Kuanzishwa kwa kodi ya sherehe Moshi ni pigo jingine kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Kuanzishwa kwa kodi ya sherehe Moshi ni pigo jingine kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
673
Reaction score
1,318
Mnamo tarehe 9/05/2024, Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ilitangaza kuanzisha kodi mpya ya sherehe katika wilaya hiyo. Kodi hii imeelekezwa kulipwa na wenye sherehe (waandaaji wa shughuli), jambo ambalo limezua mjadala mkali miongoni mwa wakazi wa wilaya hiyo. Wakazi wanahoji mantiki ya mwenye sherehe kubebeshwa mzigo wa kulipa kodi, ikizingatiwa kwamba sherehe mara nyingi si chanzo cha mapato kwa waandaaji wake.

mendez_m_c_a-20240524-0001.jpg


Swali la msingi hapa ni: Je, mwenye sherehe ndiye anayefaidi kiuchumi kupitia sherehe hiyo kiasi cha kuwajibika kulipa kodi? Kama lengo la kodi ni kukusanya mapato kutokana na shughuli za kibiashara, kwanini asiwe mwenye ukumbi wa sherehe ndiye anayelipa kodi hiyo, ikizingatiwa kwamba yeye ndiye anayepata kipato moja kwa moja kutokana na kukodisha ukumbi wake kwa sherehe hizo?

Nadhani ipo haja ya kutafuta majibu na ufafanuzi zaidi kutoka kwa mamlaka husika kuhusu uhalali na mantiki ya kodi hii mpya, ama kuwapa nafasi wananchi katika kupendekeza njia mbadala ambazo zinaweza kuwa na tija zaidi kwa pande zote.

Pia unaweza kusoma Thread 'Ili ufanye harusi au sherehe Moshi lazima ulipe Kodi za Manispaa Tsh. 230,000'
 
Kwa sababu hii ni sherehe na sheria iko wazi wakati wa malipo unapunguza kama ile ya withholding tax. Kwa mfano mziki labda ni Tsh 150,000 si unalipa 130,000 alafu unalipa 20,000 kama sheria ilivotamuka
 
 
kumbe issue ni ukumbi tu
basi tutafanyia sherehe majumbani mwetu tuone hayo matozo yenu ya kila siku
 
Hamna haja ya sherehe kubwa kubwa za kukodisha ukumbi tenaa

Shughuli za kuchangishana kwa sherehe zitapunguaa kwa baadhi ya maeneo

Kuna mdau anasema mbona hiyo kodi ni ndogo sana ukilinganisha na wanachokula kamati ya maandalizi
 
Kuna mdau anasema mbona hiyo kodi ni ndogo sana ukilinganisha na wanachokula kamati ya maandalizi
Tatizo linaweza lisiwepo katika kodi, ila tatizo ni mantiki ya kumlipisha kodi hiyo mwenye sherehe. Mfano, kuna kodi ya Tanesco ya kila mwezi lakini hata katika nyumba ya kupanga anailipa mwenye nyumba. Kwanini na hii kodi asingelipa mwenye ukumbi?​
 
Sherehe zimezidi,pesa mnayo
Kwanini wasiwatandike kodi

Ova
 
Back
Top Bottom