Korea yanunua ardhi "kwa mkopo" Tanzania, Serikali yasita kuthibitisha

Korea yanunua ardhi "kwa mkopo" Tanzania, Serikali yasita kuthibitisha

Mbalamwezi,
Lakini hatujasikia kuwa Putin amewapa Wakorea ruhusa ya kuchimba natural gas ili kugharimia huo mradi. That is the big difference! Watachimba dhahabu yetu na madini mengineyo, kugharimia mradi na faida wanaweka mfukoni.

Kwa hiyo, itakuwa vema tukiwanyima madini na tuwape mashamba pekee, tukiogopa faida watayopata kwenye madini hayo wasiweze kuwekeza shambani?

Je, ikiwa tumekubaliana nao wachimbe madini, kwa mtaji wao, nasi tukaridhika, na pia wakawekeza kwenye mashamba kwa pesa yao, iwe ya kutoka kwenye madini hayo au kwingine, tukubali?

Mimi naona tatizo si kuchimba madini au kutumia ardhi yetu, bali ni namna Tanzania inavyoweza kutajirika kutokana na mikataba tunayoingia na Wakorea.

Kwa uwezo wetu wenyewe, tumefaidikaje na ardhi kubwa hivi kama hadi leo tunalimia jembe la mkono, na hakuna hata benki moja inayomkopesha mkulima wa kawaida?

watu wetu, kwa kutokua thamani ya ardhi sasa wanawauzia wakenya, wanajenga nyumba. Kwa nini wakorea watakaowafundisha uwekezaji wa kilimo wasipangishwe ardhi, nasi tukajifunza kwao?

Hii si nchi ya kuagiza chakula na kuomba msaada wa unga toka nje, na wala si nchi ya kuingiza juisi ya matunda toka uarabuni. Lakini inafanya hivyo, kwa nini?

Kwa nini tuagize hata toothpick toka China?
 
Geek,

kichwa cha hii thread yako, hakika kinatia chumvi nyingi kwenye habari hii. Hebu jaribu kuisoma na kuichambua kwa umakini kidogo, uangalie hata pande zote za uwekezaji unaozungumziwa, hasi na chanya. Vinginevyo utakuwa umezama kwenye wimbi la waandishi wa magazeti uchwara ya yellow journalism mkuu!


That is what it is. Tanzania hatujui thamani ya ardhi. Je unatambua kuwa kuna watu wanakufa kwa njaa Tanzania? Kama jibu ni ndiyo, kwanini tunashindwa kujitosheleza kwa chakula?

Serikali inaendeshwa kibabaishaji, hakuna policy ya kilimo inayotekelezeka, wala hakuna strategy ya kufanya kilimo cha uhakika.

Au haya ndiyo mageuzi ya "Kilimo Kwanza", mnaimbiwa wimbo huo kisha mnaitikia Kilimo Kwanza. Lakini huu ni upuuzi tu, hakuna cha kujitetea hapa.

Kwanini tusitumie ardhi tuliyonayo kuzalisha mazao ambayo sisi wenyewe tungeuza Korea Kusini na sehemu nyingine duniani, kwa bei tunayotaka? Lakini pia tukawa na chakula cha kutosheleza mahitaji ya nchi yetu?
 
Last edited:
Inasikitisha sana kuona tumeshindwa kuwa wabunifu kiasi hiki mpaka tunaenda kukaribisha wengine waje watumie ardhi yetu kujizalishia chakula chao tena kwa mtaji wa raslimali zetu, kwa malipo tu ya sie pia kujifunza!!! Kimeshindikana kipi kwa sisi wenyewe kutumia raslimali tulizonazo kuwawezesha wakulima wetu ikiwa hawana ujuzi basi tuwafundishe kwa kuajiri wataalamu au tuwapeleke shule. Nchi yetu ni maskini, ila inabidi tuache kujidanganya na tuwe wawazi kwa nafsi zetu kwamba katika hali zote za kimaskini tulizo nazo mbaya kuliko...ni umaskini wetu wa kimawazo. Kuanzia tunakotokea kwa kuchagua viongozi wasio na utu,ubinadamu,"logic" wala "vision"
 
Kwa hiyo, itakuwa vema tukiwanyima madini na tuwape mashamba pekee, tukiogopa faida watayopata kwenye madini hayo wasiweze kuwekeza shambani?

