Kubenea na siasa za Kyela

Status
Not open for further replies.

- Hoja nzito sana hiyo yaani wana-Kyela kuwa na Radio yao, regardless ni ya nani au siyo, lakini hiyo ni plus hapo tupo pamoja sana!

Respect.


FMEs!
 

1Tupo wote Fmes.Tunashukuru kwa ushauri.
2.Wache watumie kalamu zao kutuchafua na sisi tutawachafua humu.Hili ndilo Bunge letu na sisi.

3.Hatuna sehemu nyingine ya kwenda kukabiliana na uonevu huu wa media za Tanzania zilizojaa rushwa,interest binafsi na ujinga.

4.Inashangaza mtu anakuwa wa kwanza kuandika mabaya ya ufisadi na huyohuyo anapokea pesa kutoka kwa wana siasa ili awasafishe.

5.Wana kyela wangekuwa wajinga nafikiri tusingefika hapa tulipofikia.Gazeti la Nipashe na Majira yaliandika ujinga mwingi sana kuhusu kyela.Mpaka unajiuliza kuwa huyu Mhariri wa Nipashe na majira,kweli wamesomea hizo fani zao? au wamechukuliwa tu ili waje kupika majungu?.

6.Fmes, usiombe yaje kukuta haya ya magazeti ya bongo.Wengine yalitupata na wakati sio hata wana siasa na hapo hapo nilimchukia mengi na media zake.Ndiyo ukawa mwanzo wa kuamini kuwa kumbe mengi ni mnyanyasaji sana wa watanzania na tofauti na watazania wengi wanavyoamini.

7.Mengi na media zake hana ata chembe ya Ubinadamu.Kwa watu ambao wanamsoma kwenye magazati yake na kumuona kwenye Tv wanaweza kuamini kuwa huyu mtu ni mzalendo wa kweli.
 
.

Mkuu Sam.
1.Yule mjinga anayejiita Mwafrika or Solomon David or Mzee Mwanakijiji amesema hii ya Mwakalinga ni Low level na hivyo Kubenea hawezi kuja kuijibu.

.......

No,

Yule mjinga anayejiita mwafrika or Solomon David or Mzee Mwanakijiji amesema kuwa hii ya Mwakalinga ni high level (kwa elimu ya poland na pesa za kifisadi za Rostam Azizi) kwa kubenea kujibu
 

Wewe Mwakalinga lini umewalaumu wahindi (wa kiume) kama Rostam wakati ndio wanafadhili kampeni yako?
 

Pyuuu,

Mwakalinga nawe umezidi kulialika kaa kitoto kichanga. Siku ukipata ubunge (wa poland) utakuwa unakesha kwenye vyombo vya habari kulia lia jinsi unavyoonewa.
 

Habari zinazoingia hapa ni kuwa Rostam anachumbia kwenu

Tuseme unasema kweli. Niliandika Mwakyembe wewe unasema Mwakalinga. Na tukiandika Mwakalinga tunamaanisha Mwakyembe? Kama ni hivyo mechi imeisha. Aliyepokea milioni 400 kummaliza Mwakalinga ni Mwakyembe. Na ni Mwakyembe aliahidi watu LAPUTOPU.

Na pia kuwa Mwakalinga ni wa Sikonge wakati Sikonge ni wa Kyela


Natumaini moja ya vipindi vya kwanza kwenye Kyela FM vitahusu wizi wa vifaa vya kompyuta (hivi ile kesi yenu imeisha?)
 
Habari zinazoingia hapa ni kuwa Rostam anachumbia kwenu.

Na pia kuwa Mwakalinga ni wa Sikonge wakati Sikonge ni wa Kyela

Natumaini moja ya vipindi vya kwanza kwenye Kyela FM vitahusu wizi wa vifaa vya kompyuta (hivi ile kesi yenu imeisha?)


Mkuu, kama unafikiri kuwa na Computer basi ndiyo kuwa na Radio, Njoo nikupe hii LAPUTOPU ninayotumia au hata hiyo unaandikia kama hauko Internet Cafe. Nenda fungua radio yako mkuu kama mambo ni rahisi hivyo. Mlikuwa wapi msifungue? Tangu mwaka 2005 mpo Kyela na computer zenu mlishindwa nini? Walau mumpe HONGERA homeboy wenu kwa juhudi ya kubwa ya kufanikisha hiyo Kyela FM.

Mwisho lazima tuwape Wakyela hongera nyingi kwa kufanikiwa kuwa na Radio yao. Mtu akisema ni Radio ya Mwakalinga basi huyo akapimwe Mirembe (kama wewe vile). Ili kufanikisha, watu wengi sana wameshiriki. Mwakyembe angelikuwa mtu wa ushirikiano, basi na yeye angelisaidia sana kuwepo hii Radio na hadi leo msaada wake bado wasubiriwa.

