Korona imetushinda,yatutia sononeko

Korona imetushinda,yatutia sononeko

Joined
Mar 30, 2020
Posts
4
Reaction score
0
Korona imetushinda,yatutia sononeko
Mazao tuliyopanda,bangi miraa tumbako
Kuuza tunapoenda,wateja hawapo soko
Eti ndiko kuzuia,Korona isizagae.

Magunia ya makaa,tulochoma msituni
Siku mbili yamekaa,stendi gari hatwoni
Serikali mekataa, gari kwingia mjini
Eti ndio kuzuia, Korona izisambae.

Ifikapo saa moja,kinywa chao kimenena
Nti nzima kila mja,si ndani ‘kipatikana
Ataiona miuja, tangu kale hajaona
Eti ndio kuzuia, Korona izipambae.

Tukutuku na matatu, zibebazo abiria
Zibebe wachache watu, si wengi kupindukia
Abiria wasifutu, barakao kuvalia
Eti ndio kuzuia, Korona izimomae.

Ukienda kila kona, mijini na mashambani
Vieuzi utaona, maji ndoo na beseni
Muaji tusomuona, tukimuosha jamani!
Eti ndiko kuzuia, Korona izienee.

Ifikapo saa moja,kinywa chao kimenena
Nti nzima kila mja, si ndani ‘kipatikana
Ataiona miuja, tangu kale hajaona
Eti ndio kuzuia, Korona izipambae.

Tukutuku na matatu,zibebazo abiria
Zibebe wachache watu, si wengi kupindukia
Abiria wasifutu, barakao kuvalia
Eti ndio kuzuia, Korona izimomae.

Ukienda kila kona, mijini na mashambani
Vieuzi utaona, maji ndoo na beseni
Muaji tusomuona, tukimuosha jamani!
Eti ndio kuzuia, Korona izienee.

images%20(2).jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo naingia na verse!

Korona virusi umeweka heshima, hadi kima wanatoa vilio kama yatima. Hakuna bavicha, makucha wala masista.

Karantini Korona, utakufa na sonona, kama Giampaollo Simona ......
 
Korona imetushinda,yatutia sononeko
Mazao tuliyopanda,bangi miraa tumbako
Kuuza tunapoenda,wateja hawapo soko
Eti ndiko kuzuia,Korona isizagae.



Magunia ya makaa,tulochoma msituni
Siku mbili yamekaa,stendi gari hatwoni
Serikali mekataa,gari kwingia mjini
Eti ndio kuzuia,Korona izisambae.


Ifikapo saa moja,kinywa chao kimenena
Nti nzima kila mja,si ndani ‘kipatikana
Ataiona miuja,tangu kale hajaona
Eti ndio kuzuia,Korona izipambae.


Tukutuku na matatu,zibebazo abiria
Zibebe wachache watu,si wengi kupindukia
Abiria wasifutu,barakao kuvalia
Eti ndio kuzuia,Korona izimomae.

Ukienda kila kona, mijini na mashambani
Vieuzi utaona, maji ndoo na beseni
Muaji tusomuona, tukimuosha jamani!
Eti ndiko kuzuia, Korona izienee.


Ifikapo saa moja,kinywa chao kimenena
Nti nzima kila mja,si ndani ‘kipatikana
Ataiona miuja,tangu kale hajaona
Eti ndio kuzuia,Korona izipambae.


Tukutuku na matatu,zibebazo abiria
Zibebe wachache watu,si wengi kupindukia
Abiria wasifutu,barakao kuvalia
Eti ndio kuzuia,Korona izimomae.

Ukienda kila kona, mijini na mashambani
Vieuzi utaona, maji ndoo na beseni
Muaji tusomuona, tukimuosha jamani!
Eti ndio kuzuia, Korona izienee.View attachment 1405068View attachment 1405070

Sent using Jamii Forums mobile app
Big up ndugu, shairi zuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hasa mie ndo korona mwenyewe ngoja nikujibu!

Korona nitawakorona,maisha kujutia
Achaneni na yule ngoma,hajui kafulia
Nitapita Kila Kona,homa mtazisikia!
Singida mpaka dodoma,hodihodi naingia!.

Nipisheni nipite,vikwazo nitatoboa
Uwe dume uwe jike,kote nitaacha doa
Mkiniruhusu nipite,koro nitawaondoa.

Dalili zangu zilezile,mafua na kukohoa
Kipimo changu kilekile,joto lisilo poa!
Nguvu yangu ileile,mapafu kutoboa!
Na Mimi yuleyule,corona nisie poa!😜

Jichungeni kwa kunawa,nisije waangusha
Kote pigeni dawa, nikose pakupita
Mtakapoona sawa,nitakuja kwa kuchupa!
Wanaotafuta dawa,korona nawahasa
Wafanye iwe sawa,kabla sijapapasa😜😜
 
Back
Top Bottom