Kuachiwa kwa Sanga ni moja ya maridhiano aliyosema Mbowe, hata kama hatumpendi lakini apewe heshima yake

Kuachiwa kwa Sanga ni moja ya maridhiano aliyosema Mbowe, hata kama hatumpendi lakini apewe heshima yake

Hivi ni mimi ambaye naona kuna jambo halipo sawa ? Kama mtu hastahili kuwekwa ndani kwanini awekwe ndani in the first place ? Na kama anastahili / alistahili kuwekwa ndani kwanini aachiwe hata kama ni maridhiano ?

Nadhani badala ya kutatua matatizo yaliyopo tunaongeza matatizo kwa jina la kufanya utatuzi....
 
Ingekuwa maridhiano angetolewa na DPP kama Mbowe. Ila Sanga kashinda kesi ya uonevu iliyofubguliwa na serikali dhalimu ya CCM . Halafu hakuna maridhiano kwenye haki ya mtu. Nashangaa Mbowe abayeshangilia kupata Ruzuku kisa maridhiano.
 
Bila "maridhiano" unaamini angeshinda ?

"...mtu yeyote wa Serikali anaweza kumpigia simu jaji akamwambia huyo usimpe hukumu hiyo, usimpe haki yake"

- Rostam (ulimi ulipoteleza)
Sanga ni Tishio kwa nani?
 
Katika moja ya mambo ya maridhiano baina ya Chadema na Mhe.Rais ilikuwa inahusu wafungwa wa kisiasa, Chadema waliomba mchakato wa kisheria uweze kufanyika ili watu wao waliokuwa magerezani waachiwe.

Mbowe aliliongea suala hili akipinga wale waliokuwa wanadai kuwa maridhiano hayakuwa na tija wala faida yoyote.Kimsingi Lissu ndio alisema maridhiano hayana maana na hayakuwa na faida.

Mbowe alikana maridhiano kutokuwa na faida, alisema yapo mambo walifanikiwa na yapo ambayo hawakufanikiwa.

Moja ni hili la watuhumiwa wao kuachiwa magerezani, kweli waliachiwa wote wakabakia mawili, hata Kinana alipokuwa makamu mwenyekiti wa CCM alitolea ufafanuzi suala hilo, waliobakia walikuwa na kesi za mauaji na zilikuwa zinaendelea mahakamani ikiwemo hii ya Sanga.

Kwahiyo hata Sanga kuachiwa leo na mahakama naweza kutabiri kuwa ni utekelezaji wa yale maridhiano ya kipindi kile.

Hivyo naona kabisa maridhiano ya kisiasa ni muhimu sana kuliko kama anavyodhani Lissu,ambaye ni msomi mzuri asiyekuwa na maarifa.

Kwa sababu hata huko ulaya, nchi zinapigana vita huku zikiendelea kukaa mezani.Huwezi kusema maridhiano hayana maana.
Kwa hiyo mtu akionewa, halafu akashtakiwa halafu akaachiwa. Waliomuonea/dhurumu haki yake wanapongezwa kwa kuachiwa mtuhumiwa?! Hivi ni vituko!
 
Karibu Tena uraiani collegemate...miaka minne ya gerezani sio mchezo kabisaa...
 
Maridhiano huku Soka na wenzie hadi leo hawajulikani walipo? Hayo yote si yametokea baada ya hayo yaliyoitwa maridhiano?

Namuunga mkono Lissu, Mbowe ni simba mzee aliyeishiwa mbinu.
Wote ni wazee
1. FA Mbowe-1961..........umri 63.......baba yake alikuwa ni mwana CCM, kakulia kwenye CCM akajikita kwenye biashara. Aliwahi kutaka kujimilikisha sehemu mojawapo ya eneo la mnazi mmoja, akazungushia uzio wa bati tayari kuanza ujenzi, lakini kuna waziri mmoja machachari (RIP) alitibua hilo.
2. TA Lissu-1967...........umri 57..................ana washabiki kutoka ndani ya CCM, ni mwana CCM ijapokuwa halipii kadi. Asingekuwa mwana CCM asingechaguliwa kujiunga na chuo kikuu cha serikali.
 
Back
Top Bottom