Solomon David, ile radio hadi leo inahitaji misaada ya aina nyingi sana. Kama wewe na kundi lako kweli mwatoka Kyela, basi wasilianeni na Mwakalinga na mmalizie kazi kidogo iliyobaki ili Radio iwe inafanya kazi siku nzima. Kila msaada unahitajika. Msiwe Roho Korosho kwa sababu tu Mwanzilishi wa wazo alikuwa Mwakalinga, na yeye kwa sasa kashajitoa. Mwisho wa siku watafaidi Wakyela wote na kwa sababu ina nguvu, watafaidika hadi nje ya Kyela.

Wito wangu ni kwa Wakyela wote: FMes, Mwakipesile, Masanilo, Nsensi, Mwafrika, Jile, Shalom, Engineer, Bambubile, Mkulima, Malafyale, Mwanjala, Mwakyembe, Mwanakijiji (kama kweli anatoka Kyela), Mwakalinga, Lugombo, Ogah (shemeji yenu), na wengine wote niliowasahau. Kila msaada unahitajika kuanzia vifaa hadi kuandaa vipindi. Wote mwakaribishwa katika kufanikisha hii kazi. Kumbukeni mwisho wa siku anayetakiwa kuwa MSHINDI ni mwanamchi wa KYELA. Atakayesema vingine basi ni FISADI na hatakiwi kuwa KIONGOZI wa Wakyela.
 

Kaka Sikonge,

nakubaliana na mengi uliyoandika hapo juu. Hivi unatoka kijiji gani Kyela? Naona unatuchanganya mara kyela mara sikonge. Mimi mtu wa itete karibu kwa mzee Mwanjala. Kwenye hii thread sitatumia jina langu la kawaida maana nisije nikazua ugomvi.
 
Ya Kyela mengine hayo!

MKUU WA MKOA ARIDHIA MADIWANI KUMVUA MADARAKA MWENYEKITI HALMASHAURI
 
habari nyingi za kubenea siku hizi zimejaa majungu na uongo sana, what happened to his journalistic expertise?
sifa inalewesha kuliko divai na vilevile umesahau ya judas wa iskarioti???
 

Lugambo,
Mie Kyela sijawahi hata kufika. Nilishaishi zamani saana Mbeya mjini wakati Sister akiwa mwalimu shule ya Roleza. Ninachokumbuka hadi leo ni kupanda gari ya mwalimu gani sijui na tuaenda kuangalia Maporomoko ya maji. Hata leo sifahamu ilikuwa wapi.

Kunako majaliwa, mwakani 2010 nitakuwa huko kwa mara ya kwanza. Nimekuwa nikisikia hivyo vijiji na vitongoji vya Kyela na ningelitamani sana kuviona. Pia ningelitamani kuwaona LIVE mtu kama Mwakyembe na Mwakipesile. Huyu Mwakipesile nasikia ni Mbabe si kawaida.

Mwakalinga Family nimeanza kuwafahamu tangu mwaka 1988 nilipokuwa Arusha. Tulienda Tengeru kwenye mashindano ya Kwaya za kanisa la Lutheran Church na hapo nilikutana na ndugu yao wa kwanza. Kutoka hapo nilianza kukutana nao mmoja baada ya mwingine.
 
Na kwa kuwaumiza roho, kitu ni cha JAMII ya Wanakyela na si cha mtu binafsi. Hata Mwakyembe anaweza kuja kutumia.


, Kyela FM iko hewani...... HONGERA wana KYELA kwa kufanikiwa kuwa na mtambo wenu.


Mkuu naomba unisaidie kujua jambo moja dogo tu, hivi mgawanyo wa hisa (shares) ukoje katika hiyo kyela fm,

au kwa maneno mengine nauliza kwamba umiliki wa kyela fm ukoje? nani anaimiliki na ana hisa kiasi gani?

ni hayo tu mzee wa saikong!!
 

Unalialia nini sasa?
 
.....
Natumaini moja ya vipindi vya kwanza kwenye Kyela FM vitahusu wizi wa vifaa vya kompyuta (hivi ile kesi yenu imeisha?)

Dayyyymmm,

Sasa mwizi wa kompyuta hapa ni nani - Sikonge/Muheza au Samwel/Magoli/Mkulima/Mkama/Msauzi/Bambumbile/Lugombo/Mtanzania/Mwakalinga?
 
Kuna mgombea mwingine yuko Kyela sasa akijiuza kwa wananchi huko vijijini. Jina lake ni Elius Mwakalinga wa wizara ya miundo mbinu, Dar Es Salaam. Vijana kama kawaida yao wanapata posho yao na mwaka mpya utakuwa wa furaha.

Hawa Mwakalinga mbona wengi sana? Mwaka 2005 waligombea Mwakalinga wawili ambao hawakuwa ndugu na pia sio ndugu na hawa Mwakalinga wanaogombea sasa.

