Kubenea wa MWANAHALISI amenunuliwa na mafisadi?

Kubenea wa MWANAHALISI amenunuliwa na mafisadi?

I believe n i hope kubenea ni mtu makini hawezi fanya hivyo...huwezi kulinganisha kubenea na viongozi wa CCM ambao
mara nyingi huramba matapishi yao
 
Milioni 20? Si angelisema tu Chadema wakamchangia? Na tena Wabunge tu wachache wangelimpa.

Huu ni uwongo wa hali ya juu kuwa mitambo kama hiyo iuzwe kwa bei ya Euro 10,000/-

Mafisadi wana mbinu milioni kidogo ukicheza ngoma yao tu umekwisha. Hii ni moja kati ya mbinu zao za kupoteza watu uelekeo ili wapumue
 
Kauli mbinu ya wapinga ufisadi MITAMBO KWA ROSTAM, MWANAHALISI PALEPALE
 
Kubenea huyuhuyu au mwingine? Nini 20 milioni jamani! kwani pesa anazopata kwa kuuza nakala za gazeti lake si mchezo! Let us wait for next mawanaHALISI!!!
 
mtoa mada anasema kweli kubenea kawekwa mfukoni mafisadi kama mizezi miwili iliyopita na amekuwa akionekana sana na mtoto wa EL (FRED LOWASSA) na kazi kubwa sasa ni kuwapiga mawe kina nape,sitta,mwakyembe na wengine wote ambao wanapiga vita ufisadi ila kuhusu mtambo kwa ufahamu wangu hakuna mtambo wa mil 20 wa kuachapisha gazeti
 
Na Ndimara naye kanunuliwa au Kubenea peke yake? Kama ni Kubenea peke yake bado RA anakazi ngumu, hajakamilisha deal
 
. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda.

Hana lolote huyu, mbona hao watu wote aliowataja tayari wameshajichafua kitaifa au ndani ya chama, hawana hata haja ya kuguswa. Hiyo ni mbinu ya JK kujaribu kutaka rafiki zake wakisema siri zake ambazo tayari kubenea anazo ionekane ni mafisadi. Hakuna lolote. Hata kama maenunuliwa mambo ya KJ na kale ka- toy kake lazima tuyape kama alivyomfanyia mwenzake CHINGA, alivyomchafua ili yeye umaarufu uongezeke si aliona raha,sasa ngoja aipate chungu yake
 
Kijembe ambacho mmoja wa mapacha watatu wa ufisadi, Rostam Aziz Abdulrasul, alikirusha kwa Saed Kubenea kuwa anaweza kumnunulia mtambo wa kuchapishia gazeti lake la MwanaHalisi mapema mwaka huu, kimegeuka kuwa "azma iliyotimia" baada ya mwandishi huyo machachari aliyejizolea sifa kemkem kwa ujasiri kutiwa mfukoni na sasa ni sehemu ya majeshi ya Rostam ya kumlinda na kuwasambaratisha wabaya wake!

Kubenea ambaye mwaka juzi alishambuliwa na watu "wasiojulikana" na kumwagiwa tindikali machoni karibu apofuke, kasahau yote hayo na sasa ni silaha ya kuaminika ya Rostam katika kujihami dhidi ya kampeni kali ya CCM inayoongozwa na Katibu Mwenezi Taifa Nape Nnauye ili mkuu wake mpya Rostam abakie na gamba lake.

Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia Kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na Kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za Rostam na Lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. milioni 20.

Gazeti la MwanaHalisi ambalo limekuwa kwa muda mrefu msumari wa moto kwa mapacha watatu wa ufisadi kutokana na Kubenea kuamini kwamba wawili kati ya mapacha hao watatu walihusika na mpango wa kumtoa roho au kumpa kilema cha maisha, halitabeba taarifa tena za Lowassa wala Rostam ila za wabaya wao hao.

Mathalan, toleo la kesho kutwa la MwanaHalisi tayari lina taarifa ndefu ya Daniel Porokwa akiwamwagia sumu "maadui" wa RA na EL bila kujali kuwa gazeti lake lilimwandika Porokwa mwaka jana kuwa kibaraka wa Lowassa baada ya kujitoa kugombea Ubunge jimbo la Monduli. Porokwa "alizawadiwa" kazi ya Katibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya, gari mpya aina ya NOAH, shilingi milioni 2, na ng'ombe kadhaa baada ya kujisalimisha na kukubali Lowassa amkanyage kichwani kwa mila eti ya Kimasai kama siyo ya kishirikina.