Je, ikiwa tumekubaliana nao wachimbe madini, kwa mtaji wao, nasi tukaridhika, na pia wakawekeza kwenye mashamba kwa pesa yao, iwe ya kutoka kwenye madini hayo au kwingine, tukubali?

Mimi naona tatizo si kuchimba madini au kutumia ardhi yetu, bali ni namna Tanzania inavyoweza kutajirika kutokana na mikataba tunayoingia na Wakorea.

Kwa uwezo wetu wenyewe, tumefaidikaje na ardhi kubwa hivi kama hadi leo tunalimia jembe la mkono, na hakuna hata benki moja inayomkopesha mkulima wa kawaida?

watu wetu, kwa kutokua thamani ya ardhi sasa wanawauzia wakenya, wanajenga nyumba. Kwa nini wakorea watakaowafundisha uwekezaji wa kilimo wasipangishwe ardhi, nasi tukajifunza kwao?

Hii si nchi ya kuagiza chakula na kuomba msaada wa unga toka nje, na wala si nchi ya kuingiza juisi ya matunda toka uarabuni. Lakini inafanya hivyo, kwa nini?

Kwa nini tuagize hata toothpick toka China?
Nitajie hata nchi moja tu katika dunia ya leo ambayo imepiga hatua za maendeleo kwa kukodisha ardhi yake kwa nchi nyingine. Tuache bla, bla.
 
Ndugu yangu, kama wewe huamini kuna walakini basi unaishi sayari nyingine. Tutajie mradi mmoja mkubwa ulioendelezwa Tanzania pasipo kashfa ya corruption.

Kiongozi,

Nakubaliana na wewe. Tatizo mojawapo linalowakabili waTz ni wananchi na viongozi wenye upeo duni, wanaodhani matatizo yetu ya kiuchumi yatatatuliwa na wageni. Na hata leo humu ndani kuna thread ya mkuu wa kaya bila aibu akinadi kuwa uchumi wetu hauwezi kukua bila input ya uwekezaji wa kigeni. Kauli hopeless kama hii kama inatoka kwa kiongozi wa nchi, unataraji nini kutoka kwa mwananchi wa kawaida?
 
"We plan to set up an education centre for Tanzanian farmers in the food-processing zone in order to transfer agricultural know-how and irrigation expertise to them."

He said about 100bn won ($83m) would be spent to develop an initial 100 sq km of land over the next few years.

South Korea's Yonhap news agency reported that the corporation hoped to exploit deposits of iron ore, gold and copper in other parts of the Tanzania to help fund its project.

God of Israel, Koreans building an agricultural centre for farmers in Tanzania, jamani hivi sisi tuna akili kweli???? Sokoine ipo , vyuo vyote vya certificate na diploma tulivyochukua toka kwa mkoloni vinafanya nini, kwa kutuona hivyo na wakenya wakaamua kutaka kujenga chao eti kufundisha Watanzania.

KNCU walijenga chuo maalumu kwa ajili ya kahawa wakati wa ukoloni kwa hela ya wakulima wa kahawa leo chuo tujengewe na wakorea ???? Disgusting.

$ 83,000,000 to develop land in the next few years hizi hela TZ mbona ni hela mbuzi tu Richmond kwa siku ilikuwa US $ ngapi vile? Radar, Michuzi ya EPA tunapata miradi mingapi kama hii, meremeta hebu oneni wadau naona kama vile huu ni mchezo wa kuigiza.

Mwisho sasa the catch is:

South Korea's Yonhap news agency reported that the corporation hoped to exploit deposits of iron ore, gold and copper in other parts of the Tanzania to help fund its project.
Kwa hiyo hiyo hela inayotumika ni yetu wala sio yao, kama serikali inasoma hii hapo tunaingia mkenge watoto wa mujini wanaita changa la macho na sisi tunakwenda kichwa kichwa, Banana Zorro usije ukatuimba bure. Ngoja ngoja naonekana ...................................
 
South Korea's Yonhap news agency reported that the corporation hoped to exploit deposits of iron ore, gold and copper in other parts of the Tanzania to help fund its project.

Bolded ndiyo wamefuata kupitia mgongo wa Kuendeleza kilimo ambacho eti nusu ni kwa ajili ya koreans.

Hivi nchi hii tuna analytical economist na wanasheria?? It sounds as if today is a Fools Day!!! Shit!
 