Elius Mwakalinga ndiye kamanda wa vijana wa wilaya ya Kyela na hana undugu na George Mwakalinga.

Elius Mwakalinga anakuwa mtu wa tano kuonyesha nia ya kugombea Kyela.
 
Mkuu naomba unisaidie kujua jambo moja dogo tu, hivi mgawanyo wa hisa (shares) ukoje katika hiyo kyela fm,

au kwa maneno mengine nauliza kwamba umiliki wa kyela fm ukoje? nani anaimiliki na ana hisa kiasi gani?

ni hayo tu mzee wa saikong!!

Project title: KYELA FM RADIO

KBC-(Hii ni ya Mwakalingas).

Applying Institution: KBC COMMUNITY INITIATIVE SERVICES (KCIS).
(hii inahusisha KBC na Local community of Kyela and Kyela district council).


Kama ilivyo malengo makubwa ya George Mwakalinga ni kusaidia Wana Kyela. Sasa moja ya ndoto zake ilikuwa hii Radio. Hadi sasa hivi wana Kyela wameshaanza kufaidika na wameifurahia sana. Kuanza kusema SHARE kwa sasa ni kama ndoto kwani hii RADIO inakula hela kama SPONJI inavyokunywa maji na hadi sasa hivi, wahusika wote wanafanya kazi kwa KUJITOLEA na bado kuna vifaa vinahitajika. Ndiyo maana nimesema WANAKYELA wote waungane na WAIMALIZIE hii RADIO ili iweze kufanya kazi kwa siku nzima kama siyo 24/7. Itabidi kwanza kuifikisha sehemu hii RADIO iwe inajitegema walau ilipe mishahara na mwisho ndiyo walau kuanza kufikiria FAIDA zigawanywe vipi na hapo ndiyo mtu uanze KUULIZA SHARE. Wanakyela kazi kwenu. Hadi sasa hivi ni WATU wengi wameshasaidia kuwepo kwa Radio ingawa KBC ndiyo inabeba MSALABA mkubwa sana katika kuifanikisha hii RADIO.

Tungelikuwa na hizo milioni 400 alizotowa Lowassa, tungeliifanya kwa haraka sana kwani gharama zake zote hadi na kuwa na pesa ya mishahara ya wafanyakazi kwa miaka 2, sidhani kama inafika hata nusu ya hizo milioni 400.
 

Mkuu Ahsante kwa ufafanuzi wako, lakini bado nina kaswali kengine ka nyongeza.

kwani kama biashara(nachukulia mfano wa kyela fm) haijaanza kutoa faida huwa hakuna mgawanyo wa share?

kwakuwa hata katika kujitolea kwao kila mmoja anatoa kadri ya uwezo wake, au hao wadau wa kyela fm wao wanalingana uwezo kwa hiyo hawaoni umuhimu wa kugawana share mapema kabla ya kuanza kupata faida?

huoni kwamba siku wakianza kupata faida na hawakuwa wamejiwekea utaratibu na misingi ya kueleweka tangu mwanzo, inaweza kusababisha kuparaganyika kama sio kuporomoka kwa hiyo kyela fm?

Btw: hivi ule mradi wa umeme wa upepo pale kwa watani zangu singida, uliosababisha rafiki yako mwakyembe na jirani ndugu yako rostam wagombee kijiji cha kisasida mbona kama nakumbuka kwamba kila mtu alikuwa anajua share zake na mradi haujaanza, au uliisanza mi ndo mgeni hapa mjini?

Au mradi wa umeme na radio ni tofauti kama usiku na giza!!?
 

Mwita,

Wamiliki wa hiyo radio ni KCIS ambayo ni NGO na Halmashauri ya wilaya ya Kyela kwaniaba ya wananchi wote na hakuna shares.

Hao hapo juu wanawakilishwa na board ya radio ambayo inafanya kazi kwa kujitolea.

Lengo sio faida na inatakiwa tu iwe na uwezo wa kujiendesha.

Mwakalinga baada ya kuingia kwenye siasa kajitoa kwenye board, hivi nilichoandika hapa sio official na kama unataka zaidi wasiliana na wahusika ambao hata ukiulizia hapo TCRA watakupatia contacts zao au nitumie PM nitakupatia.
 

- Hehehe! Mkuu Sikonge heshima mbele sana, mimi sitokei huko Kyela wala sijawahi kufika huko, lakini nina washikaji wengi sana wa karibu kutoka huko, otherwise bado ninashukuru sana kwa kunihusisha sana na jopo la kuamua nani anafaa kuwa mbunge wa huko I am humbled!

- Nudugu yangu Saeed Kubenea, ninaamini kwamba yupo bize sana, lakini akimaliza shuguli zake lazima tutamuona tu hapa na style yake ya upanga kwa upanga, maana huwa sio kawaida yake kukimbia mashambulizi subira yavuta heri jamani!

Respect.


FMEs!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…