Korea Kaskazini yaangusha mabaki ya kombora la masafa marefu ndani ya eneo la Japan

Korea Kaskazini yaangusha mabaki ya kombora la masafa marefu ndani ya eneo la Japan

Majaribio wamefanya kwenye ardhi ya nchi nyingine, ni wazi huyu dogo husaka vita.
North korea hajarusha makombora kwenye ardhi ya japan na majaribio ya sasa hayajakiuka maadhimio ya UN kwa mujibu wa mkuu wa majeshi ya US yaliyopo korea kusini.

Kilichopo jina la bahari ndilo limewachanganya. Hii bahari wajapan wanaita bahari ya japan wakati wakorea(north na south) wanaita bahari ya mashariki.
Kuna kutokuelewana kati ya korea na japan kuhusu hii bahari.

Lakini makombora majaribio yamefanywa ndani ya mipaka ya korea kaskazini.
 
Majaribio wamefanya kwenye ardhi ya nchi nyingine, ni wazi huyu dogo husaka vita.
Hiyo ni kawaida Sana kwa mabaki kuangukia kwenye ardhi ya nchi nyingine
 
Japan huwa anatulia kimya kwa sababu mabaki yake yanadondokea kwenye bahari yao kwa kuwa wanaharibu mabomu ya masafa marefu ipo kipindi alikua anayajaribu uelekeo wa SK nusu wazipige hao ndio akabadili uelekeo sema USA ndio anawachezesha Kwata ila wao wanajua ni ndugu kabisaa ila USA kwa interest zake anatengeneza bifu na kiduku anaweka mazingira magumu kwa pande zote mbili...

Inaitwa international geopolitics.... Lazima dunia ikae mkao wa balance fulani hivi, hairuhusiwi muwe ndugu nyote, inapaswa kanda fulani mnanuniana ili biashara na uchumi wa dunia uweze kutamalaki. Wahoji wabobezi kwenye haya mambo watakupa darasa, usisubiri hata siku moja dunia tukawa na amani pembe zote, na hata Marekani akianguka leo, lazima ataibuka mwingine wa kuendeleza chokochoko ulimwenguni.
 
North korea hajarusha makombora kwenye ardhi ya japan na majaribio ya sasa hayajakiuka maadhimio ya UN kwa mujibu wa mkuu wa majeshi ya US yaliyopo korea kusini.

Kilichopo jina la bahari ndilo limewachanganya. Hii bahari wajapan wanaita bahari ya japan wakati wakorea(north na south) wanaita bahari ya mashariki.
Kuna kutokuelewana kati ya korea na japan kuhusu hii bahari.

Lakini makombora majaribio yamefanywa ndani ya mipaka ya korea kaskazini.

Mbona asifanye kwake ndani, kwanini afanye kwenye eneo la bahari lenye utata baina yake na Japan kama sio ugomvi anaousaka, akirindima hayo makombora kwenye milima na mapori yake hakuna atakayehoji, au atupe kwenye eneo lake la bahari watamuacha kimya.

Hebu waza, itokee mimi na wewe tuna bifu na kaugomvi fulani, halafu nirushe ngumi kama ninayeelekeza kwenye pua lako ila nisitishe kabla kukugusa, niambie kama utakua na amani au wewe pia utajiandaa tuzipige.
 

Korea Kaskazini yafyatua makombora ya masafa marefu katika bahari ya Japan​

Kim Jong Un

CHANZO CHA PICHA, REUTERS. Maelezo ya picha: Kiongozi huyo wa Korea Kaskazini amerudia kufanyia majaribio makombora ya masafa marefu

Korea Kaskazini imefyatua makombora mawili ya masafa marefu ndani ya bahari ya Japan, zimesema Marekani na Japan-likiwa ni jaribio la kwanza la aina hiyo tangu Joe Biden awe rais wa Marekani.

Pyongyang ilizuiwa kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu, ambayo yanaangaliwa kama silaha za kutisha, chini ya Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.

Japan imesema kifusi kimeanguka ndani ya eneo lake la maji.

Hii inakuja siku chache tu baada ya Korea Kaskazini kufyatua makombora yasiyo ya Bahari ya Manjano.

Waziri mkuu wa Japan Yoshihide Suga amesema Alhamisi kwamba majaribio hayo yanaleta tisho kwa usalama na amani kwa nchi yake pamoja na kanda hiyo nzima.

Taarifa ya pamoja kutoka kwa wakuu wa jeshi nchini Korea Kusini awali ilisema makombora hayo yalirushwa kutoka katika "kitu ambacho hakijatambulika ".

