Kuacha alama kwa mpenzi wako uliyemsaidia katika maisha ni muhimu

Kuacha alama kwa mpenzi wako uliyemsaidia katika maisha ni muhimu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Huwa na tatizo la kupenda na kutamani wanawake wazuri wazuri; nimejaribu kulikemea hili pepo, lakini haliondoki.

Mwezi uliopita, nikiwa kwenye mishe mishe zangu, nikakutana na dada mmoja, ni mtu mzima, na kwa uzuri aliokuwa nao, ukanishawishi nipambane niweke kituo; tukasalimiana, nikawa najaribu anielekeze maeneo fulani; ila lengo langu ni kupata namba.

Baada ya kunielekeza; nikamshawishi, na akanipatia namba.

Tukawa tunawasiliana, na kuendelea kufahamiana zaidi. Hajaolewa ila ana mtoto mmoja, pia ameajiriwa kwenye kampuni ya mtu binafsi.

Nikatafuta jumamosi moja, nikamtoa 'out' ili tuweze kuzungumza zaidi. Mbaya zaidi, wote ni wanywaji, tukawa tunapiga chupa na vitafunwa huku tukibadilishana mawazo.

Katika mazungumzo, nikaona ameanza kubadilisha sauti, na kuleta sauti ya kudeka deka, mara akaanza kuniita 'baby'; kusikia hivyo, nikajisemea kimoyo kimoyo, hili ni zigo langu.

Akasema,''baby, natamani niache kazi; kwa kasababu hii kazi ninayoifanya, inanichosha sana, na sifurahii maisha, nakuwa mtumwa''. Nikamuuliza unata ufanye nini, ukiacha kazi? Akanijibu biashara.

Akaendelea,'' Baby, naomba uniongezee mtaji''. Nikamuuliza kiasi gani? Akaniambie milioni 7.

Mwili ukashtuka ghafla, nikaanza kutafakari, mi nitanufaika na nini kama nitatoa hiyo fedha.

Nikamjibu; nizalie kwanza mtoto; ukibeba mimba ikiwa na miezi minne nakupatia tatu, na ukijifungua namalizia nne.

Akaniambia, haina shida.

Kwa nini nilimuambia hivyo? Kwa sababu hawa watu wakifanikiwa huko mbele huwa wanasahau walikotoka; ni bora uache alama.​
 
Huwa na tatizo la kupenda na kutamani wanawake wazuri wazuri; nimejaribu kulikemea hili pepo, lakini haliondoki.

Mwezi uliopita, nikiwa kwenye mishe mishe zangu, nikakutana na dada mmoja, ni mtu mzima, na kwa uzuri aliokuwa nao,​
Milioni 7 kwa malezi ya mtoto maisha yako yote! Ngozi nyeusi kuendelea hakuna!
 
Kwahiyo umeridhia kutoa hiyo million 7 kwa kigezo cha kupata mtoto kati yake na wewe? ...
Kwa ulimbwende alionao, itabidi kuacha alama mkuu; salio litakuwa advance kwa malezi ya mtoto kama atazingua huko mbele
 
Kwa ulimbwende alionao, itabidi kuacha alama mkuu; salio litakuwa advance kwa malezi ya mtoto kama atazingua huko mbele
Kwanini usioe tu mkuu ili hilo lifanyake mkiwa ndani ya ndoa, pia itakuwa rahisi kwako ku-monitor hicho anachotaka kukifanya, million 7 is huge amount to give someone kwa mipango ya mdomoni tu.
 
Kwanini usioe tu mkuu ili hilo lifanyake mkiwa ndani ya ndoa, pia itakuwa rahisi kwako ku-monitor hicho anachotaka kukifanya, million 7 is huge amount to give someone kwa mipango ya mdomoni tu
Nilishaoa mkuu, na nina watoto wakubwa; huyu ni mpenzi wa kando moyo umeteketea, kutokana na hitaji lake, naye inabidi akubaliane na hitaji langu
 
Ok mkuu nisikuingilie sana may be kwa kipato chako 7 million is just a peanut to give someone
Ni kubwa mkuu, ndio maana nikampa mtihani kuwepo na alama, ili hiyo biashara imsaidie mtoto.
 
Back
Top Bottom