Whats a shame@! Kubenea anahongeka kwa mil 20 tu!
 
Homeboy

Jamaa anauza story hakuna kitu kama hicho! Ni vita wanapigana Magamba hao wanajaribu kumtumia Kubenea kama AK47. Kubenea is not that much cheap. Wanajua Magazeti yao ya Uhuru, Mzalendo, Habari leo hayauziki.
Mkuu sio kuuzika tuu,hata bure bado watu wengi hawayasomi. Jamaa mmoja aliniambia alisahau gazeti lake la HabariLeo Posta na baada ya masaa matatu aliporudi alilikuta palepale ila limewekewa kajiwe ili lisipeperuke,nilicheka sana
 
Nimejaribu kufanya utafiti pori. Mbele yangu nina faili zima la magazeti ya MwanaHALISI. Toleo la mwisho ambalo gazeti hili liliandika habari ya kumbamiza Lowassa ni tarehe 6 Aprili kwa kichwa cha habari: "Lowassa hasafishiki."

Baada ya hapo, matoleo yote 6 yaliyofuata ya MwanaHALISI yamekuwa na habari za kuwatetea kiaina kina RACHEL (Rostam Aziz, CHEnge na Lowassa), kumwandama Kikwete na kujaribu kumgombanisha Kikwete na Sekretariati ya CCM.

Angalia kama ifuatavyo matoleo haya mfululizo ya MwanaHALISI:

1.Kikwete 'jino kwa jino' na Lowassa (13 Aprili)

Habari hii ilipotoshwa makusudi kujaribu kuonesha kuwa uamuzi wa NEC wa kuwafuta kazi mafisadi ndani ya CCM ni vita kali vya madaraka kati ya Kikwete na Lowassa na si uamuzi rasmi wa CCM kama chama.

2. Dk. Slaa amweka pabaya Kikwete (20 Aprili 2011)

Habari hii iliyokuja immediately baada ya kikao cha NEC ya CCM imesema kuwa Slaa amtaja tena Kikwete katika ufisadi. Ikaongeza kuwa avuruga mkakati wa "gamba." Habari nyingine kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti hilo ikasema kuwa: Lowassa, Rostam, Chenge bado

3. Mukama amdanganya Kikwete(27 Aprili 2011)

Habari hii ikitaka kuonesha kuwa Sekretariati ya CCM mpya iliyochukua nafasi baada ya kufukuzwa kwa mafisadi haifai.

4. Kikwete mahakamani (4 Mei 2011)

Huku habari nyingine ikisema CCM yafyata kwa mafisadi

5. Nyumba ya Kikwete yazua utata (11 Mei 2011)

Gazeti hili likiwa linaendelea kumwandama Kikwete kwa tuhuma huku likikaa kimya kuhusu kina RACHEL.

6. Kikwete ndani ya CCJ (18 Mei 2011)

Huu ni muendelezo ule ule wa mkakati wa kina RACHEL wa kuibua tuhuma dhidi ya Kikwete kupitia MwanaHALISI ili wao waweze kusalimika.

Naomba kuwasilisha...
 
Ntachangia kesho baada ya kulitathmini mwanahalisi kwa kina..
 
Nimejaribu kufanya utafiti pori. Mbele yangu nina faili zima la magazeti ya MwanaHALISI. Toleo la mwisho ambalo gazeti hili liliandika habari ya kumbamiza Lowassa ni tarehe 6 Aprili kwa kichwa cha habari: "Lowassa hasafishiki."

Baada ya hapo, matoleo yote 6 yaliyofuata ya MwanaHALISI yamekuwa na habari za kuwatetea kiaina kina RACHEL (Rostam Aziz, CHEnge na Lowassa), kumwandama Kikwete na kujaribu kumgombanisha Kikwete na Sekretariati ya CCM.

Angalia kama ifuatavyo matoleo haya mfululizo ya MwanaHALISI:

1.Kikwete 'jino kwa jino' na Lowassa (13 Aprili)

Habari hii ilipotoshwa makusudi kujaribu kuonesha kuwa uamuzi wa NEC wa kuwafuta kazi mafisadi ndani ya CCM ni vita kali vya madaraka kati ya Kikwete na Lowassa na si uamuzi rasmi wa CCM kama chama.

