Kuanza kuhusisha siasa kumtengenezea Muuaji kadi ya Chadema ama kuonyesha UCCM wake ni ushamba

Kuanza kuhusisha siasa kumtengenezea Muuaji kadi ya Chadema ama kuonyesha UCCM wake ni ushamba

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
BINAMU HIMSELF: TUKIO LA MAUAJI SALENDER BRIDGE JANA

Tukio la mauaji Salender Bridge jana

Kumekuwa na hisia na hukumu nyingi kuhusiana na tukio la jana lililopoteza maisha ya watu watano. Ugaidi, kisasi, chuki vimetajwa kama sababu na baadhi ya wengi, Ilimradi kila mmoja amesema anavyodhani ni sawa.

Kiujumla ni tukio baya, linaloleta picha mbaya ndani na nje ya nchi. Ni tukio ambalo tukiruhusu kila mmoja atoe hukumu yake, aongee apendavyo balaa lake liko mbeleni maana watu wataikataa ripoti ya kipelelezi ambayo Mh Rais ameagiza itolewe haraka.

Wakati palishakuwa na hali ya utulivu Dar es Salaam baada ya mabadiliko yaliyofanywa ktk jeshi la Polisi jambo hili lisipofuatiliwa kwa umakini litaleta doa. Je ni kweli polisi walitaka kumdhulumu dhahabu zake? Je ni suala la ugaidi? Je ni tatizo la kiakili? Yote tuyasubirie yatolewe na wahusika.

Kuanza kuhusisha siasa (kumtengenezea Muuaji kadi ya Chadema ama kuonyesha UCCM wake ni ushamba). Maana hakuna chama kinachoweza kuhimiza mauaji ya watu wake. Kama mtu ni MUOVU ashughulikiwe kama YEYE BINAFSI na sio taasisi, dini ama kabila lake.

Ni imani ya kila mmoja kwamba wenye jukumu la kuitoa ripoti ya tukio hilo WATAISIMAMIA KWELI kwa faida ya nchi. Kama ni ugaidi hatua stahiki za kuufuatilia mtandao huo zichukiwe na kama kuna huo uchafu wa dhuluma nao usemwe maana kuna wasio waaminifu.

Nirudie kulipongeza Jeshi la Polisi kwa namna walivyokabiliana na tukio hilo, lakini niupongeze ushujaa binafsi wa askari walioonekana katika video clips namna walivyokabiliana na Bwana Hamza.

Tuombe pia wakati huu wa uchunguzi ukiendelea familia ya kina Hamza isielemezewe uovu wakati wa kutafuta kiini cha jambo hili. Wabaki kuwa wasaidizi muhimu kwa dola na sio watuhumiwa muhimu.


BinamuHimself!

IMG-20210826-WA0017.jpg


IMG-20210826-WA0012.jpg
 
Tutasikia mengi sana kuhusu huyo jamaa
 
Nilishangazwa sana kuona baadhi ya Member niliokua nawaona wapo vizuri kichwani, kushindwa kuona kama picha hiyo ya Mwisho kua nI Fake, NILISHANGAA SANA.
 
Nilishangazwa sana na baadhi ya Member niliokua nawaona wapo vizuri kichwani, kushindwa kuona kama picha hiyo ya Mwisho kua na Fake, NILISHANGAA SANA.
Tatizo watu walifagilia uchama kwenye tukio hilo na kuongeza porojo nyingi ili kukilaumu chama kimoja.
 
Pia tuchukue nafasi hii kumpongeza kijana mwenzetu kusimamia anachoamini na kukataa dhuluma mpaka amedondoka na wanne kwa upendo kabisa. A moment of silence please for Mr Hamza
 
Back
Top Bottom