Krismasi za kukumbuka (sad memories)

Krismasi za kukumbuka (sad memories)

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Leo ni sikukuu ya Christmas .. Siku kubwa ulimwengu kote.. Kwa wiki nzima hii yametokea matukio ambayo yatakuwa ni simulizi za kukumbuka miaka mingi iijayo
Mimi ninazo simulizi mbili nawe kama unayo uta share nasi

Ukata Christmas ya 1993
ilikuwa kipindi cha Mwinyi
Tumeshamaliza chuo tulitakiwa kwenda jeshini kisha ajira.. Serikali ikawa haina hela za kutupeleka jeshini wala kutupa ajira.. Ule msoto ule wee acha tu
Ikawa sasa ni mwendo wa vibarua... Na kutembelea fursa..wakati fursa kubwa kipindi cha Christmas ukiachana na vyakula toka mikoani ni miti ya Christmas
Sasa hii kwetu ipo mingi sana hivyo unakata tu bila kulipa chochote
Nikapanga na jamaa yangu yeye huko mkoani akate akodi fuso apakie mimi nitapokea mzigo Ubungo palipokuwa kituo kikuu cha uuzaji
Timing ya miti ya Chtistmas ilikuwa ni siku nne za mwisho kabla ya sikukuu yenyewe
Logistics na kukata na kupakia zikatuchelewesha kwa siku moja nzima!
Fuso likaingia Ubungo tarehe 24 mchana... Pakiwa pamefurika miti😂 tena mizuri kuliko yetu
Hatukuweza kuuza hata miti kumi kati ya miti zaidi ya 150 tuliyobeba
Fuso hatukuwa tumelipia hata senti.. Tuliukimbia ule mzigo tukamtelekeza dereva na konda wake pale Ubungo Tanesco
Uzuri hakukuwa na simu za mkononi.. Walimiliki wachache tena matajiri
Kwetu sisi siku kama ya leo tarehe 25.12.1993 ilikuwa siku mbaya ya kukumbukwa daima
Mwisho wa simulizi ya kwanza
 
Simulizi. Ya pili itaanzia hapa
FB_IMG_1735081775239.jpg
 
😂😂😂😂😂! Umenimbusha mwaka 2006 nikiwa nimejishikisha kibarua cha kufundisha shule moja Dar maarufu ya private ya wakatoliki. Basi, katika zungumza zungumza muda wa chai ikatokea hoja ya biashara ya kununua mbuzi mikoani na kuzileta Dar machinjioni Vingunguti na kuziuza kwa bei nzuri. Yaani mikoani mbuzi unamnunu elfu 5 hadi 8 lakini ukimfikisha Dar bei ni kuanzia 30 elfu hadi 60. Mwalimu mwenzetu kajaa mazima sijui hela alizitoa wapi kapakia lory. Kipindi hicho kilikuwa kipindi cha mvua daraja la Luvu likafurika magari hayapiti mbuzi kwa wiki mbuzi wengi wakadhoofu na kufa. Kwa ufupi hakuambualia hata senti na mwisho wa siku akawa haonekani kazini mpaka natoka pale sikuwahi kumuona!
 
😂😂😂😂😂! Umenimbusha mwaka 2006 nikiwa nimejishikisha kibarua cha kufundisha shule moja Dar maarufu ya private ya wakatoliki. Basi, katika zungumza zungumza muda wa chai ikatokea hoja ya biashara ya kununua mbuzi mikoani na kuzileta Dar machinjioni Vingunguti na kuziuza kwa bei nzuri. Yaani mikoani mbuzi unamnunu elfu 5 hadi 8 lakini ukimfikisha Dar bei ni kuanzia 30 elfu hadi 60. Mwalimu mwenzetu kajaa mazima siju hela alizitoa wapi kapakia lory. Kipindi hicho kilikuwa kipindi cha mvua daraja la Luvu likafurika magari hayapiti mbuzi kwa wiki mbuzi wengi wakadhoofu na kufa. Kwa ufupi hakuambuali ahata senti na mwisho wa siku akawa haonekani kazini mpaka natoka pale sikuwahi kumuona!
Huyo alikwenda kujinyonga maskini ..haya mambo yasikie tu ukisimuliwa yasikukute😁
 
