Kuchagua viongozi wasio na elimu ndicho chanzo cha umasikini Tanzania

Kuchagua viongozi wasio na elimu ndicho chanzo cha umasikini Tanzania

HIMARS

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
70,791
Reaction score
98,334
  • Wabunge
  • Madiwani
  • Wenyeviti serikali za mitaa
Hawa ndio watu ambao wanasababisha nchi yetu iende hovyo hovyo.

Wabunge ambao hawajasoma hawana tija wala msaada kwa taifa na sababu ni kuwa hawaelewi miswada inayopelekwa bungeni, hivyo wao hukubaliana na kila kitu wanachoambiwa.

Madiwani kwenye Halmshauri wapo ambao hawawezi andika karatasi nzima lakini hao ndo wasimamizi wa mapato ya halmshauri zetu, je tutegemee nini?

Wenyeviti wa Serikali za Mitaa hawa ndio wasimamizi wakuu wa Sera za Kielimi, Ardhi etc, makazi horera yamesababishwa na hawa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, wao na Ofisi zao kwa Makusudi wamekuwa wakikubali mtu ajenge bila kupeleka Ramani na kuona kama yaenda au haiendani.

Hata kwenye Ripoti ya CAG imeonesha kuna wafanyakazi 740 ambao wapo kwenye vyeo wasivyo sitahili kuwepo.

Ukiangalia bungeni, wabunge wengi mule kazi yao ni kusifu na kuabudu badala ya kuongea mambo ya msingi kwa jamii.

NB: Tusipojirekebisha hakika Nchi yetu itapotea.
 
Hao ndio wanaofaa ktk siasa na uongozi. Nakupenda [emoji1241]
 
Unataka kujua tatizo linakoanzia? Zunguka shule zote Tanzania, Bara & Visiwani, za dini, asasi binafsi na za serikali, waulize wale the best students (at least best 20 ama 50), iwapo hata mmojawapo angependa kuwa mwanasiasa baadaye.

Majibu yao yatakushangaza kama siyo kukustaajabisha.
 
Back
Top Bottom