KRC Genk yatwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka ya Ubelgiji 2018/19

KRC Genk yatwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka ya Ubelgiji 2018/19

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Klabu ya KRC Genk imetwaa rasmi ubingwa wa ligi kuu ya soka ya nchini Ubelgiji, Belgium Jupiler League kwa msimu wa kuanzia 2018/2019.

Klabu hiyo ya KRC Genk ambayo anakipiga nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ambaye pia ni kinara wa mabao kwenye ligi hiyo ya Ubelgiji, Mbwana Samatta Samagoal77, imetwaa ubingwa baada ya kutoka sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Anderlecht na kuweza kufikisha pointi 51 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine.

Ubingwa huo wa KRC Genk umepatikana baada ya wapinzani wao wa karibu kwenye kinyang'anyiro Uchampioni, Club Brugge kupoteza mchezo wao kwa kipigo cha mabao 2-0 mbele ya Standard Liege hivyo kupoteza uwezo wa kufikisha pointi 51 huku ukiwa umebaki mchezo mmoja katika mchuano wa timu sita bora.

Kwa ubingwa huo KRC Genk wamepata nafasi ya kucheza michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao.


IMG_20190516_235002_123.jpeg
IMG_20190516_235035_240.jpeg
 
Hiyo ni hatua ya pili ya mechi za kutafuta bingwa wa jumla na wawakilishi wa UCL/Europa...Huja baada ya hatua ya kwanza

Hatua ya kwanza huwa na timu 16, ambapo timu sita za juu (top 6) baada ya kucheza michezo 30 ndizo zinazo qualify kucheza hatua ya pili (championship playoff)...
Klabu mbona chache sana hivyo katika hiyo ligi?
 
Hii ligi ina timu sita tu?
Hapana, hizo 6 ni zile top on league ambapo zinaingia kwenye kinyanganyiro cha club bingwa ulaya, uefa/uropa league. hapo ukiangalia genk na club buluge zimefuzu tayari kucheza uefa mwakani. hizo mbili zinazofata hapo nazo tayari zimefuzu tayari kucheza uefa/uropa league mwakana. hizo mbili za mwisho kabisa zinaingia ktk play off mshindi anayepatikana anaungana na zile team mbili hapo juu zilizofuzu uefa/ueropa league
 
Hapana, hizo 6 ni zile top on league ambapo zinaingia kwenye kinyanganyiro cha club bingwa ulaya, uefa/uropa league. hapo ukiangalia genk na club buluge zimefuzu tayari kucheza uefa mwakani. hizo mbili zinazofata hapo nazo tayari zimefuzu tayari kucheza uefa/uropa league mwakana. hizo mbili za mwisho kabisa zinaingia ktk play off mshindi anayepatikana anaungana na zile team mbili hapo juu zilizofuzu uefa/ueropa league
Hizo mbili zinazocheza playoffs zitacheza dhidi ya nani?
 
Back
Top Bottom