KUCHELEWA KWA MALIPO YA WANANCHI WA KATA YA NYATWALI WILAYANI BUNDA

KUCHELEWA KWA MALIPO YA WANANCHI WA KATA YA NYATWALI WILAYANI BUNDA

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Wananchi wa Kata ya Nyatwali waliamuriwa na Serikali kupisha eneo hilo ili pawe mapito ya wanyama pori mpaka Ziwa Victoria na wanyama waweze kuchunga na kunywa maji kwa urahisi. Wananchi walifanyiwa tathmini ya maeneo yao, mali zao na sasa imekwishapita mwaka moja na nusu tangu kufanyika kwa tathmini hiyo. Kama ilivyo sheria ya ardhi ni kuwa tathmini ikifanyika na ikapita miezi sita bila malipo basi waathirika wanatakiwa wafanyiwe tathmnini upya au walipwe nyongeza ya 7%. Hivyo wananchi wa Nyatwali wanastahili nyongeza ya asilimia 7% pindi watakapolipwa vinginevyo suala hili litapelekwa mbele ya sheria ili wananchi hawa wapate haki yao kama sheria ya ardhi inavyotamka.
 
Sizani kama kuna Malipo hapo kila siku wanapigwa hadithi,mara malipo yapo mbioni ,mara hela ipo tiyari Tanapa,Uongo mtupu na hiyo 7% ni haki yao lkn haitatolewa na hii Serekali ya CCM
 
nyatwali ni strategical area katika ecosystem ya serengeti, hawa wananchi walipwe haraka
 
Back
Top Bottom