... i sometimes wish i was born chinese, but again, may be i would've been one of those ran over by military tanks at Tiananmen Square!!!!
 
S Korea agrees Tanzania land deal

South Korea's Yonhap news agency reported that the corporation hoped to exploit deposits of iron ore, gold and copper in other parts of the Tanzania to help fund its project.

The deal comes weeks after Tanzanian Prime Minister Mizengo Pinda visited Seoul, when the two nations promised closer ties.

Source: BBC News

Waungwana, mmesoma hapo juu? Kwa maneno mengine mtaji wa hawa jamaa utapatikana ndani ya nchi yetu kwa kutumia rasilimali zetu. Si ajabu nao wao watachukua 97% na kutuachia 3% ya mapato yatakayotokana na rasilimali zetu. Wanakuja maskini na kuondoka mabilionea. Huu mkataba utawekwa hadharani ili Watanzania tuuchambue!? au utakuwa ni Siri kali!?
 
"Hyundai Heavy Industries said in April it had reached a deal to develop 5 0000 hectares of Russian farmland, to produce 60 000 tons of corn and beans annually by 2014."

http://www.iol.co.za/index.php?set_id=1&click_id=87&art_id=nw20090924084905703C603651

Russia ya Putin yauzwa kwa Wakorea?

Kwenye hiyo habari yako ndugu yangu wamesema:
Heavily populated and resource-poor South Korea is looking overseas to secure stable supplies of natural resources, including food.

Nafkili utajua nia yao ya kuja kwetu sio chakula bali na pia.......malizia
 
Hongera serekali ya Rais kikwete wananchi walikuchaguo kwa wingi wapo nawe ongoza taifa .


Ha ha ha ha ha Duh! Watanzania wapo pamoja na Kikwete katika kuiuza Tanzania na rasilimali zake kwa Wageni! Ukistaajabu ya Mussa....
 
Btw, zile baadhi ya hela za epa zilizosemekana kurudishwa na kuwekezwa kwenye kilimo zisingeweza kufanikisha zoezi hili?!
 
Hii itatusaidia kupata manufaa kwani nusu nzima ya hayo mazao yanabaki kwenye soko letu, tutajifunza namna ipi wenzetu wataweza kufanya kinachotushinda sisi kwa sasa kwenye Ardhi yetu.

Seuse, Nyerere alitaifisha mashamba kibao kwa wakulima wakubwa baada ya azimio la Arusha yakatushinda kuyaendesha kama tunavyojuwa. Sasa kwa nini tusiwa[e watu wanaoweza ili tujifunze na tufaidike?

Hii ya kusema Tanzania inauzwa kwa Korea, ni uzushi, fitina na majungu yasiyo na maendeleo, hizi roho mbaya ndio zinatufanya tusiendelee, ndio haya yananifanya nikubaliane na kauli ya ''Miafrika Ndivyo Tulivyo''!

Ngugu JF tunaheshimu mawazo ya kila mtu hata ikiwa ni utoko. Asante
 
Kwenye hiyo habari yako ndugu yangu wamesema:


Nafkili utajua nia yao ya kuja kwetu sio chakula bali na pia.......malizia

Hasa hapo umegonga kichwa cha msumiri, wanasema you've nailed it down. Watu wameisoma hii story katika face value, imagine kuwa hilo eneo wanalodai wanataka kulima mazao lina hazina kubwa ya madini, wakianza kuchimba na kuyapeleka kwao kuna mtu atafungua mdomo kama mkataba umesema wana haki ya any natural resources zitakazopatikana katika ardhi husika?

Kwanza tujue location yenyewe, kisha inaweza kusaidia kujua mambo zaidi. After all, hii ni ardhi yetu, hatujaenda kuomba kwa mtu.Ila wajinga wachache wanajipa mamlaka destructive.

NAULIZA TENA, IKAJA PATIKANA ALMASI KWENYE HIYO ARDHI, ITAKUWA NI MALI YA KOREA KUSINI au ya SERIKALI YA KIKWETE INAYOLIA NJIA KILA KUKICHA?
 
Thing is, tumejifunza mara nyingi kuwa si kila tunachoambiwa ndivyo kilivyo. Maswali yangu ni kutaka kujua mpango huo ni wa manufaa kwa Tanzania? Ujue hapo ni mkataba umesainiwa, isije kuwa ni mambo kama migodi ya madini ambayo hatuambulii kitu cha maana. Lakini kwanini walifanya siri mpaka walipokubaliana.

