Kuamka asubuhi na kukuta sehemu ya nywele au ndevu zimenyolewa

enstein1

Member
Joined
Jul 14, 2009
Posts
68
Reaction score
29
Kuna watu inatutokea unaamka asubuhi na kukuta sehemu ya nywele kiachwani au kidevu ghafla zimenyolewa kwa mtindo wa Ki/vishilingi an nywele huchelewa sana kuota tena. Hii kisayasansi inasababishwa na nini? Kuna watu wanasema uchawi lakini sipendi sana kuamini hilo!
Majibu tafadhali!
 
Duh! Duniani kuna mikasa eh! Unaamka unajikuta na mashilingi kichwani? Dah! Haiya, ngoja tusubiri maelezo ya kitaalamu. Hii mpya kwangu, sijawahi isikia.
 
Ni Kweli ukiwa umelala usiku na ukamka Asubuhi ukakuta kwenye nywele zako au ndevu zako zimenyolewa itakuwa wewe umenyolewa na wachawiwakati wa usiku umelala. Sasa unakataaa nini wakati ulipo lala kwani ulimwita kinyozi aje kukunyowa nywele zako Mkuu enstein1 Ukiamini au kutokuamini hilo ni shauri yako mwenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Mambo hayo yapo sana ya kuamka umenyolewa au hata umekatwa kucha ... Ki ufupi ni mambo ya kichawi japo hayana madhara sana zaidi ya kukupa hofu tu

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
si bora kichwani kuna swahiba wangu mmoja huko ukerewe aliamka asubuhi akakuta uvuzi wote umefyekwa.alikuwa bwana shamba mbona alikimbia kituo cha kazi
 
utakuwa umerogwa tu..hao ni wachawi..wahi kwenye ramli...

 
si bora kichwani kuna swahiba wangu mmoja huko ukerewe aliamka asubuhi akakuta uvuzi wote umefyekwa.alikuwa bwana shamba mbona alikimbia kituo cha kazi

Inashangaza haya mambo ya kijinga bado yako sana Africa. Badala ya kujipumzisha mijitu inafanya mambo ya hovyo hovyo yasiyo na tija. Sasa kunyoa watu bure bila malipo ili iweje?
 
Sasa hospital wanawezanpiga ramli? mambo ya sangoma mpelekee sangoma. hao serikali ndo wapiga ramli wakubwa mbona wanakesha kwa bibi yangu...ila tunafanya siri..

Huyu jamaa kama anataka basi nimuelekeze aje kwa bibi yangu na mambo yake yatakuwa saafi tu...

Akawahi kwa kupiga Ramli wakati Serikali imepiga Marufuku mambo ya Ramli aende Hospitali akapigiwe Ramli ya Ki-Hospitali labda Ma-Daktari wataweza kumtibu huko.
 
wewe subiri ukilogwa ndo utaamini kuwa uchawi unafanya kazi. Hv ww hawa wanaoteka albino unafikiri ni watu wadogo. Lazma uwe fisadi ndo unaweza huyo unyama..

Sipendi kuamini uchawi hata kama upo.
 
Hahahah umenikumbusha jamaa mmoja alitoka mjini kwenda kijijini kwao.....baadabya siku mbili aliamka amenyolewa kichwani sehemu tatu tofauti...yaani walimpungua haswa

Ikabidi atafute kinyozi amkwangue zote tu

Hapana chezea sayansi ya kiafrika
 
Kama una jina la YESU watakuloga hadi watachoka ila watakuona ukiwa vile vile.
wewe subiri ukilogwa ndo utaamini kuwa uchawi unafanya kazi. Hv ww hawa wanaoteka albino unafikiri ni watu wadogo. Lazma uwe fisadi ndo unaweza huyo unyama..
 
utakuwa umerogwa tu..hao ni wachawi..wahi kwenye ramli...

Kova akikusikia na wazee wako wa ramli utaunganishwa na panya road sio muda mrefu....
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka niliwahi kunyolewa kope mara kwa mara nikiwa O level miaka hiyo ila sikujua ni nani alikuwa akininyoa usiku,Namshukuru sana rafiki yangu mmoja from morogoro kuanza kunisisitiza Maombi

From there,hadi leo sijawahi tokewa na hivyo vitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…