Kuanzishwe sajili za muda, ziitwe "Holiday signing" au "Sajili za Utalii" kwa Wachezaji Maarufu Duniani.

Kuanzishwe sajili za muda, ziitwe "Holiday signing" au "Sajili za Utalii" kwa Wachezaji Maarufu Duniani.

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Badala ya kusubiri Wachezaji wakishaacha kucheza na kupoteza umaarufu ndio Waje kama Mbalozi wa bidhaa au kampeni fulani, tufike mahali kukawa na sajili za muda ambapo Wachezaji Maarufu na wenye Mashabiki wengi Ulimwenguni kote wataweza kwenda kucheza popote pale Duniani akijiridhisha kwamba ana Mashabiki wa kutosha kwenye nchi hiyo, walau mechi moja.

Sidhani kama kuna atakayepingana na mimi kuwa Duniani kuna Ushabiki wa Vilabu na Ushabiki wa Mchezaji mmoja mmoja hata kama Mchezaji huyo anachezea timu wasiyoishabikia.

Hii ni kumaanisha ya kuwa Mchezaji ataweza kusainiwa na timu ya nchi yoyote akacheze mechi moja kwa gharama watakazokubaliana zikijumuisha na bima ya usalama wake, yaani walau mara moja kwa Mwaka Mtu kama Lewandosky anakuja kuichezea Simba mechi moja wapo ya ushindani, bila kujali atacheza vizuri au vibaya muhimu ni uwepo wake tu, baada ya hapo mkataba umeisha anarudi timu yake.
 
Lewandosky aje simba aiseee najua ni mfano tu ila itamshusha sana sana maana ana program za makocha na madaktari wake bado hali ya hewa bado ratiba za ligi yao,ucl etc yaani zote akache aje kukomba bil 20 za mo kwa dakika 30 daah

Mara munyama CR7 yulee ruvu shooting,najiuzulu kumshabikia aiseee
 
Lewandosky aje simba aiseee najua ni mfano tu ila itamshusha sana sana maana ana program za makocha na madaktari wake bado hali ya hewa bado ratiba za ligi yao,ucl etc yaani zote akache aje kukomba bil 20 za mo kwa dakika 30 daah

Mara munyama CR7 yulee ruvu shooting,najiuzulu kumshabikia aiseee
Ndio maana nikasema ni package maalumu.

Kwani hawezi kuja kutoa msaada kwa Wahitaji waliopo hapa nchini?...kwani hawezi kuja kutembelea Mbuga zetu kama Mtalii?...naye si Mtu kama hao wenzake wanaokuja kutalii?.

Na nimesema ni biashara kwa hiyo wanakaa na kukubaliana ilimradi na Wahusika huku wajiridhishe kuwa wataipata thamani ya kugharamia safari yake hiyo....hii inamaanisha na hiyo timu yake yote nao wanakuwa ndani ya mpango.

Lengo kuu linakuwa ni burudani, Utalii, Hamasa n.k.
 
Mpira ni biashara pana yenye maslah ukiigusa kidogo tu either unaharibiwa au unaharibika. Fatilia sakata la papaaa perez na ligi yake aliyotaka kuianzisha.

Wazo lako la package umetoa mfano aje kuchezea simba sio kutoa msaada. Kutoa msaada hakulipwi mkuu.

Umetoa mfano wa lendo aje acheze simba mechi ya ushindani haijalish kacheza vibaya au vizuri,unawafahamu wazee wa kubet kweli. Mechi zitakua fixed. Raha ya mchezo haitakuwepo

Wachezaji wengi wakubwa wana wadhamini na mikataba yao,hakuna mdhamini atakayekubali mchezaji kurisk career yake kiivyo. Wazo lako wapo wanaolifanyia kazi ila ni huko nchini mwao.

Labda wazo lako liwe kutoa msaada na sio package ya kulipwa acheze mechi ya ushindani.

Kama ulivyosema nao ni binadamu na binadamu anahitaji privacy so utalii haki yake atatalii kimya kimya
Ndio maana nikasema ni package maalumu.

Kwani hawezi kuja kutoa msaada kwa Wahitaji waliopo hapa nchini?...kwani hawezi kuja kutembelea Mbuga zetu kama Mtalii?...naye si Mtu kama hao wenzake wanaokuja kutalii?.

Na nimesema ni biashara kwa hiyo wanakaa na kukubaliana ilimradi na Wahusika huku wajiridhishe kuwa wataipata thamani ya kugharamia safari yake hiyo....hii inamaanisha na hiyo timu yake yote nao wanakuwa ndani ya mpango.

Lengo kuu linakuwa ni burudani, Utalii, Hamasa n.k.
 
Hii ni ndoto tu Kama ndoto zingine nyingi. Tuombe tu Muotaji aamke Mapema kabla hajafikia pointi ya kwenda Kujisaidia haja ndogo asijelowesha mashuka.....!
 
Ujinga ukikomaa huzaa upumbavu, upumbavu ukikomaa huzaa upunguwani,
Mwanangu upo na upunguwani level 6.
Tuache uoga kwani hakuna lisilowezekana chini ya jua.

Hao kina Mbape wanapenda utalii pia...waje huku bongo wacheze wapate vibe jipya...aone mazingira ya Bongo...apite Serengeti kidogo asepe.

Mambo ya kusubiri akishastaafu ndio aje wala hatuhitaji maana wakati huo kutakuwa na nyota nyingine zinawaka.
 
Back
Top Bottom