Daaaa! Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni krismasi ndio inafika, mimi ni muajiriwa mahali fulani kipindi hicho. Halafu ndani naishi na mwanamke japo si wa ndoa na tuna mtoto mmoja. Sikukuu inafika sina kitu mfukoni na kazini hatujalipwa.

Sasa wife anasisitiza tununue chochote hata ikiwezekana tukope. Nikiangalia sioni shehemu ya kukopa. Nikamwambia wife kakope kwa mangi maharagwe tu leo tutakula tusubiri sikukuu ya mwaka mpya nitajipanga. Wife Kagoma hadi ikawa kelele ndani. Mara karopoka leo sili (mimi) na wala hapiki chochote.

Kumbe bwana mama mwenye nyumba alikuwa anasikiliza tu. Nilikuwa nimepanga nyumba tunaishi na mwenye nyumba nyumba moja kasoro vyumba tu, si unajua uswahilini.

Nikachukulia mzaha nikatulia ndani nacheki TV chaneli kama zote nabadili tu, sina ramani kabisa ya kutoka siku hiyo. Basi bwana mama mwenye nyumba kwa huruma zake kumbe kapika na ziada. Mida ya saa nane mchana nasikia anamwita wife. Hapo ni kwamba dogo (mtoto wetu) kakotogewa uji mchache asubuhi na mimi hata sikutaka kuuonja. Ndani kuna unga, mchele, viazi mviringo dagaa na mafuta ya kupikia. Mkaa upo na gesi tulikuwa nayo, kwa hiyo ilikuwa ni maamuzi tu ya wife kupika.

Wife katoka kwenda chumba cha mama mwenye nyumba, sikujua kaitiwa nini. Masikio hayana pazia bwana. Nikasikia akamwambia wife: NILISIKIA MABISHANO YENU NA MUMEO. KWA BAHATI MIMI NINA NAFASI KIDOGO NIMEAMUA NIONGEZE CHAKULA ILI NA NYIE MPATE JAPO SIKUKUU IENDE VIZIRI. LETA VYOMBO UPAKUE CHAKUALA HIKI HAPO KAMA UNAVYOONA.

Mara wife yuko ndani anachukua hotpot na mabakuli. Kaelekea kwa mwenye nyumba na baada ya mda karudi na pilau kuku, ndizi za kupika na kachumbari. Kaweka mezani wala hakunusemesha. Nami nikachuna tu. Kamwita dogo akasogea kampakulia chakuala, mimi nimekomaa na TV kama kipofu vile.

Kwa kweli nilijisikia aibu sana sana. Kuzuga nikajifanya naenda dukani kununua soda (nilichukua matupu manne). Sikupita kwa mangi nikala chocho nikatikeza mtaa wa pili. Nikaelekea kwa mshikaji wangu, yeye alikuwa bachela, hajaoa. Bahati nikamkuta nae kachili tu. Nikampa stori nzima.

Mwanangu akasononeka sana. Kaanza kunikumbusha mambo ya longi mara ooooo, huyo demu wako usingezaa nae tulukwambia sio wife material unaona sasa... Tukapiga stori pale za kutosha. Kumbe mwenzangu asubuhi kapiga zake supu hana shida.

Ikabidi nijikaze kiume, tena ukizingatia niko na mwana. Nikampa live sina hata jero na kazini hatujalipwa, tena sijala. Mwana akanielewa. Akasema kuhusu wife shauri yake... Akanitoa tukaenda kupiga kitimoto choma bwana... Baada ya hapo gambe likaanza hadi saa tano usiku nakumbuka nyumbani. Hapo simu nilizima ttka mchana. Kurudi home wife kafungua mlango mimi direct kitandani hakuna neno hata moja. Kesho yake wife anaomba msamaha. Nikaona isiwe tabu ni maisha tu nikammsamehe.
 
