DOKEZO Kongole kwa Serikali kwa kuondoa muingiliano wa kazi za TFDA na TBS, ikiwapendeza sasa muitazame RITA na NIDA

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Ngoja niwaze na mie! Hivi hawa WMA nao sijui wafutwe au waunganishwe unganishwe tu huko huko!!!!
 
Ngoja niwaze na mie! Hivi hawa WMA nao sijui wafutwe au waunganishwe unganishwe tu huko huko!!!!

Labda hawa wapelekwe tu TBS kule maana majukumu yao ni kihakiki VIWANGO vya vipimo na mizani, (kama mamizani ya duka la mangi/bucha, matanker ya mafuta, body za lory za mchanga/kokoto, pump za mafuta, urefu na unene wa vifaa mbali mbali kama vya ujenzi kuhakiki kama vipimo viko sawa, vifaa tiba, n.k) so kwa sababu lengo lao ni kuhakiki VIWANGO na UBORA wa vitu hivyo kuhakikisha vimefikia standards basi peleka TBS.
 
Kweli jaman vibaka na wqbakaji nao waunganishe utendaji wao ,mabaa maid na mchangu doa nao wawe taasisi moja yqqni sasa waajiriwe machangudoa tu kwenye hizi local bar!hata waganga na wachawi pia wawe idara moja chini ya waziri wa ushirikina
 
Kweli jaman vibaka na wqbakaji nao waunganishe utendaji wao ,mabaa maid na mchangu doa nao wawe taasisi moja yqqni sasa waajiriwe machangudoa tu kwenye hizi local bar!hata waganga na wachawi pia wawe idara moja chini ya waziri wa ushirikina

Unaandika nini mkuu?
 

Nakubaliana na wewe na ndio nlichomaanisha. Kazi zinazofanywa na Pharmacy Council awali zilikuwa zinafanywa na TFDA.
Ishu ya Chakula na hata Vipodozi zingeeendelea kubaki TFDA. Kilichotakiwa ni kumsaifdia mfanyabiashara kupata mahitaji yake (kwa maana ya vibali, usajili wa majengo, matakwa ya usimamizi/taratibu za kiundeshaji) ndani ya taasisi moja. Na haya yangeangaliwa tangu mwanzoni ikiwa ni pamoja na kuweka mbali siasa au maslahi binafsi kusingekuwa na haja ya mabadiiliko ya mara kwa mara/yasiyo ya lazima kwenye taasisi husika.
 
Moja Kati ya maamuzi mabovu ya Serikali hii ni kutenganisha Chakula na Vipodozi kutoka TFDA. TBS ni miongoni mwa Taasisi dhaifu sana. Haina mifumo , haina utaalamu wala haina Watumishi au Ofisi za Kanda kulinganisha na TFDA. Ni suala la muda tuu kabla Wafanyabishara hawajaanza kupiga tena kelele kwa kucheleweshewa vibali ama usajili wa bidhaa/ majengo.

Serikali ilileta Blue print ambayo ilitakiwa iwe mwarobaini wa muingiliano unaodaiwa kuwapo lakini Serikali imeshindwa kuiheshimu Blue print yake na kuja na kupeleka usimamizi TBS .

Ieleweke TBS haikuanzishwa kama regulatory body, haina regulatory framework wala Stratergic plan yao( kama wanayo) haipo ki regulation. Hili ni suala la muda kabla hawajaumbuka
 
MM bado siungi mkono swala hili bali ninachoweza kusema ni kuwa,Kwa technologia ilipofikia kwa sasa haina shida kwa hizi taasisi kufanya kazi pamoja kwa kuunganisha mifumo yake mfano ukienda TBS unamalizana nao sawa na ukienda kwa TFDA the same way ukienda PCCB wawe na connection na TISS ,SUMATRA wawe na EWURA, NIDA iambatane sambamba na RITA,mitandao ya simu sambamba na TCRA,TCU na vyuo vyote,mabenk na system za serikali(siyo unaenda bank unaambia hatutambua hii kitambulisho cha sehemu fulani) nk
Sisi raia wa kawaida tupate huduma popote pale lkn wao wafanye yote yanayowezekana kujua jinsi ya kushirikiana kwenye hizo taasisi.
 
Unaandika nini mkuu?
Najua bas!nimechanganyikiwa kimtindo ghafla tu maichukia nchi yangu kuliko chochote kile bas kila neno naliona adui kwangu yaani nimedata kiaina!
Hata wewe jifanye mkulima ndio utajua hali yangu ikoje sasa!
 
Kwani mifuko ya kijamii ilipounganishwa wafanyakazi wa taasisi hizo walipelekwa/walibaki/walitawanywa wapi?

Hebu ulizia (wataalamu njooni) kwa wajuvi humu jamvini ili uni tag na mimi nipate mwanga/uelewa.
hapa ipo kazi sana,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…