban miaka minne sasa, amefanya nini kubadilisha misingi mibovu hii?


OK, unachukua kitu chenye ukweli na kuki-stretch to the limit. ni kweli kulikuwa na a cabal of northerners, aprticularly people from Mara (Butiku, Apiyo, Musuguri mpaka vijana wa enzi zile kina Matiko etc). Lakini hii impression unayoitoa hapa kwamba hawa watu walikuwa wameweka lockdown kwenye system si kweli. Na wala Nyerere hakuwa zezeta wa kuchaguliwa watu na Butiku to that extent. Maneno yako mwenyewe yanakusuta, umesema bila ya kuwa northerner mtu alikuwa hawezi kupata kazi za usalama wa taifa na jeshi, halafu hapo hapo umemtaja Kitine kama mkuu wa usalama, Hivi Kitine ni northerner yule? Si mtu wa nyanda za juu kusini yule? Na hata mkuu mwingine wa usalama zamani ambaye sasa yuko ubalozini NY, Dr. Augustine Phillip Mahiga, alishika hii post na ni mtu wa kutoka Iringa. Hivi Nyerere kama angekuwa mkabila kiasi hicho angemuachia Mwinyi achukue urais baada yake? Warioba aliteuliwa kuwa PM na nani kama si Mwinyi?

Nakubali Butiku, Apiyo na wazee fulani wa Kikurya/ Kijita/ Kizanaki walio roll na hii Ikulu/ Intelligece/ Armed Forces clique walikuwa na impunity ya ajabu, complete with their crazed sex parties kwa mzee Butiku ( ndiyo maana naona hii moral authority yake inakuwa tainted na hypocrisy na nostalgia to an extent) . But this movement is bigger than Butiku, kuna yule kichaa msemaovyo wa kimasai anayepiga mke wake na kuamini mke ni property mpaka leo, by the name of Mateo Qaresi, Qaresi is too real to engage is some political nostalgia. Na washukuru yule Zen Buddhist wa kuitwa Phillip Mangula ameamua kukaa kimya kwa kufuata Confucian principles zake za "silence is golden" kwa sababu yule ndiye anayejua mikakati yote ya chama na anapewa data na team yake mpaka leo.


You not only missed the boat, you missed the entire monsoon season.

This is not about trying to Nyerereize Kikwete, Kikwete is cut from a different cloth, hawa wazee wanakemea blatant disregard for leadership principles na a clear lack of direction. Kikwete amekuwa a laughingstock kiasi cha kwamba hata sisi tulioamini kwamba Ali Hassan Mwinyi ndiye aliyekuwa rais lowest kabisa katika uongozi na hakutakuja kuwa na rais atakayemshinda kwa hilo, tumebadili mawazo sasa na tunaona Kikwete kachukua kombe hilo.



Mara unawataka wazee wasiseme, mara unawataka waandike vitabu - as if that is any different- yaani hueleweki unataka nini.

Hebu angalia wale wazee kwenye kongamano lile. They are all spent forces. Hawana jipya. Mimi ningefurahi kama UDSM na vyuo vingine wangewatumia wazee hao kama wahadhiri ili wawafundishe vijana uzoefu wao.

Mara wazee spent forces hawana jipya, mara UDSM na vyuo vingine viwatumie hao kama wahadhiri wawafundishe vijana uzoefu wao.

Hii schizophrenia inatoka wapi hii? Can you make up your mind?

Spent forces wasio na jipya wataenda kufundisha nini cha muhimu vyuoni?

Wahadhiri wanaoweza kufundisha vyuoni watakuwaje spent forces?
 

hufai kabisa
 
Ndugu mtoa hoja - "marigwe", ninaheshimu uhuru na haki uliyonayo ya kutoa maoni lakini sikubaliani na wewe na mtu mwingine yeyote ambaye atajaribu ku-discredit maoni yaliyotolewa na akina Butiku katika kongamano.

Kwanza kabisa hoja yako ya kumnyima kura Nape Nnauye simply kwa sababu ameweza kuwa na ujasiri wa kukemea uzembe wa rais, hiyo peke yake inaonesha kwamba wewe haufai kuwa na haki ya kupiga kura - na hayo ni maoni yangu tu.

Sasa nikija kwenye hoja yako ya msingi kuhusu uhalali wa kongamano lile kuzungumzia mustakabali wa Taifa letu, sidhani kama kuna sehemu nyingine yeyote ambayo ilifaa kujadili suala hilo zaidi ya kwenye hilo kongamano. The venue was right, the time was right and those (Butiku et'al) were the right people kumkemea Rais.

Jaribu kujiuliza, ni nani mwenye credibility zaidi ya akina Butiku na wenzake katika kulizungumzia suala la ukosefu wa ujasiri wa Rais? Ni wapi suala hilo lingeweza kujadiliwa na kupata mvuto kutoka kwenye jamii kama sio kwenye kongamano la kumuenzi Mwalimu?

Maneno yaliyosemwa na hawa makada waCCM yamemchoma sana JK na wapambe wake kama Makamba, kwa sababu ni maneno ya kweli na yanawauma. JK nchi imemshinda na hii inadhihirishwa na safari zake za kila siku za nje ya nchi ambazo HAZINA TIJA kwa Taifa.Watanzania tuna matatizo mengi makubwa yanayohitaji a very close attention ya Rais na mawaziri wake, lakini JK hashikiki na haambiliki.

Kwa nini tusimseme Rais kwa kuamua kufanya safari nyingine tena ya kwenda Copenhagen tena na watu 60? Watu wote hao ni kwa madhumuni gani? Halafu watu wakilalamika wanaambiwa wana chuki binafsi, hivi kama Nkangaa lishindwa na Dewji kwenye uchanguzi wa CCM sasa kwanini asiwe na chuki binafsi dhidi ya Dewji? Hizi sababu za kipumbavu zinazotolewa na akina Makamba whenever Rais akiwa critisized na kuwahusisha hao critics kuwa na chuki. Nadhani muda umefika kwa waTanzania kuzomea tukiwasikia utetezi wa kipuuzi hivyo. Watu wanatetea maslahi ya taifa halafu JK na wapambe wake wanaleta utetezi wa kipuuzi wa chuki binafsi, hayo ni mambo ya kishoga na hayana nafasi katika utetezi wa maslahi ya Taifa. Ninbgewashauri wawe more objective na wawaachie confirmed psycho cases kama Sofia Simba ndio watoe sababu za kipuuzi za CHUKI BINAFSI.
 

Kwa haya uliyoyaandika hata Makamba hawezi kukusifia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…