Daaaa! Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni krismasi ndio inafika, mimi ni muajiriwa mahali fulani kipindi hicho. Halafu ndani naishi na mwanamke japo si wa ndoa na tuna mtoto mmoja. Sikukuu inafika sina kitu mfukoni na kazini hatujalipwa.

Sasa wife anasisitiza tununue chochote hata ikiwezekana tukope. Nikiangalia sioni shehemu ya kukopa. Nikamwambia wife kakope kwa mangi maharagwe tu leo tutakula tusubiri sikukuu ya mwaka mpya nitajipanga. Wife Kagoma hadi ikawa kelele ndani. Mara karopoka leo sili (mimi) na wala hapiki chochote.

Kumbe bwana mama mwenye nyumba alikuwa anasikiliza tu. Nilikuwa nimepanga nyumba tunaishi na mwenye nyumba nyumba moja kasoro vyumba tu, si unajua uswahilini.

Nikachukulia mzaha nikatulia ndani nacheki TV chaneli kama zote nabadili tu, sina ramani kabisa ya kutoka siku hiyo. Basi bwana mama mwenye nyumba kwa huruma zake kumbe kapika na ziada. Mida ya saa nane mchana nasikia anamwita wife. Hapo ni kwamba dogo (mtoto wetu) kakotogewa uji mchache asubuhi na mimi hata sikutaka kuuonja. Ndani kuna unga, mchele, viazi mviringo dagaa na mafuta ya kupikia. Mkaa upo na gesi tulikuwa nayo, kwa hiyo ilikuwa ni maamuzi tu ya wife kupika.

Wife katoka kwenda chumba cha mama mwenye nyumba, sikujua kaitiwa nini. Masikio hayana pazia bwana. Nikasikia akamwambia wife: NILISIKIA MABISHANO YENU NA MUMEO. KWA BAHATI MIMI NINA NAFASI KIDOGO NIMEAMUA NIONGEZE CHAKULA ILI NA NYIE MPATE JAPO SIKUKUU IENDE VIZIRI. LETA VYOMBO UPAKUE CHAKUALA HIKI HAPO KAMA UNAVYOONA.

Mara wife yuko ndani anachukua hotpot na mabakuli. Kaelekea kwa mwenye nyumba na baada ya mda karudi na pilau kuku, ndizi za kupika na kachumbari. Kaweka mezani wala hakunusemesha. Nami nikachuna tu. Kamwita dogo akasogea kampakulia chakuala, mimi nimekomaa na TV kama kipofu vile.

Kwa kweli nilijisikia aibu sana sana. Kuzuga nikajifanya naenda dukani kununua soda (nilichukua matupu manne). Sikupita kwa mangi nikala chocho nikatikeza mtaa wa pili. Nikaelekea kwa mshikaji wangu, yeye alikuwa bachela, hajaoa. Bahati nikamkuta nae kachili tu. Nikampa stori nzima.

Mwanangu akasononeka sana. Kaanza kunikumbusha mambo ya longi mara ooooo, huyo demu wako usingezaa nae tulukwambia sio wife material unaona sasa... Tukapiga stori pale za kutosha. Kumbe mwenzangu asubuhi kapiga zake supu hana shida.

