Korea yanunua ardhi "kwa mkopo" Tanzania, Serikali yasita kuthibitisha


Watu hawataki kuliona hilo Jasusi. Hao 'wachukuaji' wanakuja bila hata mtaji wanavuna rasilimali zetu ili kupata mtaji wao halafu huo mtaji uliopatikana kupitia rasilimali zetu ndiyo wanawekeza halafu kwa ujinga wa Tanzania tunasema tumewakaribisha 'wawekezaji' kumbe hawana uwekezaji wowote ni matapeli tu! Only in Tanzania!
 
baada ya sera ya ARI MPYA ,NGUVU MPYA NA KASI MPYA KUPROVE FAILURE, sasa amekuja na SERa mpya ya KILIMO KWANZA
yaani hapo ni kilimo tu kama ni WENYE KUBEBA ALMASI SAWA, WENYE KUBEBA GOLD SAWA, WENYE KUBEBA CHUMA SAWA, LAKINI KILIMO KWANZA
TEHE TEHEE

Naona wabadilishe na kuita sera yao, Usanii Kwanza. Maana badala ya kutwambia sera za Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya pamoja na Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana zimeishia wapi na mafanikio yake yalikuwa yapi wamerukia KILIMO KWANZA kwa kujiandaa na 2010! Naona tu bora wawe na sera ya USANII KWANZA.
 

Son:

Ni makosa makubwa kusema kuwa wanakuja bila mtaji. Kuna kitu kinaitwa Human Capital, watu wenye skills. Kama bila kuwa na watu wenye skills hata Ethiopia ingeweza kuja ku-invest Tanzania.
 
Son:

Ni makosa makubwa kusema kuwa wanakuja bila mtaji. Kuna kitu kinaitwa Human Capital, watu wenye skills. Kama bila kuwa na watu wenye skills hata Ethiopia ingeweza kuja ku-invest Tanzania.

Basi si wakifunge kabisa kabisa hiki chuo cha Sokoine!
 
Unaweza ukawa sahihi Jasusi,

lakini wanawezaje kuchimba madini wakiwa mikono mitupu, nasi tunashindwaje kuchimba madini hayo hayo mikono mitupu?

Siyo kwamba tunashindwa. Sera zetu ni kuvutia wawekezaji. Full stop!
 
Hapa Mh. Wasira anakana...
Tusubirie Jumatatu ijayo.... kama statement ya Waziri wa Kilimo bado itakuwa imesimama dede!!!
 
Son:

Ni makosa makubwa kusema kuwa wanakuja bila mtaji. Kuna kitu kinaitwa Human Capital, watu wenye skills. Kama bila kuwa na watu wenye skills hata Ethiopia ingeweza kuja ku-invest Tanzania.

Ha ha ha ha ha Hata Barrick wana watu wenye skills za certificate tu za miezi 9 au less than that na wakati huo huo wanalipwa $4,000 na wakati huo Wabongo wenzetu wenye elimu ya juu kuwashinda hao hao "wenye skills' za certificates walikuwa wanaambulia 10% tu ya mishahara ya hao wenye skills. Nimeshafanya kazi na the so called TXs wengi tu kutoka nchi mbali mbali na 'skills zao' nyingi ni questionable na Watanzania tumewazidi kwa mbali tu lakini bado walikuwa wanaitwa "Tanzania Experts" na kulipwa mishahara minono na huku hawana uexpert wowote!

Wale makaburu wa Net Group Problems ambao Mkapa aliwapa kuendesha TANESCO nao walikuwa na skills lakini baadaye walikuja kugundulika ni watupu kabisa hawajui chochote kuhusu umeme na wala hawakuwahi kuendesha shirika la uzalishaji umeme. Hawa Wakorea nao watakuwa ni matapeli tu.
 
Basi si wakifunge kabisa kabisa hiki chuo cha Sokoine!

Steve D:

Nilirudi Tanzania na nikaenda mitaa ya pugu Road kutafuta tractor. Valmet wakanipa bei ya kama 35 Millioni. Nikaona kubwa sana na jamaa wakanambia kuwa kuna mikopo ya serikali inaitwa mikopo ya pembejeo.

