Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 60,050
- 104,466
Mimi nakaa Dar uswahilini, lakini hapo uswahilini kwangu ni kama pa kishuwa, basi nikienda mitaa ya uswahilini kwenyewe sasa kwenye skwata magenge yao karoti inakatwa vipande na hoho inakatwa vipande, hapo kipande sh 50 ushindwe mwenyewe.Kama ulidhani ulielewa somo la fraction au decimal jitafakari
Kuna robo ta robo
Watu wa mikoani huwa wanashangaa watu wa mjini kula miguu,utumbo na vichwa vya kuku,ule sio umasikini bali ni utamaduni tu.ndiomaana mtu wa pwani yuko tayari kuacha kula wali akala matandu au ukoko.
Kuna kabila moja wanakula wale wadudu jamii ya panzi,sasa bwana mmoja toka hilokabila akasafiri jwenda mkoa X akakuta jamaa wanakula njiwa,akawabeza sana kuwa mnakula tunjiwa tudogo hivi,wakamwambia kati ya njiwana senene kipi kikubwa....
Nilikuwa likizo mkoa Y maduka ya huku kuna hadi kipimo cha sukari ya sh 200,sijajua ni utamaduni au umasikini,yaani rob9 kilo inagawiwa maranne au zaidi kupata hiyo sukari ya 200.
Mafuta ya kula halikadhalika yapo hadi ya 100
Life is good
Hapa kwenyewe nimeshapiga supu ya maharagwe jero, chapati 2 sh 600 jumla 1100 breakfast ya nguvu.
Ukishindwa kuishi uswahilini usiitamani Masaki maishani kwako, mshikaki tu buku 3.