Ni vigumu sana kusema harusi zisichangiwe, hii inatokana na tabia ambayo tumejiwekea ya kutaka kufanya sherehe kubwa kubwa za harusi ambazo ni vigumu sana kwa mtu mmoja kuweza kufanya hivyo, ndio maana utamkuta mtu anatembeza bakuli la mchango (card za mchango) ili aweze kukamilisha malengo yake aliyo ta weka.....
Hivi juzi tu jamaa yangu wakaribu ali funga ndoa na harusi yake ili gharimu takribani tsh million 17, na kulikuwa hakuna pombe, kilicho ni shangaza kwenye harusi hii haikufana sana japo ili gharimu pesa nyingi sana, nimesema hivyo kwa kuwa kuna rafiki yangu alifanya harusi ya tsh million 4 tu huwezi hamini ilifana sana na watu walikuwa wengi kushinda hiyo iliyo gharimu million 17.
Nilicho jifunza hapa ni kwamba harusi unaweza kujipanga mwenyewe kwa kuigharamikia , kwa mfano hiyo ya million 4 ni pesa ndogo sana ambayo mtu unaweza kujipanga kwa mwaka mmoja na kipata na kufunga ndoa pasipo kuwasumbua watu.
Tatizo kubwa lipo kwetu wenyewe kwamba tuna taka vitu vya gharama kubwa na ambavyo hatuwezi kivi fanya wenyewe pasipo kutegemea michango ya watu.
Umefika mda sasa watanzania tu funguke macho na kufanya mambo ya maendeleo na kuachana na hizi hanasa na masaa 4/6 ambazo mwishoe ndoa ina vunjika ndani ya wiki moja huku ukiwaacha ndugu zako kwa kilala njaa kutokana na harusi yako.
Kwa wenzetu ulaya kwa jinsi nilivyoona huwa wanafanya harusi ya kawaida sana na ambayo hai gharimu pesa nyingi sana na muoaji na muolewaji ndio huwa wana gharamia kwa 90% gharama ya harusi yao,ambapo ni tofauti na huku bongo ambako utakuwa bwana harusi mara nyingine anachangiwa hadi kununua gauni la bibi harusi.