Nimefuatilia mikopo hiyo. Kweli hipo. Nalichotakiwa ni kuonyesha mali isiyoondosheka. Nimefungua shamba na nachukua mikopo na naanza UKABAILA bongo.

Hivyo sioni sababu ya graduate wa SUA kushindwa kutumia elimu yake.
 
Siyo kwamba tunashindwa. Sera zetu ni kuvutia wawekezaji. Full stop!

Sawa, lakini mkuu Jasusi ukisema hivyo inaonekana kama vile wawekezaji walikuja kwanza, yakafuata madini, kumbe ukweli ni kwamba tulikuwa na madini haya kabla ya historia ya nchi hii, na je, tuliyafanyia nini?

Kuna samaki wengi sana kule baharini, lakini ni pale tunapoibiwa tu ndiyo tunashtuka, wakati hata uwezo wa kuwalinda hao samaki hatuna...bora kipi sasa katika kutumia utajiri huu, tugawane na wenye uwezo wa kuvua, kulima kwa teknoljia na kujiendeleza hatimaye tufanye sisi wenyewe, au tuutazame tu huu utajiri huku ukiibiwa?
 

Son:

Hawa jamaa wanakuja kwenye kilimo. Kilimo hakina skills za nguvu, tunachoshindwa ni nini?

Acheni longolongo.
 

...Mkulu Zakumi, Je, hiyo ni moja la lile fungu la marudisho ya EPA?... seriously!

...Serikali ni mwezezashi, kwanini iwe sirisiri kutangaza kuwawezesha top graduate 10 tu kutoka pale na kuwapa 50Mill kila mmoja (again, fungu la EPA) na kuwatengea maeneo huku wakiwatafutia market Korea, Uarabuni, n.k. na sehemu za kununulia machinery kwa bei nafuu huko Uisraeli?!
 

Mkuu Bubu Ataka Kusema,

You have said it all, Should I say more!!!! Huyo ni mtetezi wa siku zote wa upuuzi ufanyikao Tanzania. Naogopa hata kuchangia kwenye hii mada kwani nitaishia kutukana!!!!

Vichwa panzi ndio wameshikiria usukani Tanzania. How can someone with full sound mind can accept such a deal?

Tiba
 
Hebu mwambie Msaudia kuwa mgawane mafuta yao kama atakuelewa. Ni kwa nini sisi tu ndiyo tuwe kwenye kapu la kugawana? Ndiyo, madini tulikuwa nayo na Nyerere akasema ngoja Watanzania wasome wapate utaalamu waje wayachimbe lakini guess what. Na Watanzania wamesoma kiasi kwamba tunao wataalamu wengi tu wa madini. Lakini Mafisadi waliposhika hatamu tu wakawakaribisha maswahiba wao, wakawapa msamaha wa kodi na leo tunasifika kuwa wazalishaji wa 3 duniani kwa madini lakini we have nothing to show for. Hebu nikuulize: Johannesburg ulijengwa kwa dhahabu iliyokuwa inachimbwa pale. Je leo na keshokutwa kweli Bulyankulu itakuja kuendelea kama Johannesburg? Tutashuhudia barabara zinazopita hewani na sewage safi au tutabaki na makorongo tu? Sasa ardhi is our last refuge. Na hiyo tumeanza kuichezea.
 

Huo ni mfano mzuri Zakumi, hongera sana. Lakini wengi wetu mawazo ya kilimo tunaona ni ya kimasikini na kizamani sana. Hata wanaosomea, wengi wao wanasubiri kuajiriwa!

Na hata mawazo ya mikopo kama tunayo, ni mikopo ya prado tu, kwa ajili ya kwenda kulewea pale Rose Garden.

Kuwekeza katika kilimo, ambako 80% ya Watanzania wanategemea, ndiyo njia sahihi ya kusababisha hali bora kwa kila Mtanzania. Lakini hata sisi tunaobeba maboksi, baadhi yetu tungependa zaidi biashara za kuonekana na wenzetu, kubanana na waarabu kuuza magari nk. Kilimo tunakiogopa, na hatupendi kujifunza mambo mapya kwa sababu tunaogopa changes.
 