Bw Biden bado hajatoa taarifa rasmi kuhusu jaribio la hivi karibuni la Korea Kaskazini.

Siku ya Jumanne alipuuza ufyatuaji wa makombora yasiyo ya masafa marefu yaliyorushwa mwishoni mwa juma, akisema kuwa Marekani haikuchukulia jaribio hilo kama uchokozi. Makombora hayo ya masafa mafupi yalidhaniwa kuwa ya kutumia roketi au ni ya masafa marefu ambayo kwa kawaida hulenga eneo fulani, ambayo hayajapigwa marufuku na Baraza la Usalama laUmoja wa Mataifa.

Jaribio hili lina maana gani?​

Hili ni jambo kubwa sana kwa Marekani na washirika wake

Jaribio la mwishoni mwa juma la makombora ya yasiyo ya ballistic linaweza kupuuzwa. Lakini jaribio hili la makombora ya ballistic ni ukiukaji wa wazi wa vikwazo vya Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.

Kwa kusema hivyo, mtangulizi wa Bw Biden Donald Trump hakutaka maswali yoyote kuhusu jaribio la silaha sawa na hizo mwaka 2019.

Mkataba baina ya Bw Trump na Kim Jong-un uliofikiwa nchijni Singapore mwaka 2018 ulikuwa kwamba Pyongyang haitajaribu makombora ya masafa marefu ya ballistic au silaha za nyuklia.

Wakati ule, Ikulu ya White House haikujihusisha na majaribio madogo zaidi ya makombora.

Lakini maafisa wa Bw Biden ndio wametoka tu nchini Japan na Korea Kusini, na kuahidi kuwa "Marekani imerejea" na inawaunga mkono washirika wake.

Labda sasa, utawala Biden, utatakiwa kutoa tamko kuhusu jaribio la silaha ambazo zinatishia marafiki zake Kaskazini mwa Asia.

Washington ia itatambua kuwa Pyongyang ina silaha kubwa katika gala lakeambazo haijazifanyia majaribio tangu mwaka 2017.

North Korea imetengwa kwa mwaka mmoja. Hata iliamua kukata biashara zake nyingi na mshirika wake mkuu China kutokana na janga la Covid-19 , na uchumi wake unasemekana kuwa katika hali mbaya.

Sasa wakati ikionekana kurejesha majaribio yake ya silaha, wengi wanashangaa ni kwa kiwango gani anachotaka kukifikia Bw Kim Jong-un ili kuweza kuutishia utawala wa Marekani.

Majaribio haya yanafanyika huku utawala wa Biden ukiendelea kujaribu kufanya mawasiliano ya kidiplomasia na Korea Kaskazini.
Uchokozi waziwazi
 
Inaitwa international geopolitics.... Lazima dunia ikae mkao wa balance fulani hivi, hairuhusiwi muwe ndugu nyote, inapaswa kanda fulani mnanuniana ili biashara na uchumi wa dunia uweze kutamalaki. Wahoji wabobezi kwenye haya mambo watakupa darasa, usisubiri hata siku moja dunia tukawa na amani pembe zote, na hata Marekani akianguka leo, lazima ataibuka mwingine wa kuendeleza chokochoko ulimwenguni.
Nimuhoji nani mimi ni mmoja Watanzania wachache tuliofika daraja linaloitenganisha China na Korea kaskazini sikuweza kupata visa ya NK kwa sababu nilikua na visa ya USA kitambo kwenye ile passport yangu ya zamani hapo Beijing ubalozi wa NK unaishia kwa Askari wa nje wanakwambia you Amerikani...
 
Nimuhoji nani mimi ni mmoja Watanzania wachache tuliofika daraja linaloitenganisha China na Korea kaskazini sikuweza kupata visa ya NK kwa sababu nilikua na visa ya USA kitambo kwenye ile passport yangu ya zamani hapo Beijing ubalozi wa NK unaishia kwa Askari wa nje wanakwambia you Amerikani...

Itakua haukunielewa, hata kama umefika mpaka kwa Kim na mkanywa chai naye ila nilichokisema ndio uhalisia wa dunia, chukua muda wako kufuatilia chokochoko zote za dunia na zilivyokaa kiuchumi na kimahusiano utaelewa.
 
