Hicho kitu hakiruhusiwi ila ni kibishi tu maisha yanaenda
Faida zake ni kupunguza gharama kwa aliyebebwa,maana anakuwa amekosa room hivyo badala ya kwenda kupanga chumba (ambapo obviously ni expensive kwa maisha ya mwanafunzi anayetegemea boom pekee) anakuwa analipa ile fee ya room nusu na mbebaji nusu
Pia inaongeza ushirikiano,mshikamano na undugu mpya.Mara nyingi mtu mkibebana anakuwa kama kaka yako mdogo wako hivyo unapanua wigo wa marafiki na ndugu
Hasara zake ni kuishi kwa kujibana,kitanda kimoja watu wawili,chumba kimoja,watu wanane badala ya wanne,hivyo kuna hatari ya kuambukizana magonjwa hasa kwa njia ya hewa
Ni kinyume cha sheria za vyuo vingi
Wengine watakuja kuongezea ,but kwangu mimi faida za kubebana zinazidi hasara zake