Ikabidi nijikaze kiume, tena ukizingatia niko na mwana. Nikampa live sina hata jero na kazini hatujalipwa, tena sijala. Mwana akanielewa. Akasema kuhusu wife shauri yake... Akanitoa tukaenda kupiga kitimoto choma bwana... Baada ya hapo gambe likaanza hadi saa tano usiku nakumbuka nyumbani. Hapo simu nilizima ttka mchana. Kurudi home wife kafungua mlango mimi direct kitandani hakuna neno hata moja. Kesho yake wife anaomba msamaha. Nikaona isiwe tabu ni maisha tu nikammsamehe.
Sijui kwanini huwa sipendi ugomvi wa makelele!.
pole mkuu ndo maisha
 
Kuna Christmas moja niliilia kwenye kota za police, sitosahau. Ilikuwa napenda sana kwenda kusherekea Christmas na mwaka mpya kwa bibi ifakara. Sasa kipindi hicho hakuna usafiri zaidi ya train ya tazara. Hakuna barabara za kueleweka dar-ifakara unaweza hata tumia wiki kwa gari. Tar 24 nikapandishwa train nakumbuka nilikuwa mdogo saana ila kuna mtu nilikabidhiwa anishushe ifakara pale nitapokelewa na bibi. Sijui nilijichanganya vipi nikapoteana naye kwenye train, na safari ilikuwa usiku. Chuma imetembeeaa, kumbe nimepitiliza kituo nikaja kuuliza kumbe tumeshapita kama vituo vitatu nyuma almost 80kms, usiku kama wa saa saba. Abilia wakamwambia TTE, anishushe sehemu inaitwa mngeta. Ni giza sijawahi ona mvua inanyesha. Nimeshikilia mikate ambayo nilimbebea bibi.
Kile kisehemu ni mji mdogo sana, train ilivyoondoka watu wote wakapotea nikabaki nimekaa karibu na ofisi ya mizigo nalia tu. Akaja askari mmoja sijui wa tazara yule, nikamuelezeaa. Akanichukua akanipeleka kwake nalia tu hata kula sili, nimekumbatia mikate yangu. Simu hakuna ikabidi kesho yake wakatumia zile simu za tazara kupiga ifakara wakaunganisha na simu za posta, ndo nikaongea na bibi hiyo ilikuwa next day jioni. Watoto wakawa wamenizunguka wananishangaa tu nimepotea.
Nilikataa kula chakula chao nilikula tu mkate kidogo, jioni wakanipeleka kanisani (catholic) lipo milimani hivi. Kule nilibahatika kuna gari ya mapadre lilikuwa linaenda ifakara kesho yake.
Nilifika kwa bibi nimechoka sana na mikate imeharibika. Ile Christmas ilikuwa ya mateso sana kwangu
 
Daaaa! Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni krismasi ndio inafika, mimi ni muajiriwa mahali fulani kipindi hicho. Halafu ndani naishi na mwanamke japo si wa ndoa na tuna mtoto mmoja. Sikukuu inafika sina kitu mfukoni na kazini hatujalipwa.

Sasa wife anasisitiza tununue chochote hata ikiwezekana tukope. Nikiangalia sioni shehemu ya kukopa. Nikamwambia wife kakope kwa mangi maharagwe tu leo tutakula tusubiri sikukuu ya mwaka mpya nitajipanga. Wife Kagoma hadi ikawa kelele ndani. Mara karopoka leo sili (mimi) na wala hapiki chochote.

Kumbe bwana mama mwenye nyumba alikuwa anasikiliza tu. Nilikuwa nimepanga nyumba tunaishi na mwenye nyumba nyumba moja kasoro vyumba tu, si unajua uswahilini.

Nikachukulia mzaha nikatulia ndani nacheki TV chaneli kama zote nabadili tu, sina ramani kabisa ya kutoka siku hiyo. Basi bwana mama mwenye nyumba kwa huruma zake kumbe kapika na ziada. Mida ya saa nane mchana nasikia anamwita wife. Hapo ni kwamba dogo (mtoto wetu) kakotogewa uji mchache asubuhi na mimi hata sikutaka kuuonja. Ndani kuna unga, mchele, viazi mviringo dagaa na mafuta ya kupikia. Mkaa upo na gesi tulikuwa nayo, kwa hiyo ilikuwa ni maamuzi tu ya wife kupika.

