Wewe mbona ulipoambiwa una majina kibao hapa JF ukaruka kama kuku? Toa jina lako sahihi na wana JF watapigwa na shock maana unayoandika kwa jina la mwafrika hayaendani na wewe.
Nilipoambiwa na nani? Yaani wewe mkulima (nadhani jina lako sahihi ni vithieri Azizi bin Rostam) uniambie kuwa nitumie jina langu sahihi? jina sahihi ni lipi? bin Lowasa (bosi wa Mwakalinga) au bin Rostam (la kwako).
JF hailazimishi mtu kujitambulisha kwa majina yake mpaka anapoamua mwenyewe. Hivyo ndivyo walivyofanya watu wengi wakiwemo mwaklinga na Zitto.
Yaani unajichanganya hadi unachekesha. Paragraph ya kwanza unadai kuwa mimi nijitambulishe kwa jina "sahihi" kisha para ya pili unasisitiza cha kawaida (underscore the obvious) kuwa JF hailazimishi kujitaja?
Mwakalinga siasa zimekushinda, kaendeshe redio yako au kaendeleze maboksi ya lucient (wtf) maana angalau huko hautajichanganya kama hivi.
Tena naona Mwakalinga kafanya la maana kwa kulikubali na jina analolitumia siku zote za huko nyuma. Sasa kama kuna unafiki wowote nendeni kautafute na tuleteeni hapa ili tu,lime huyo Mtanzania aka Mwakalinga.
Mwakalinga bado hajui anachotaka: ubunge, upambe wa rostam, kufanya kazi ulaya, kuanzisha shule ya chekechea kyela, kuendeleza redio, au kuwa mpiga debe wa mafisadi ndani ya ccm.
Hadi hapo atakapofanya uamuzi huu, yeye ataendelea kuwa flip flopper of all times hapa JF.
Kubenea unafikiri mjinga, kaingia mitini kwasababu hana utetezi juu ya hili. Kwa lugha ya vijana amelikoroga, mwache alinywe.
Kubenea anasubiri kuona kama Mwakalinga atabadilisha story. Kila siku anabadili majina, maamuzi, na maandiko. Mtu mwenye akili za kutosha hawezi kujibu hoja za mtu asiye na msimamo kama Mwakalinga.