Kumekuwa na mafundisho mengi yanayosema ni vizuri kuandika busines plan kabla ya kuanza biashara/mradi,Lakin ukifuatilia kwa undani hakuna business plan hata moja ambayo huwa inaonesha kipindi cha hasara,Na ukifuatilia biashara nyingi hufa ndani ya mwaka wa kwanza,Na wakati huo mtu ana business plan mkononi inayoonyesha angepata faida kubwa saaaana,Nakushauri anza biashara yako hata bila ya business plan,Biashara ni vitendo sio faida ya kwenye makaratasi.Uliza wafanyabiasbara waliofanikiwa Kama walianza kwa kuandika business plan.. ANZA LEO BIASHARA,USINGOJE KESHO.
Business plan au kwa lugha ya kiswahili Mchanganuo wa biashara, kwa uelewa wangu una kazi zifuatazo.
1. Kumuongoza mtu na kumpa mchanganuo wa biashara anayotaka kuifanya.
Mfano unataka kuanzisha biashara ya kukamua mafuta ya alizeti huezi ukarupuka na kusema 10mil inatosha, lazima ukae ufanye tafiti kidogo, na hapa sio una assume prices, lazima uweke price zilizo realistic, mfano:
-je mashine za kukamua alizeti ni bei gani
-mashine inakula umeme kiasi gani
-chupa unazotumia kupack mafuta yako iwe 1ltr, 3ltr, 5ltr ni shingapi
- labels nazo bei gani
-je gunia la alizeti ni how much(kipindi cha on season bei iko chini/off season bei iko juu)
-mafuta utauza bei gani
-mashudu utauza bei gani
Hizi ni factors chache tu sio lazima kuichambua hii biashara in deep
2.kazi nyingine ya business plan inamsaidia mtu apewe mkopo(loan), kma wewe ni mfanya biashara na unataka uchukue loan kubwa ya ku grow au ku expand lazima business plan ihusike, hyo business plan itaandikwa kwa kutokana mtiririko wa financial records zako, toka uanze biashara, kma una previous loans umewahi ku clear vizuri au kudefault n.k, hii business plan ndo itakukingia wewe kifua uweze pata mkopo bank wa kutanua biashara yako. Washanya biashara wakubwa wengi wakifika stage ya ku expand their businesses lazima watumie business plans, kuna mashirika mengi wanaandika business plans na kuwasaidia watu wapate mkopo.
3. Business plan inamsaidia mfanya biashara aweze kupata wawekezaji(investors), bila business plan, huwezi kumshawishi mwekezaji aingize pesa kwenye biashara yako, lazima umpe business plan, una pitch(present) business plan mbele yake, au pannel akiwa convinced anawekeza pesa in ur venture
4. Business plan, inatumika kumsaidia mtu apate grants (ruzuku), kuna organization nyingi tu zinatoa grant funding, but lazima uwe na mchanganuo wa biashara.
Naongea with experience, kma entrepreneur, bcz nishapitia process ya kutafuta loan, nishajaribu kutafta investors, na pia nishawai kuandika kuomba grants na nikapata grant funding three times.
Lakini kama unafanya a normal business sio lazima uingie deep kuandika professional business plan, fanya tafiti, zijue gharama zote (costs) jua mauzo yako (sales), then chukua sales minus costs upate faida (profit) haina haja kuandika professional business plan, dont complicate.
Mwisho wa siku uwe na business plan au usiwe nayo haina maana kwamba, huwezi pata loss.
Japo kuna kipingele kwenye business plan inaitwa SWOT analysis (Strengths, Weakness, Opportunities, Threats) kwenye Weakness and Threats hapo ndo unaelezea possible conditions zinazoweza kukuletea hasara.
kuna unforseen events nyingi zinaweza kukuletea hasara, theft, kutapeliwa,mashine breakdowns, gari kupata ajali wakati una safirisha na products kuharibika n.k
Note: Huo ndo uelewa wangu, siongei kama consultant kwamba nimejaribu kujitangazia indirectly nipate watu niwaandikie business plans, hua nikiandika B.P hua i do it for my own use.
Sent using
Jamii Forums mobile app