Kortini kwa kuua wazazi wao

Kortini kwa kuua wazazi wao

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Kortini kwa kuua wazazi wao


Na Bazil Makungu, Ludewa

WAKAZI wa Madunda Wilaya ya Ludewa, mkoani Iringa, Bw. Tito Willa (29) na mkewe Bi. Theopista Mtitu (29) juzi wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya kwa makosa mawili ya kuwaua
wazazi wao, Bw. Laurent Willa (60) na Bi. Alfonsia Msanga (56) kwa kuwakata vichwa.

Wakisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo, Bi. Mariam Rhobi Omari, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Bw. Robert Mwaluswa alisema katika kosa la kwanza washtakiwa wote kwa pamoja Desemba 25 mwaka huu saa 12:00 jioni walimuua Laurent Willa kwa panga na kutenganisha kichwa chake na kiwiliwili nyumbani mwake.

Katika kosa la pili, Bw. Robert aliiambia mahakama hiyo kuwa katika muda na mahali palepale washtakiwa kwa makusudi walimuua kwa mapanga Bi. Alfonsia Msanga na kutenganisha kichwa na kiwiliwili chake. Pia watoto hao baada ya kufanya mauaji hao wanadaiwa walifanya sherehe.

Awali akizungumza na Majira mtoto wa marehemu, Bw. Damasco Willa alisema amepata karatasi aliyoandika na marehemu kama wosia iliyodai amechoshwa na vitisho kutoka kwa mwanawe, kwamba angemuua wakati wowote.

"Muda mrefu sasa kaka yangu amekuwa akimpa vitisho baba na mama yangu bila sababu yoyote ya msingi huku akiwasingizia mambo ya ushirikina, jambo ambalo siyo la kweli," alisema.Washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.
 
"Muda mrefu sasa kaka yangu amekuwa akimpa vitisho baba na mama yangu bila sababu yoyote ya msingi huku akiwasingizia mambo ya ushirikina, jambo ambalo siyo la kweli," alisema.Washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.

Haya ni maoni ya marehemu na pekee yake bado haliwezi kuwaunganisha watuhumiwa kwenye shitaka la mauaji.............
 
Back
Top Bottom