2. Dk. Slaa amweka pabaya Kikwete (20 Aprili 2011)

Habari hii iliyokuja immediately baada ya kikao cha NEC ya CCM imesema kuwa Slaa amtaja tena Kikwete katika ufisadi. Ikaongeza kuwa avuruga mkakati wa "gamba." Habari nyingine kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti hilo ikasema kuwa: Lowassa, Rostam, Chenge bado

3. Mukama amdanganya Kikwete(27 Aprili 2011)

Habari hii ikitaka kuonesha kuwa Sekretariati ya CCM mpya iliyochukua nafasi baada ya kufukuzwa kwa mafisadi haifai.

4. Kikwete mahakamani (4 Mei 2011)

Huku habari nyingine ikisema CCM yafyata kwa mafisadi

5. Nyumba ya Kikwete yazua utata (11 Mei 2011)

Gazeti hili likiwa linaendelea kumwandama Kikwete kwa tuhuma huku likikaa kimya kuhusu kina RACHEL.

6. Kikwete ndani ya CCJ (18 Mei 2011)

Huu ni muendelezo ule ule wa mkakati wa kina RACHEL wa kuibua tuhuma dhidi ya Kikwete kupitia MwanaHALISI ili wao waweze kusalimika.

Naomba kuwasilisha...

Ukiangakia kweli unaona kuna trend/pattern hapa inajaribu kujengwa. Wakati habari kubwa tangu kikao cha NEC imekuwa ni Rostam Aziz na Chenge na Lowassa kutakiwa kufukuzwa CCM, MWANAHALISI kwa makusudi wameamua kupoteza mwelekeo na kula sahani moja na KIKWETE tu. Katika zaidi ya mwezi mmoja uliopita, Raia Mwema, KULIKONI na DIRA yamekuwa yakiwabamiza kina RACHEL kwani hiyo ndiyo habari kubwa ya sasa. Kumbe MWANAHALISI inaonekana wamepewa kazi maalumu na kina RACHEL.

Kwa mwenendo huu, nabashiri headlines za story za matoleo yajayo ya MWANAHALISI:

1. Kikwete sasa ajuta kumfukuza kazi Makamba

2. Kingunge amtaka Kikwete asifukuze kina RACHEL

3. Kikwete matatani tena

4. Lowassa tishio kwa Kikwete

BURIANI MWANAHALISI!
 
Hali kama hii, kama ni kweli, imewakumba wengi nchi hii akiwemo Rais wetu wa sasa. Kuendesha gazeti kwa kutegemea mapato ya barabarani tu bila matangazo ya biashara ni shughuli pevu. Tulio wengi hatuwaungi mkono kwa hali na mali wenzetu wanaoonyesha uchungu wa kweli wa Taifa letu na rasilimali zake. Kubenea atakuwa amefuata nyayo za Salva Rweyemamu kweli?
 
Kama ni kweli basi money can buy anything except peoples' power!!! Lakini nina wasiwasi mkubwa na mtoa mada hivi ni mtambo wa aina gani unaouzwa mil.20 labda tupe ufafanuzi kidogo!!

Mwanga tu huyo hakuna mtambo wa mil 20 vinginevyo kila mtu angeumiliki labda amnunulie photocopy machine
 
pole mtoa mada nenda manzese kawadanganye mateja pale ndo watakuelewa
 
kijembe ambacho mmoja wa mapacha watatu wa ufisadi, rostam aziz abdulrasul, alikirusha kwa saed kubenea kuwa anaweza kumnunulia mtambo wa kuchapishia gazeti lake la mwanahalisi mapema mwaka huu, kimegeuka kuwa "azma iliyotimia" baada ya mwandishi huyo machachari aliyejizolea sifa kemkem kwa ujasiri kutiwa mfukoni na sasa ni sehemu ya majeshi ya rostam ya kumlinda na kuwasambaratisha wabaya wake!

Kubenea ambaye mwaka juzi alishambuliwa na watu "wasiojulikana" na kumwagiwa tindikali machoni karibu apofuke, kasahau yote hayo na sasa ni silaha ya kuaminika ya rostam katika kujihami dhidi ya kampeni kali ya ccm inayoongozwa na katibu mwenezi taifa nape nnauye ili mkuu wake mpya rostam abakie na gamba lake.

Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za rostam na lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni jk na familia yake, "mtoto wa mkulima", magufuli, chilligati, nape, sitta, anne kilango, ole sendeka, lembeli, mwandosya, membe, kinana, mwakyembe, mkuchika, chatanda na kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. Milioni 20.

