Kosa kubwa tulilolifanya, na kwanini tunasahihisha 2010

Kosa kubwa tulilolifanya, na kwanini tunasahihisha 2010

Mawazo ya kupata mahitaji ya wananchi katika kuunda Ilani za vyama na kusimamia utekelezaji wake ni jambo zuri sana. kinachotakiwa ni namna ya kuweza kusimamia na kutengeneza hizo ilani. Kuundwa kwa chombo kitakayoshughulikia uundwaji wa ilani hizo.

Matatizo yanayoweza kujitokeza ni kama yafuatayo:

1. Tofauti za kiitikadi za vyama vya siasa: Vyama vya siasa hutoa ahadi zao kulingana na itikadi zao na hasa jinsi vinavyoona/amini na kujipanga kutekeleza mambo mbalimbali wanayoahidi kuyatekeleza endapo watachaguliwa.

2. Muda mrefu utahitajika ili kuweza kuunda, kukusanya na kutengeneza Ilani hizo, na baadae kuzipeleka kwa wananchi kwa uhakiki kabla ya kuelimisha vyama vya siasa kwa ajili ya makubaliano ya kuwa ilani kamili.

3. Itahitajika umakini mkubwa katika uandaaji wa makundi ya wananchi ili kuweza kufikia lengo linalokusudiwa, kwa muda unaotegemewa na kwa ubora stahiki. Elimu kwa waanchi juu ya malengo/matarajio ya ilani hizo ni jambo muhimu sana.

4. Udanganyifu wa vyama kuhusu utekelezaji wa ilani hizo za wananchi. Ni rahisi zaidi kwa kila chama kuahidi kuwa kina uwezo wa kutekeleza mapendekezo yote ya ilani za wananchi, na hiyo kuwa kinyume wakati wa utekelezaji. Hivyo ni rahisi kuchagua serikali iliyodanganya na itakayodai kuwa ilani haikutekelezeka na haikuwa yao.

Kwa muda mrefu (tangu tuanze kuwa na chaguzi za vyama vingi vya siasa), vyama vimekuwa vikitengeneza Ilani zao na kuzisoma kwa wananchi wakati wa kampeni. Wananchi hawajawahi kupata nafasi ya kutosha kupitia ilani hizo na kuzitolea maoni yao. Nadhani si vibaya vyama vikaunda ilani. Ila ni vyema zaidi ilani zikasambazwa na kupatikana mapema ili wapiga kura (wananchi) waweze kuzichambua na kuzielewa ili waweze kufanya maamuzi mazuri katika uchaguzi.
 
I'll argue differently.. wao wanapoweka gogo leo wanafikiria kuwa litawasaidia na baadaye na huko mbeleni.. hivyo watachagua gogo la aina gani, lenye sifa gani na lenye kukidhi mahitaji gani ya sasa na ya mbeleni. Hivyo wanapotatua tatizo lao la "sasa" wakati huo huo wanatatua tatizo lao la baadaye. Sisi tunatenganisha (kama ulivyojaribu) kuwa tutatue matatizo ya sasa kwanza halafu tukishayatatua tufikirie namna ya kutatua matatizo ya baadaye.. this as I have pointed out, is what we have been doing for almost 50 years..

guess what happens? tunajikuta bado tuna matatizo ya jana!
Mkuu Mwanakijiji, ni kweli kuwa tumekuwa tukitatua matatizo ya sasa kwa kuzingatia mahitaji ya wakati huo tu. Na si ajabu ndio maana hatupigi hatua za maana.

Kinachotakiwa ni kutatua matatizo tuliyonayo sasa kwa kuzingatia mahitaji ya wakati mrefu ujao. Kwa mfano, haisaidii kujenga barabara ya njia moja katika jiji kama Dar, ukijua kuwa baada ya muda mfupi barabara hiyo itakuwa haipitiki kwasababu za msongamano mkubwa wa magari unatokana na ukuaji wa mji na ongezeko la watu.

Kwa maana nyingine, haisaidii kujenga sasa barabara ambayo ilitakiwa kuwa imejengwa hivyo miaka 50 iliyopita.

Kinachotakiwa ni plan za muda mrefu kutekelezwa katika kila nafasi inayopatikana. Na sio kuziba ufa kwa kutumia pesa nyingi badala ya kutumia pesa zaidi kidogo kujenga kitu ambacho kitakupa nafuu kwa miaka mingi ijayo.
 
Ninachoamini adui wa maendeleo ya kisiasa Tanzania ni wasomi, hawashiriki siasa, waoga, wanapenda kunyenyekea, aibu tupu.

U
kitaka kuamini maneno yangu angalia takwimu za ushindi wa CCM mijini ambako kunawatu wengi wenye elimu ya uraia, kweli ni aibu tupu, maeneo yote kuzunguka vyuo vya elimu ya juu ndipo ambako CCM ilishinda kwa kishindo zaidi.

Hii nimeikubali na nitatizo, ni kweli kabisa wasomi wetu na sisi wenyewe, ni adui wa maendeleoo yetu! It is said that middle class, which are most of the leite are opportunistic, they will only join the lower class when its them with benefits at stake, but not when the poor suffers.

ndio maana huoni prof milionea, they are afraid of risks of few exceptions. Tuanza na JF lets be responsible nad every one of us should change at least two guy out of the forum. that way jamii itabadilika na nchi itaendelea.
 
CCM ndio wanatengeneza mambo kama haya ya ajabu ajabu katika taifa letu na pia itakuwa ni kitu cha umuhimu sana kama mabadiliko yakianzia kwetu sisi
 
nguvumali.. unajua nchi kama Marekani hawajawa na miradi mikubwa ya barabara ya kitaifa kwa miaka mingi sana.. hizi highway tunazoziona sasa hivi zilijengwa miaka ya hamsini.. leo hii ni kupanua tu hapa na pale.. kumodernize madaraja n.k.. sisi bado tunahangaika na Ubungo na traffic lights zake!

Duuuuh!

Teh teh MJJ, Tatizo la viongozi wetu wengi hawapendi kupanua mawazo yao na kuyatendea kazi, Mipango miji inawashinda leo hii wataweza wapi kupanua barabara na isitoshe kuna viongozi wengine vichaaa wameisha pigia mpango barabara za juuu! Kuhamia DODOMA tu kumewashinda sasa siwaelewi hawa viongozi wetu mkichwani mwao kunafikilia nini?

Nadhani kuna haja ya kuwauliza hao watakao gombea do they really need changes? mie sioni haja wala umuhimu wa Ilani zao za uchaguzi za kufanya mambo kwa ujumla uatasikia oooh CCM imewafanyieni hiki mara kile na ndio ilikuwa kwa ilani yetu jamani! Basi mtu pangie kuwa next 5yrs ni haya tutayafanya ilituone improvement every 5yrs.

Au mrudisheni nchi kuwa katika majimbo this is what i think its the best, Muone hao ma mayor watakao chaguliwa kama watalaza damu kwani akichemka tu watu wa jimbo lake watasema hawana imani nae faster ndipo uongozi utaru na kwa adabu, hii ya jumla jumla wana JF twadanganyana kweli kweli kwani kupata kiongozi mwadilifu kwa kipindi hiki ni kazi kweli kweli kwani wapo wachache na hawana nafasi ili wafanya kazi ya wananchi

 
Back
Top Bottom