Itakua haukunielewa, hata kama umefika mpaka kwa Kim na mkanywa chai naye ila nilichokisema ndio uhalisia wa dunia, chukua muda wako kufuatilia chokochoko zote za dunia na zilivyokaa kiuchumi na kimahusiano utaelewa.
Ndio maana nimekwambia mimi siasa pamoja na kusikia huwa natumia muda wangu kwenda kujifunza mwenyewe sio kwa wapiga mbiu...
 
Mbona asifanye kwake ndani, kwanini afanye kwenye eneo la bahari lenye utata baina yake na Japan kama sio ugomvi anaousaka, akirindima hayo makombora kwenye milima na mapori yake hakuna atakayehoji, au atupe kwenye eneo lake la bahari watamuacha kimya.

Hebu waza, itokee mimi na wewe tuna bifu na kaugomvi fulani, halafu nirushe ngumi kama ninayeelekeza kwenye pua lako ila nisitishe kabla kukugusa, niambie kama utakua na amani au wewe pia utajiandaa tuzipige.
Hakuna mchi yoyoye inayozuiwa kutumia bahari ambayo ipo ndani ya mipaka yake.

Pili, utata uliopo kati ya korea na japan ni kuhusu jina la bahari tu na mipaka ya kila nchi inafahamika.
640px-Sea_of_Japan_naming_dispute.png


Hivyo, hakuna nchi yoyoye ambayo imewahi adhibiwa kwa kufanya makombora ya masafa mafupi na korea kaskazini hakuvunja resolution yoyote ya UN.
 
Hakuna mchi yoyoye inayozuiwa kutumia bahari ambayo ipo ndani ya mipaka yake.

Pili, utata uliopo kati ya korea na japan ni kuhusu jina la bahari tu na mipaka ya kila nchi inafahamika.
640px-Sea_of_Japan_naming_dispute.png


Hivyo, hakuna nchi yoyoye ambayo imewahi adhibiwa kwa kufanya makombora ya masafa mafupi na korea kaskazini hakuvunja resolution yoyote ya UN.

Haingii akilini ufanye majaribio ya makombora ya masafa marefu karibu na hasidi yako na pasipigwe makelele, kwa mfano Tanzana na Malawi huwa na kaugomvi fulani kuhusu jina la ziwa wanalochangia, sasa leo JWTZ waende kufanya majaribio ya makombora yenye uwezo wa kufika mji mkuu wa Malawi, wayafanyie hapo kwenye ziwa hilo......hata kama watakua wanapiga kwenye fukwe za Tanzania, lazima kutaibua yaliyofukiwa.

_98979449_north_korea_missile_test_29nov_without_altitude-nc.png
 
Haingii akilini ufanye majaribio ya makombora ya masafa marefu karibu na hasidi yako na pasipigwe makelele, kwa mfano Tanzana na Malawi huwa na kaugomvi fulani kuhusu jina la ziwa wanalochangia, sasa leo JWTZ waende kufanya majaribio ya makombora yenye uwezo wa kufika mji mkuu wa Malawi, wayafanyie hapo kwenye ziwa hilo......hata kama watakua wanapiga kwenye fukwe za Tanzania, lazima kutaibua yaliyofukiwa.

_98979449_north_korea_missile_test_29nov_without_altitude-nc.png
Ni wapi huko ambapo wamesema kuwa makombora ya sasa ni masafa marefu?

Korea Kaskazini amefanya majaribio ya makombora ya masafa mafupi ndani ya mipaka yake, ambalo hili hata mkuu wa majeshi ya us korea kusini amekiri kuwa ya kawaida na hakuna resolution yoyote iliyokiukwa.

Soma tena madai yako na nilichoandika utata kati ya korea na japani ni kuhusu JINA na sio MIPAKA kama mfano ulioutoa wa tz na malawi kuhusu ziwa nyasa.

Ndio maana kwenye bahari hiyo meli na ndege haziwezi pita maeneo ya mipaka ya North bila ruhusa yao na UN inatambua hilo.
 
Nimuhoji nani mimi ni mmoja Watanzania wachache tuliofika daraja linaloitenganisha China na Korea kaskazini sikuweza kupata visa ya NK kwa sababu nilikua na visa ya USA kitambo kwenye ile passport yangu ya zamani hapo Beijing ubalozi wa NK unaishia kwa Askari wa nje wanakwambia you Amerikani...
North Korea does not have an embassy in the United States, so the visa must be obtained overseas ie.. at the DPRK Embassy in Beijing China
 
Alafu siku zote yule anayeanza chokochoko hua anakuja kupigwa vibaya...
 
Back
Top Bottom