Gazeti la mwanahalisi ambalo limekuwa kwa muda mrefu msumari wa moto kwa mapacha watatu wa ufisadi kutokana na kubenea kuamini kwamba wawili kati ya mapacha hao watatu walihusika na mpango wa kumtoa roho au kumpa kilema cha maisha, halitabeba taarifa tena za lowassa wala rostam ila za wabaya wao hao.

Mathalan, toleo la kesho kutwa la mwanahalisi tayari lina taarifa ndefu ya daniel porokwa akiwamwagia sumu "maadui" wa ra na el bila kujali kuwa gazeti lake lilimwandika porokwa mwaka jana kuwa kibaraka wa lowassa baada ya kujitoa kugombea ubunge jimbo la monduli. Porokwa "alizawadiwa" kazi ya katibu msaidizi wa ccm wa wilaya, gari mpya aina ya noah, shilingi milioni 2, na ng'ombe kadhaa baada ya kujisalimisha na kukubali lowassa amkanyage kichwani kwa mila eti ya kimasai kama siyo ya kishirikina.
kiukweli mimi bado hujanipata.......................
 
MAFISADI HAWANA JIPYA WAMEDODA NA WAMEFULIA KISIASA..........................., bado naendelea kuamini kwamba mafisadi hawana jipya na watazidi kuchemsha na kundi lao lote na vijana wao wote wao ndio wanaopanga njama na kumuingiza madarakani kijana wao kutoka visiwani JAMAL KASSIM kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mh Masauni(Mb) naamini hawatafanikiwa hata kidogo....nasema hata kidogo.

-wacha wamnunulia Kubenea hata JUMBO MASHINE PRINTER nini hicho kikoroboi cha milioni 20-30, ila njama wanazozipanga hazitafua dafu hata kidogo wanaplan nyingi kuliko uwezo wao wa kufikiri, wanahela nyingi hawajui wazifanyie nini, wanakundi kubwa lisilo kuwa na tija, hakuna watakalofanikiwa hao. plan wanazotumia kumuingiza JAMAL KASSIM kuwa mwenyekiti UVCCM hazitafua dafu ni bora litibuke tusubiri mwakani 2012 kuliko hizo njama zao, kikao kilichokaliwa na hao vijana wao wa mwmvulia chini ya HUSSEN BASHE BASHE wasidhani havijulikani vinajulikana na wanayoyafanya yanajulikana.

-WANAPINGO KAMA IFUATAVYO: kama LOWASA hawi rais 2015 basi kijana wao EMENUEL NCHIMBI awe rais na LOWASA kuwa WAZIRI MKUU TENA hiyo ndio hesabu yao hata hili wataula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua, leo wamemgeuka mwanamama wao MARY CHATANDA kwa kuwa hakuweza kumsaidia demu wao BATILDA BURIAN kuwa mbunge ARUSHA MJINI sasa imekula kwao waendelee kuvurugana tu na kijana wao JAMES MILLYA mwalimu sijui shule ipi ya sekondari aendelee kutumika utadhani sio mmasai halisi.

-wanamthumu kijana wa watu bure MRISHO GAMBO bila sababu yeyote japo naye mwanzo alikuwa wao lakini hawakumpenda na baadae amejua ukweli sasa wanamuona mbaya, nchii kila aliyekataliwa na BABA W TAIFA MWALIM JULIUS KAMBARAGE NYERERE HAKUNA ATAKACHOFANYA KIKAKUBALIKA MILELE hata kama utamfanyia mtu madhali ni ww unafanya itakula kwako na hao unaowafanyia.

-LOWASA ALISHAKATALIWA NA BABA WA TAIFA watanzania wanajua hilo....................., Mzee kambarage alishawahi toa hundi ya DOLLA LAKI TANO AMBAYO LOWASA ALIHONGWA NA WAHINDI KUKIUZA KIPANDE CHA ARDHI LEO NDIO KUNA SHULE YA AGKHAN MZIZIMA PRIMARY SCHOOL, hii lilikuwa MKUTANO MKUU WA HALMASHAURI KUU 1995 watanzania hawajasahau na hawatasahau hilo. wakati huo alikuwa WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO.