Wife katoka kwenda chumba cha mama mwenye nyumba, sikujua kaitiwa nini. Masikio hayana pazia bwana. Nikasikia akamwambia wife: NILISIKIA MABISHANO YENU NA MUMEO. KWA BAHATI MIMI NINA NAFASI KIDOGO NIMEAMUA NIONGEZE CHAKULA ILI NA NYIE MPATE JAPO SIKUKUU IENDE VIZIRI. LETA VYOMBO UPAKUE CHAKUALA HIKI HAPO KAMA UNAVYOONA.

Mara wife yuko ndani anachukua hotpot na mabakuli. Kaelekea kwa mwenye nyumba na baada ya mda karudi na pilau kuku, ndizi za kupika na kachumbari. Kaweka mezani wala hakunusemesha. Nami nikachuna tu. Kamwita dogo akasogea kampakulia chakuala, mimi nimekomaa na TV kama kipofu vile.

Kwa kweli nilijisikia aibu sana sana. Kuzuga nikajifanya naenda dukani kununua soda (nilichukua matupu manne). Sikupita kwa mangi nikala chocho nikatikeza mtaa wa pili. Nikaelekea kwa mshikaji wangu, yeye alikuwa bachela, hajaoa. Bahati nikamkuta nae kachili tu. Nikampa stori nzima.

Mwanangu akasononeka sana. Kaanza kunikumbusha mambo ya longi mara ooooo, huyo demu wako usingezaa nae tulukwambia sio wife material unaona sasa... Tukapiga stori pale za kutosha. Kumbe mwenzangu asubuhi kapiga zake supu hana shida.

Ikabidi nijikaze kiume, tena ukizingatia niko na mwana. Nikampa live sina hata jero na kazini hatujalipwa, tena sijala. Mwana akanielewa. Akasema kuhusu wife shauri yake... Akanitoa tukaenda kupiga kitimoto choma bwana... Baada ya hapo gambe likaanza hadi saa tano usiku nakumbuka nyumbani. Hapo simu nilizima ttka mchana. Kurudi home wife kafungua mlango mimi direct kitandani hakuna neno hata moja. Kesho yake wife anaomba msamaha. Nikaona isiwe tabu ni maisha tu nikammsamehe.
Baada ya hapo gambe likaanza hadi saa tano usiku nakumbuka nyumbani. Hapo simu nilizima ttka mchana. Kurudi home wife kafungua mlango mimi direct kitandani hakuna neno hata moja. Kesho yake wife anaomba msamaha. Nikaona isiwe tabu ni maisha tu nikammsamehe.😂
FB_IMG_1735111528775.jpg
 
Leo ni sikukuu ya Christmas .. Siku kubwa ulimwengu kote.. Kwa wiki nzima hii yametokea matukio ambayo yatakuwa ni simulizi za kukumbuka miaka mingi iijayo
Mimi ninazo simulizi mbili nawe kama unayo uta share nasi

Ukata Christmas ya 1993
ilikuwa kipindi cha Mkapa
Tumeshamaliza chuo tulitakiwa kwenda jeshini kisha ajira.. Serikali ikawa haina hela za kutupeleka jeshini wala kutupa ajira.. Ule msoto ule wee acha tu
Ikawa sasa ni mwendo wa vibarua... Na kutembelea fursa..wakati fursa kubwa kipindi cha Christmas ukiachana na vyakula toka mikoani ni miti ya Christmas
Sasa hii kwetu ipo mingi sana hivyo unakata tu bila kulipa chochote
Nikapanga na jamaa yangu yeye huko mkoani akate akodi fuso apakie mimi nitapokea mzigo Ubungo palipokuwa kituo kikuu cha uuzaji
Timing ya miti ya Chtistmas ilikuwa ni siku nne za mwisho kabla ya sikukuu yenyewe
Logistics na kukata na kupakia zikatuchelewesha kwa siku moja nzima!
Fuso likaingia Ubungo tarehe 24 mchana... Pakiwa pamefurika miti😂 tena mizuri kuliko yetu
Hatukuweza kuuza hata miti kumi kati ya miti zaidi ya 150 tuliyobeba
Fuso hatukuwa tumelipia hata senti.. Tuliukimbia ule mzigo tukamtelekeza dereva na konda wake pale Ubungo Tanesco
Uzuri hakukuwa na simu za mkononi.. Walimiliki wachache tena matajiri
Kwetu sisi siku kama ya leo tarehe 25.12.1993 ilikuwa siku mbaya ya kukumbukwa daima
Mwisho wa simulizi ya kwanza
Mkuu rekebisha 1993 ilikuwa kipindi cha mwinyi.
 
