Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,986
- 5,058
Ni kwa wale waliopitia clinical officer, kuna mpango wa kuanzisha bachelor of clinical medicine kwa miaka mitatu ambayo itakuwa tabora na mtwara. Sasa sijui huko watajifunza basic sciences(the most thing wana lack) au clinical works! Hii itaanzishwa tanzania tu kwani hakuna nchi nyingine ambayo wanasoma kozi ya aina hii. Swali nalojiuliza kwanini wasiongeze nafasi za equivalent qualifications kwenye vyuo vyetu? Na pia sijui kama kutakuwa na mpango wa kupunguza miaka kwa wenye diploma za sheria au engineering au ualimu ili wasome miaka michache zaidi.! Hii ndo tanganyika yetu ambayo wenzetu wanaongeza idadi ya wasomi walioiva sie tunatafuta short cut huku tukivalia njuga suala la jumuia ya africa mashariki.