Kuchoma choma ndani ya uke

KIDOLEGUMBA

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2013
Posts
498
Reaction score
110
Habari wadau, jana jioni mpenzi wangu ameniambia anajisikia kuchomwa chomwa ndani ya uke (kichomi), nikaona nije nijaribu kupata huduma ya kwanza kutoka kwa wadau wa afya kabla hatujachukua hatua za ziada za kwenda hospital, je anaweza akawa anasumbuliwa na ugonjwa gani wenye hizo dalili?
 
Vichomi hivi huwapata baadhi ya akina dada/mama. Pia lazima kujua aina ya kichomi hicho na kukadumu kwa muda gani.
Kuna kinachikuwa kama kisu kimechomwa na kinadumu for few seconds or minutes, sababu ni tofauti.

Kuna vingine ni matokeo ya michezo yenu, unamchubua mwenzio.

Kuna vingine ni akiwa karibu na kujimwezisha anapata aina fulani ya vichomi.

Lakini pia watakiwa kujua, je ni mjamzito?

Ana infection ya aina yeyote?

Kikubwa kamwoneni gyno.
 
Wazee wa kizamani husema ni 'chango', so wanakuwa na dawa zao wanampa hasa anapokuwa mjamzito. Wanaamini kichomi hicho chaweza kusababisha mimba kuharibika.

Wengine nao husema ni 'syndrome'
 

Nashukuru kwa maelezo, hana ujauzito kwa sasa, pia swala la infenctions tutaenda kucheki ,maana alikua anasumbuliwa na candidiasis kipindi cha nyuma, michubuko pia inawezekana ikawa inachangia. Nitaenda nae kituo cha afya kuchek zaidi.
 

hapo umeniuwa saana
 
Dah! mi nilidhani wachomwachomwa ww... nilitaka nikwambie uje unione
 
huyo fanya umpeleke hospital.huyo ni kwamba kizazi kimeshuka kipo chini.kwa huduma ya kwanza mwambie achemshe maji ya moto halafu aweke kwenye ndoo au kisado.halafu achukue mafuta ya nazi achanganye na maji hayo then akalie hayo maji kwa muda wa dk 5 ili mvuke uweze kuingia ukeni.afanye km mara tatu natumai itakwisha
 

Hii taaluma ni ya asili au hutoka kwa wanasayansi wa hospitalini?
 

mkuu kwan n michezo yetu tu?

We hauchez hizo serakas?
 

We ni doctor wa kichakani. Kizazi kinashuka chini ardhini au wapi.
 
Ni hali ya kawaida pindi msichana anapoelekea kwenye siku zake hiyo ni moja ya dalili, labda kama kinakaa sanaa ila kama ni cha kupita basi ni hali ya kawaida.
 
We ni doctor wa kichakani. Kizazi kinashuka chini ardhini au wapi.
huwa vinashuka, sema ni nadra mno, usiombee haya matatizo, kuna magonjwa ya kutisha mno.

Cha muhimu muhusika aende hospitali akajue tatizo. Hatokuwa na tatizo hilo, tatizo lake kwa maelezo yake ni la kawaida.


usiangalie hapa kama una-roho nyepesi.

prolapsed uterus - YouTube
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…