Hii kitu haikuwa siri. Viongozi wa south korea walikuja Tanzania nadhani mwaka jana kuhusu hii issue na mh. Pinda juzi alikwenda kutiliana sign tu huko kwao.

Kwa upande wangu naona kama terms ziko nzuri hakuna tatizo ili mradi wachukue ardhi ambayo siyo makazi ya watu na uzuri wa kuwekeza ktk kilimo ni kwamba ardhi bado ni ya serikali. Tofauti na madini ambapo mali ni madini yakiisha basi mnaambuia mashimo.
 
Hii itatusaidia kupata manufaa kwani nusu nzima ya hayo mazao yanabaki kwenye soko letu, tutajifunza namna ipi wenzetu wataweza kufanya kinachotushinda sisi kwa sasa kwenye Ardhi yetu.

Seuse, Nyerere alitaifisha mashamba kibao kwa wakulima wakubwa baada ya azimio la Arusha yakatushinda kuyaendesha kama tunavyojuwa. Sasa kwa nini tusiwa[e watu wanaoweza ili tujifunze na tufaidike?

Hii ya kusema Tanzania inauzwa kwa Korea, ni uzushi, fitina na majungu yasiyo na maendeleo, hizi roho mbaya ndio zinatufanya tusiendelee, ndio haya yananifanya nikubaliane na kauli ya ''Miafrika Ndivyo Tulivyo''!

Ha ha ha ha! Kigumu Chama Cha Mafisadi! Kigumu! Kwa hiyo wewe unaona mikataba ya kuvuna rasilimali zetu kwa bei karibu na bure kabisa na kuingia mikataba ambayo haina maslahi na nchi yetu kama ya wale wa makabuto toka South Africa Net Group Solutions waliongizwa na Mkapa kwa mtutu wa Bunduki pale TANESCO na mikatana ta akina BARRICK, RITES, TICTS, SASKATEL yote ni uzushi mtupu! Duh! Kweli Mifisadi ndivyo ilivyo! Mifisadi itauza hata nchi yao ili kuendeleza ufisadi wao na kuwaacha mamilioni ya raia wao wakiishi katika maisha ya ufukara wa kutisha.
 
..

Sasa kwa nini tusiwa[e watu wanaoweza ili tujifunze na tufaidike?

Hii ya kusema Tanzania inauzwa kwa Korea, ni uzushi, fitina na majungu yasiyo na maendeleo, hizi roho mbaya ndio zinatufanya tusiendelee, ndio haya yananifanya nikubaliane na kauli ya ''Miafrika Ndivyo Tulivyo''!

Yaani wewe ukipewa uraisi wa nchi, naona watanzania wote watahamishiwa jangwani ili kuwapisha "wanaoweza"
 
"Some African countries export fruit and import fruit juice, or export olives and import olive oil, simply because their past colonialists did not teach them how to process food," he told the AFP news agency.

...

South Korea's Yonhap news agency reported that the corporation hoped to exploit deposits of iron ore, gold and copper in other parts of the

WOW!!!!

What an insult. So they are buying our land and insulting us at the same time LOL! we are beyond pathetic. So who taught the Koreans how to process thier food, or were they born with this knowledge. We have been independent for more than 40 years (all under CCM by the way) why have we not learned?

What is it that we are capable of doing? This is a serious question, what are Tanzanians capable of doing?

We can't extract our own minerals
We can't exploit our own natural gas reserves
We can't protect our environment
We can't farm our own land
We can't process anything
We can't even hold our politians accountable without help from the west
We can't produce anything
etc...

I have given up on this country and the continued stupidity of our leaders.
 
Yaani wewe ukipewa uraisi wa nchi, naona watanzania wote watahamishiwa jangwani ili kuwapisha "wanaoweza"

Naam wala hujakosea, huyu ni fisadi mkubwa sana, hajali kabisa maslahi ya Tanzania na Watanzania. Na siku zote michango yake hapa jukwaani ni kuwatetea mafisadi hata siku moja hajawahi kutetea maslahi ya Watanzania na Tanzania, naona ni mmoja wa mapandikizi waliopandikizwa hapa na mafisadi na chama chama chao.
 
Back
Top Bottom