Korea Kaskazini yaadhimisha miaka 111 ya kuzaliwa kwa mwasisi wake

Korea Kaskazini yaadhimisha miaka 111 ya kuzaliwa kwa mwasisi wake

HERY HERNHO

Senior Member
Joined
Mar 4, 2022
Posts
110
Reaction score
458
20230415_04_1243526_L.jpg

  • Leo Jumamosi inatimia miaka 111 tangu kuzaliwa kwa mwasisi wa Korea Kaskazini, Kim Il Sung.
Jana Ijumaa usiku, runinga ya serikali ya nchi hiyo ilionesha video ya bango lenye maneno “kiongozi wa milele” likipandishwa juu jijini Pyongyang. Wanawake waliovalia nguo za kitamaduni walionekana wakiimba na kucheza jukwaani.

Siku ya kuzaliwa kwa Kim ni moja ya sikukuu muhimu zaidi za umma nchini Korea Kaskazini. Huenda Korea Kaskazini wakaitumia siku hii kuimarisha fahari ya nchi kama vile kutangaza mipango ya nyuklia na makombora ya nchi hiyo.

Jana Ijumaa Korea Kaskazini ilisema ilifanya jaribio la kwanza la kombora la kuvuka mabara la Hwasong-18 siku iliyotangulia. Kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong Un, alikuwepo.

Kombora hilo liliripotiwa kutumia fueli mango, inayowezesha urushaji kwa haraka.
 
Miaka ya kutumia nguvu ilishaisha kitambo,kwasasa dunia inatumia akili zaidi,kiduku anatumia nguvu nyingi sana kuaminisha watu yupo vizuri wakati uhalisia watu wake wako dhoofu hali.
 
Miaka ya kutumia nguvu ilishaisha kitambo,kwasasa dunia inatumia akili zaidi,kiduku anatumia nguvu nyingi sana kuaminisha watu yupo vizuri wakati uhalisia watu wake wako dhoofu hali.
ila marekani na ulaya nato kuvamia ....libya ....iraq .....afghanistan ....ni kutumia akili ......huko hawajatumia nguvu .....au hizo ni habari za kizamani.....miaka ya 1880 huko etii
 
Miaka ya kutumia nguvu ilishaisha kitambo,kwasasa dunia inatumia akili zaidi,kiduku anatumia nguvu nyingi sana kuaminisha watu yupo vizuri wakati uhalisia watu wake wako dhoofu hali.
alafu unasema dunia inatumia akili ni kweli hata hao unawaona hawana akili wametumi akili ndio maaana wametengeneza hayo mabalistic missiles kiasi kwamba hakuna wa kuwa tishia kama akina marekani ....na wenziiee .....kwa kifupi wana teknolojia kubwa kuliko akili zako wew
 
ila marekani na ulaya nato kuvamia ....libya ....iraq .....afghanistan ....ni kutumia akili ......huko hawajatumia nguvu .....au hizo ni habari za kizamani.....miaka ya 1880 huko etii
marekani alichokozwa na mataifa haya wewe.Osama alikuwa anaishi wapi walipoiishambulia marekani? halafu Libya unakumbuka ilitumia magaidi kulipua ndege ya abilia lock heed na kuuwa watu 350? Iran iliitumia hisbollah kuuwa askali 250 wa kimarekani Lebanon. Iraq sadam hussein alikuwa nawalipa dola 25 elfu wapalestina wakijilipua nakuuwa watu wasio na hatia Israel. sasa marekani kuyapiga mataifa haya hana kosa lolote duniani. Vitabu vyote vitakatifu kuna vifungu vinawapa ruksa wamarekani kuwapiga waarabu hao.
 
hawa jamaa wa korea kaskazini wnateseka sana na amri kumi na moja za kikomunisti. mojawapo mbaya sana ni ile isemayo ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CHAMA . kumbuka hawa jamaa bado wana matembezi ya mshikamano! wana chama chashika hatamu! wana katibu mkuu atembeaye na ving'ora!
 
hawa jamaa wa korea kaskazini wnateseka sana na amri kumi na moja za kikomunisti. mojawapo mbaya sana ni ile isemayo ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI WA CHAMA . kumbuka hawa jamaa bado wana matembezi ya mshikamano! wana chama chashika hatamu! wana katibu mkuu atembeaye na ving'ora!
Kama hapa Tanzania tunavyoteseka na "ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYE CHAMA"Ila Sisi tumeiprove zaidi Kwa kumuweka kwenya mabango.
 
Back
Top Bottom