Kama haya ndiyo mawazo ya viongozi wetu (i hope ni vinginevyo) basi hii nchi inaenda kuzimu.

Yaani Tanzania kuendelea inahitaji kuwekeza kwenye kilimo!!!, yaani kuwafuata asilimia 80 walioko kwenye kilimo na sio kuwatoa huko kwenye kilimo!!!!!????

Tanzania itaendelea kwa kuinua watu wengi toka kwenye kilimo na kuwaweka kwenye service na manufacturing na sio vinginevyo. China walijaribu kilimo kwa miaka kibao na matokeo yake yanajulikana.

Walivyogundua kuwa kilimo kinawalostisha wakageukia service na manufacturing. Kila siku namsikia Kikwete na yule mtoto wa mkulima ambaye anapanda jet kila aendako (Pinda) wanapiga makelele kuwa nchi yetu itaendela kwa kupitia kilimo ---- yeah, kilimo kwanza; ninabaki bila cha kusema.
 
Last edited:

Tatizo ni kuwa unaongelea serikali ya Kikwete ambayo ni siku si nyingi ilisaini mkataba wa madini kwenye hoteli na kisha hata baada ya kubanwa na wananchi, wameshindwa kufanya chochote.

Huku kujifunza tutaendelea kujifunza hadi kiyama ila kama viongozi hawana dira kama huyu Kikwete, ni bora wasiingie mikataba yoyote na wakoloni hawa -- huu ni mchezo tu kama ule wa Karl Peters miaka ile.
 
Pwani province.. 100,000 hectares for Korean to show us how to farm


Source The Korean Herald http://www.koreaherald.co.kr/NEWKHSITE/data/html_dir/2009/09/24/200909240088.asp
 
Hivi bunge letu linafanya kazi ipi? Nafikiri ifike mahala na ikubalike kwamba mikataba mikubwa yote ambayo serikali inataka kuifanya lazima ipate baraka za bunge kwa maana kwamba ipelekwe huko ijadiliwe na wabunge wapitishe hiyo miradi kwa kula ya ndiyo ama hapana kwa kutamka kila mbunge mmoja mmoja kwa nafsi yake ili baadaye kila mbunge awe accountable kwa watu wake na watanzania kwa ujumla,yanayofanyika sasa kama ni kweli hayaingii akilini mwa mtu!! tumeona ardhi na mashamba yalivyoleta taabu sana Zimbabwe na mpaka sasa ni shida tupu, hivi sisi bado tunakimbilia kutoa ardhi kubwa namna hiyo bila kufikiri kwa kina!! lakini shauri ya 10% who cares? Rais alisema kuwa ange review mikataba ya madini, alikiri kwamba ni mibovu lakini cha ajabu akamteua aliyeandika mikataba hiyo yaani AG wa wakati ule Chenge kuwa waziri wa miundombinu, sijui ni kwa kazi nzuri iliyotukuka aliyoifanya kama AG ilibidi apewe uwaziri tena wa wizara nyeti!! au ni uswahiba this God alone can tell! ya RITES tunayaona leo, kwa maana hiyo serikali isipewe tena mamraka ya kusaini mikataba mikubwa bila kibali cha bunge!! mfano ni huo kwamba raisi kwa maana ya serikali anaona chenge ali draft mikataba mibaya ya madini na akaahidi kuireview kwa maslahi ya Tz lakini pamoja na hayo akaona ampongeze kwa kumteua kuwa waziri!! Ndo serikali tuliyo nayo na raisi tuliyenaye!! Nafikiri it is common sense dictation mwenye mamcho aambiwi Tazama!!
Mungu ibariki Tanzania
 
More news on the land issue.. after development 50,000 hk for locals to farm on their own and remaining 50,000 hk for a Korean company



Source: http://www.iol.co.za/index.php?set_id=1&click_id=87&art_id=nw20090924084905703C603651
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…