Nakumbuka krismass ya mwaka 2003 nikiwa na miaka 10, maandalizi yalianza vizuri nimenunuliwa nguo na viatu fresh nasubiri ifike siku nikaringishie wenzangu kanisani kama unavyojua utotoni. Tarehe 24 usiku wa manane mtu anakuja kugonga nyumbani baba akatoka kumsikiliza.

Baba alikuwa na gari yake ya mizigo na dereva wake alikuwa mdogo wake kabisa, alimwambia kipindi cha sikukuu asifanye kazi hadi ipite, kumbe bamdogo kapata mzigo bila kumwambia mzee kaondoka zake bahati mbaya wakapata ajali yeye baba mdogo aliumia vibaya na mwenye mzigo akafa pale pale gari nyang'anyang'a ndio usiku ule mzee analetewa taarifa.

Kesho yake Krismasi mzee alienda msibani kwa yule mwenye mzigo maana alikuwa muislam walizika siku hiyohiyo, mama alishinda amejifungia chumbani analia siku nzima. Mimi ndio nipo nipo sina la kufanya hata nguo mpya sikupewa nivae wala hakukupikwa pilau. Siku ilikuwa ya majonzi mno bado naikumbuka kama jana vile.
 
Daaaa! Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni krismasi ndio inafika, mimi ni muajiriwa mahali fulani kipindi hicho. Halafu ndani naishi na mwanamke japo si wa ndoa na tuna mtoto mmoja. Sikukuu inafika sina kitu mfukoni na kazini hatujalipwa.

Sasa wife anasisitiza tununue chochote hata ikiwezekana tukope. Nikiangalia sioni shehemu ya kukopa. Nikamwambia wife kakope kwa mangi maharagwe tu leo tutakula tusubiri sikukuu ya mwaka mpya nitajipanga. Wife Kagoma hadi ikawa kelele ndani. Mara karopoka leo sili (mimi) na wala hapiki chochote.

Kumbe bwana mama mwenye nyumba alikuwa anasikiliza tu. Nilikuwa nimepanga nyumba tunaishi na mwenye nyumba nyumba moja kasoro vyumba tu, si unajua uswahilini.

Nikachukulia mzaha nikatulia ndani nacheki TV chaneli kama zote nabadili tu, sina ramani kabisa ya kutoka siku hiyo. Basi bwana mama mwenye nyumba kwa huruma zake kumbe kapika na ziada. Mida ya saa nane mchana nasikia anamwita wife. Hapo ni kwamba dogo (mtoto wetu) kakotogewa uji mchache asubuhi na mimi hata sikutaka kuuonja. Ndani kuna unga, mchele, viazi mviringo dagaa na mafuta ya kupikia. Mkaa upo na gesi tulikuwa nayo, kwa hiyo ilikuwa ni maamuzi tu ya wife kupika.

