Kudhibiti COVID-19 na kuepuka kulishana uchafu, tuweke sheria ya kupiga faini yeyote atayepiga chafya hadharani bila kuziba pua na mdomo

Wakati nipo secondary mwalimu wangu wa Biology alinifundisha kuwa virusi vyote havina dawa. Ndio maana hata mafua pia ni virus lakini hayana dawa bali yanapotea kwa muda lakini baadae yanarudi.

Sasa sijui ni nani yupo sahihi hapa dada yangu.
 
Umeona sasa?
Nadhani neno sahihi kutumia ni ‘tiba’.

Virusi havina tiba.

Dawa zote zilizopo ni za kukupa nafuu tu.

Mfano haya mafua ya kawaida ambayo kwa kiasi kikubwa husababishwa na rhinovirus.

Dawa zilizopo ni za kukupa nafuu tu. Nafuu ya zile symptoms zake. Lakini hazikutibu hayo mafua.

Huwa yanaisha tu yenyewe baada ya siku kadhaa.

Vivyo hivyo, hata hizi chanjo za corona, kazi yake siyo kutibu corona. Ni kupunguza tu makali yake na kuifanya isikudhuru sana.
 
Vivyo hivyo, hata hizi chanjo za corona, kazi yake siyo kutibu corona. Ni kupunguza tu makali yake na kuifanya isikudhuru sana.
Sawa mkuu. Ina maana Corona inaweza ikarudi yenyewe kwa kutokea ndani ya mwili wa mwanadamu yeye kama yeye pasipo kupata maambukizi kutoka kwa mtu mwingine?
 
Sawa mkuu. Ina maana Corona inaweza ikarudi yenyewe kwa kutokea ndani ya mwili wa mwanadamu yeye kama yeye pasipo kupata maambukizi kutoka kwa mtu mwingine?
Hilo sijui.

Ila nachojua ni kwamba mtu unaweza kuugua corona zaidi ya mara moja.

Na maambukizi si lazima uyapate toka kwa mtu. Unaweza kuyapata toka kwa wanyama wengine, pia!
 
Huyu mleta mada siku hizi anazidi kuchanganyikiwa
 
Wakati nipo secondary mwalimu wangu wa Biology alinifundisha kuwa virusi vyote havina dawa. Ndio maana hata mafua pia ni virus lakini hayana dawa bali yanapotea kwa muda lakini baadae yanarudi.

Sasa sijui ni nani yupo sahihi hapa dada yangu.
Hakika, hakuna dawa ya kuangamiza/kuua virus isipokuwa kuna chanjo ambazo ukidungwa zinazipa kinga mwili mbinu/uwezo wa kupambana na kirusi wa ukweli pale atapoingia mwilini...hizo chanjo huwa na virusi wasio na madhara like a decoy virus

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…