Kuanzia Januari 2022 ni mwendo mdundo -Tume huru ,mkiguna Tunaguruma na katiba Mpya

Kuanzia Januari 2022 ni mwendo mdundo -Tume huru ,mkiguna Tunaguruma na katiba Mpya

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
1,958
Reaction score
3,890
Viongozi mliopo serikalini mkae mkijua,kuwa linaloanza kutoa mvuke karibu litashika kasi,kinachohitajika ni tume huru ya Uchaguzi ,na hili halina mswalie Mtume,Hii kero imeshapevuka na sasa kama ni jipu linakaribia kupasuka.

Na Mliopo madarakani msiingizwe mkenge na CCM,nikimaanisha CCM kama Chama na sio Serikali iliyopo madarakani.Serikali ni ya wananchi wote kama alivyo Raisi mara tu baada ya kuapishwa yeye na serikali yake hutakiwa kuwahudumia wananchi wote bila ya kujali itikadi za vyama vya wananchi hao.

Wananchi wote sasa wanasema umefika wakati wa kuwa na Tume huru ya Uchaguzi inayojiamini kama ilivyomihimili mingine. Hii Tume iundwe na kuanzia january 2022,kila mkoa utajiimarisha katika kudai Tume huru ya Uchaguzi.

Na hili litasaidia vyama vyote ikiwemo CCM ,maana kumekuwa na uenguaji wa wapendwa wetu kutoka CCM huenguliwa na kusababisha mtafaruku ndani ya Chama na kama haitoshi hata kukigawa Chama,mifano hai ipo tele.

Dawa ni Tume huru,yale mambo ya kuenguliwa kihuni wakati hakuna kisichorekebishika yawepo,sijui unaenguliwa kwa tu umekosea herufi na upumbavu mwingi usio na maelezo.

Ukiingia kwenye kuhesabu kura nako polisi wamejaa utasema ni majeshi ya kukodiwa kiasi ya kusababisha maafa yasio na sababu za msingi.
Tume huru ni wito na jambo linalotaka kupewa kipau mbele,anaeshinda awe ameshinda bila ya mizengwe,malalamiko yasiwepo kwa asilimia 99 kama chaguzi zilizopita.

Mdharau mwiba mguu huota tende na siku hizi mdharau kipele hutibu kensa.
 
Wale viranja wa vyama vya siasa vilivyo rizevu,visikae na kushupalia mambo ya CCM wakienguana wakilipuana wakitumbuana hayo ni yao ,jamani mnasahau misemo yetu ya kiluga ...eti Vita vya panzi ....?

Hii Michawa au mipanzi iliyojaa ndani ya Serikali ya Tanzania iwacheni kama ilivyo,tunaona ni jinsi gani wanavyoivuruga nchi.

Tunahitaji sasa wimbo wa Taifa uwe ni madai ya Tume huru ya Uchaguzi mpaka kieleweke,tunasubiria huo mkutano wao walioupanga kati ya polisi msajili na vyama husika, huwaga najiuliza JWTZ hawahusiki na usalama wa nchi maana nchi inapovurugika wao ndio hupata shida,polisi huingia mitini. Katika huo mkutano ni lazima na wao wahusishwe ili tusikie neno kutoka kwao.

Zaidi ya yote viranja sasa ni mwendo mdundo kudai Tume huru ya Uchaguzi kipimo ndani ya mwaka mmoja kijulikane,sio mnakaa mpaka Jua linazama ndio mnaibuka kuwaambia wananchi ,hatuitambui tume lakini twendeni kwenye uchaguzi.

naona sasa hivi akina Mbatia,Zito wanajikita katika mambo ya CCM kama wao ni wanachama wa CCM,hayo ya CCM na michachariko yao hayawahusu,kwa sasa wao ni kujikita kwenye Dai kuu la Nchi hii la Kupata Tume huru ya Uchaguzi.
 
Mtakoma mwaka huu. Tuliwambia Uhuru wa tume na katiba bora mkatuponda. Wakati mtakapoihitaji sisi tutakuwa tumeshahamia agenda nyingine.

CCM mnachelewa sana kuelewa.

Msiwe kama Kenge Kibabo kidogo kwa mama mmeanza kulia.
 
Isipoundwa wahusika watafanywa Nini? Kwa Sheria na nguvu ya dola ipi?

Mambo muhimu kama haya ya kikatiba marekebisho yake yatafanyika baada ya kuchapana. Vinginevyo sahau
Huyo ni Taga siku zote amekuwa akipinga mabadiliko ya Katiba Mpya na Tume huru. Sijui leo kimemkuta nini
 
Kunnaanzwa na kuipinga tume ya uchaguzi iwe mpya au ya zamani, mpaka walio wengi wajiridhishe kuwa tume iliyokuwepo huwenda ikatenda haki.
 
Viongozi mliopo serikalini mkae mkijua,kuwa linaloanza kutoa mvuke karibu litashika kasi,kinachohitajika ni tume huru ya Uchaguzi ,na hili halina mswalie Mtume,Hii kero imeshapevuka na sasa kama ni jipu linakaribia kupasuka.

Na Mliopo madarakani msiingizwe mkenge na CCM,nikimaanisha CCM kama Chama na sio Serikali iliyopo madarakani.Serikali ni ya wananchi wote kama alivyo Raisi mara tu baada ya kuapishwa yeye na serikali yake hutakiwa kuwahudumia wananchi wote bila ya kujali itikadi za vyama vya wananchi hao.

Wananchi wote sasa wanasema umefika wakati wa kuwa na Tume huru ya Uchaguzi inayojiamini kama ilivyomihimili mingine. Hii Tume iundwe na kuanzia january 2022,kila mkoa utajiimarisha katika kudai Tume huru ya Uchaguzi.

Na hili litasaidia vyama vyote ikiwemo CCM ,maana kumekuwa na uenguaji wa wapendwa wetu kutoka CCM huenguliwa na kusababisha mtafaruku ndani ya Chama na kama haitoshi hata kukigawa Chama,mifano hai ipo tele.

Dawa ni Tume huru,yale mambo ya kuenguliwa kihuni wakati hakuna kisichorekebishika yawepo,sijui unaenguliwa kwa tu umekosea herufi na upumbavu mwingi usio na maelezo.

Ukiingia kwenye kuhesabu kura nako polisi wamejaa utasema ni majeshi ya kukodiwa kiasi ya kusababisha maafa yasio na sababu za msingi.
Tume huru ni wito na jambo linalotaka kupewa kipau mbele,anaeshinda awe ameshinda bila ya mizengwe,malalamiko yasiwepo kwa asilimia 99 kama chaguzi zilizopita.

Mdharau mwiba mguu huota tende na siku hizi mdharau kipele hutibu kensa.
Waeleze labda wataacha ubinafsi na njaa watakuelewa
 
Back
Top Bottom