-KUBENEA ATAKULA NAO SAHANI MOJA PAMOJA NA KUNUNULIWA HUO MTAMBO na hao aliotajiwa kuwashughulikiwa haita tokea mbona wanamiliki MAGAZETI YAO YA TAZAMA linatoka kila JUMANNE NA LIMESHINDWA KUFUA DAFU, WANAMILIKI MKAKATI linatoka kila IJUMAA nalo limeshindwa kufua DAFU? NINI WANATAPA TAPA HAWA WATU? WAMEFULA.

-WAMEKULA YA MBUZI WATAOTA MAPEMBE.............................!!!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Kuna mambo mawili makubwa kuhusiana na RACHEL ambayo nimekuwa nikiyafanyia kazi kwa wiki nzima sasa ila bado sijafikia conclusion. Mojawapo ni hili la KUBENEA kununuliwa na RACHEL ili awasadie kuwachapa wapinzani wao wakuu kisiasa, wakiwemo SAMWEL SITTA na HARRISON MWAKYEMBE. Inasemekana kuwa kazi hii inafanywa kwa ufasaha sana na MWANAHALISI, na hata gazeti lao litakalokuwa mitaani kesho linawapiga tena SITTA na MWAKYEMBE, baada ya hoja hii ya kipuuzi ya CCJ kuongezewa nguvu na DANIEL PAROKWA mwishoni mwa wiki. Kwa upande wa PAROKWA ni wazi kuwa ametumwa na RACHEL. Tutathibitisha baadaye alilipwa kiasi gani. Suala la pili ambalo nalifanyia kazi ni taarifa kuwa MPENDAZOE naye amekatiwa kitu kidogo na RACHEL ili zimsadie kwenye kesi yake ya Ubunge. Taarifa hizi zinadai kuwa baada ya MPENDAZOE kumtaja NAPE kama mmoja wa waanzilishi wa CCJ kule MBAMBA-BAY, RACHEL wakamvaa na kumtaka akamilishe kazi kwa kuwataja pia SITTA na MWAKYEMBE. Alifanya hivyo akiwa NJOMBE, baada ya kupokea kitita chake kutoka kwa jamaa mmoja mwenye asili ya Kisomali aliyetumwa huko na RACHEL. Kama nilivyodokeza hapo juu, haya bado nayafanyia uchunguzi wa kina, na nitayaanika rasmi hapa JF nikishakusanya data zote na kujiridhisha.
 
Kuna mambo mawili makubwa kuhusiana na RACHEL ambayo nimekuwa nikiyafanyia kazi kwa wiki nzima sasa ila bado sijafikia conclusion. Mojawapo ni hili la KUBENEA kununuliwa na RACHEL ili awasadie kuwachapa wapinzani wao wakuu kisiasa, wakiwemo SAMWEL SITTA na HARRISON MWAKYEMBE. Inasemekana kuwa kazi hii inafanywa kwa ufasaha sana na MWANAHALISI, na hata gazeti lao litakalokuwa mitaani kesho linawapiga tena SITTA na MWAKYEMBE, baada ya hoja hii ya kipuuzi ya CCJ kuongezewa nguvu na DANIEL PAROKWA mwishoni mwa wiki. Kwa upande wa PAROKWA ni wazi kuwa ametumwa na RACHEL. Tutathibitisha baadaye alilipwa kiasi gani. Suala la pili ambalo nalifanyia kazi ni taarifa kuwa MPENDAZOE naye amekatiwa kitu kidogo na RACHEL ili zimsadie kwenye kesi yake ya Ubunge. Taarifa hizi zinadai kuwa baada ya MPENDAZOE kumtaja NAPE kama mmoja wa waanzilishi wa CCJ kule MBAMBA-BAY, RACHEL wakamvaa na kumtaka akamilishe kazi kwa kuwataja pia SITTA na MWAKYEMBE. Alifanya hivyo akiwa NJOMBE, baada ya kupokea kitita chake kutoka kwa jamaa mmoja mwenye asili ya Kisomali aliyetumwa huko na RACHEL. Kama nilivyodokeza hapo juu, haya bado nayafanyia uchunguzi wa kina, na nitayaanika rasmi hapa JF nikishakusanya data zote na kujiridhisha.

Mkuu mimi nijuavyo Mbunge wa sasa ambaye anapambana na Mpenda mahakamani ni miongoni mwa makamanda mahiri sana na asiyeteteraka ambao RACHEL inawategemea sasa tena wamsaidie Mpenda ili wamuangushe kamanda wao? Sijui lakini nina shaka.
 
Back
Top Bottom