Wife katoka kwenda chumba cha mama mwenye nyumba, sikujua kaitiwa nini. Masikio hayana pazia bwana. Nikasikia akamwambia wife: NILISIKIA MABISHANO YENU NA MUMEO. KWA BAHATI MIMI NINA NAFASI KIDOGO NIMEAMUA NIONGEZE CHAKULA ILI NA NYIE MPATE JAPO SIKUKUU IENDE VIZIRI. LETA VYOMBO UPAKUE CHAKUALA HIKI HAPO KAMA UNAVYOONA.

Mara wife yuko ndani anachukua hotpot na mabakuli. Kaelekea kwa mwenye nyumba na baada ya mda karudi na pilau kuku, ndizi za kupika na kachumbari. Kaweka mezani wala hakunusemesha. Nami nikachuna tu. Kamwita dogo akasogea kampakulia chakuala, mimi nimekomaa na TV kama kipofu vile.

Kwa kweli nilijisikia aibu sana sana. Kuzuga nikajifanya naenda dukani kununua soda (nilichukua matupu manne). Sikupita kwa mangi nikala chocho nikatikeza mtaa wa pili. Nikaelekea kwa mshikaji wangu, yeye alikuwa bachela, hajaoa. Bahati nikamkuta nae kachili tu. Nikampa stori nzima.

Mwanangu akasononeka sana. Kaanza kunikumbusha mambo ya longi mara ooooo, huyo demu wako usingezaa nae tulukwambia sio wife material unaona sasa... Tukapiga stori pale za kutosha. Kumbe mwenzangu asubuhi kapiga zake supu hana shida.

Ikabidi nijikaze kiume, tena ukizingatia niko na mwana. Nikampa live sina hata jero na kazini hatujalipwa, tena sijala. Mwana akanielewa. Akasema kuhusu wife shauri yake... Akanitoa tukaenda kupiga kitimoto choma bwana... Baada ya hapo gambe likaanza hadi saa tano usiku nakumbuka nyumbani. Hapo simu nilizima ttka mchana. Kurudi home wife kafungua mlango mimi direct kitandani hakuna neno hata moja. Kesho yake wife anaomba msamaha. Nikaona isiwe tabu ni maisha tu nikammsamehe.
Ulifanya la maana kutoka nyumbani
 
Mkuu tunakusubiria , utupe muendelezo .
Simulizi ya pili
Hii ni 1994. Nimefanya Kazi kwa mtu kule SABASABA mpaka tar.20.. Nikaambiwa mshahara tar 23.. Kumbe tajiri kajipanga kuondoka tar 22.. Nafika kwake tar 23 naambiwa kaondoka jana kwenda mkoani😭 sikuwa na pesa kabisa
Aliyenikoa ni bibi mmoja aliyekuwa anauza maji pale SABASABA (sikuwahi kumlipa wema wake ule) alinipa shiLingi 5000 ilikuwa kubwa sana kipindi Hicho
Sasa ni tarehe 23 natakiwa kusafiri tar 24 kwenda kijijini kwa ajili ya Xmas
Basi kujiongeza nikapata mchongo wa maembe huko Chanika Mvuti
Nikafanikiwa kupata 20 ya mkopo mahali.. Nikawa na 25 sasa.. Nikaenda zangu Mvuti
In short mpaka saa tatu usiku nilikuwa Buguruni na tenga langu la maembe nikiwa nimeshatumiq kama elfu 22 hivi gharama zote na matarajio ni kupata 45 hivi
Ugeni kwenye biashara jambo baya sana.. Nikaambiwa yale maembe yangu yanaweza kununuliwa kwa jumla elfu 25 tuu ama sivyo nikomae mwenyewe niuze mojamoja
Baada ya mabishano ya muda mrefu nikashindwa mimi inabidi nikubaliane nao
Sheshe likaja kwenye kuyamwaga chini yakaguliwe😭😭😭
1. Nilichomekewa maembe mabovu almost robo tenga
2. Waliweka majani mengi chini ya tenga..
Niliambulia Shilingi elfu 9000.tuu.
 
Back
Top Bottom