Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...


Kama una ushawishi kwa ccm basi washauri wamsimamishe
Hoja namba tatu ni kama unatania,lets wait and see!
 
Pasco unataka kutuaminisha kuwa tatizo kuu la nchi yetu ni kukosa kiongozi mmoja bora wa kutuongoza, hivyo Lowassa ni mtu bora wa kipekee wakuja kutuongoza vema!!

Umechelewa sana, hakuna namna ambayo unayoweza kuwashawishi wanatanzania wa leo ambao wanaendelea kuelimishwa na CHADEMA kwa kasi ya ajabu warudi nyuma wakakueelewa, labda baadhi ya WanaCCM mazezeta ndio watakuelewa.

Kama unabisha muulize vizuri Lowassa ni kwa nini ndugu zake wameru kule Arumeru mashariki waliamua kuikataa CCM mbele ya macho yake pamoja na kupewa hongo za kila namna?
 
....Edward Ngoyai Lowassa fisadi na mbadhirifu aliyekubuhu ndiye Rais wa Moyoni wa Pasco wa JF, ama kweli maisha ni kuchagua na hatuwezi kulingana, go Pasco go....
 
Kwani asiwe Eliakimu Maswi au Mwakyembe au Ezekiel Maige au mimi Ndahani Pasco. Naogopa suprise mwenzio....
 
Last edited by a moderator:
Huyu Lowassa atatuumizia akili za kaka yetu Pasco.

Lowassa, he will never be a President of this Republic hata akigombea na Jiwe ni uhakika kuwa Jiwe litashinda. Lowassa ni mmoja waliomo kwenye list of Shame, alitajwa na rais wetu Dr Slaa kuwa ni fisadi kama Kikwete alivyo, still no difference mwizi ni mwzi tu hata ukimpa manyoya ya kuku bado ataiba hata mavi ya kuku.

Pasco you real need help ASAP
 
Hakuna kazi ngumu kama kumkampenia EL, Pasco you are on MISSION IMPOSSIBLE

 

Attachments

  • Bounce back by Jacob Zuma.jpg
    21 KB · Views: 2,696
Last edited by a moderator:

Nakufananisha na mwanamke asiye na msimamo, maana namimi wa TLP ukinisikia vizuri siku moja utasema njia yangu ya kwenda Ikulu ni nyeupeee peee!!!!!
 
Pasco, umejitahidi kufanya analysis yenye ushawishi, lakini kuna baadhi ya mambo ambayo naona haukuyatilia maanani (sijui kwa ushabiki au ni oversight tu). Kwanza, kwa ujumla, shida ya tanzania sasa hivi sidhani kama ni mtu mzuri wa kuongoza. tatizo kubwa linbaloikabili Tanzania hivi sasa ni mifumoya kiongozi ambayo haifanyikazi vile inavyotakiwa. Labda suala hili ndilo linalotutias giza na kuanza kuwajadili watu badala ya issues kwa sababu lenyewe linahusiana na personality pia.
Lowassa au mtu mwingine anaweza kuonyesha quality za kiongozi mzuri lakini uongozi ni teamwork ambayo inapaswa kusaidiwa na mdumo mzuri. hapo yanaweza kuibuka matatizo mawili makubwa ambayo yanaweza kumfanya Lowassa ashindwe akishinda. Lwanza atakuwa na tiumu ya watu kutoka CCM ambako tayari kuna madonda makubwa na kpiga vita kwa hatari sana. Pili, huku akiwa na tiumu ambayo inatafunana ndani kwa ndani, atakumbana na mfumo ambao umegota kuanya kazi. Kwa kiasi kikubwa hata Kikwete ameshindwa kutokana na sababu hizimbili kuu.
Kwa hali ilivyohivi sasa CCMinapaswa kufa na kuzaliwa upya, na izaliwe mpya kweli, ikiachana na ya kale yote. Hili ni jambo ambalosidhani kama linaweza kutokea lenyewe na sioni uwezo wa Lowassa kulifanyahili litokee.
Lakini pia kwa kiasi fulani Lowassa ameonyesha dalili za kuendeleza malumbano ya kutafunana kwa sababu ajalikana kuwa nimtu wa visasi.
Mbaya zaidi, wakati wakiendelea kutafunana ndaniya CCM, huko nje Chadema, CUF na ADC nazo zitakuwa zikiendelea kuwatafuna. Unadhani Lowassa anaweza kweli kukabiliana na hali hii hasa ukizingatia wasi wasi wakokuwa afya yake inaweza kuwa na mushkeli?
 
Last edited by a moderator:

Ila Dr ndo ana ethics za uongozi kwa kutembea na mke wa mtu na kula michango ya kanisa.
 

Ndio maana najiuliza kwanini awe yeye na siye mwingine yoyote? Maana CCM ina makundi mengi yenye nia ya kumtoa mgombea urais na sasa yanajipanga kuwa na ushawishi mkubwa kwa wapiga kura. Miaka mitatu si michache maana hata saa moja ni kubwa sana ndani ya mambo ya kisiasa.
 
Naamini hata kule Arumeru mashariki wengi walisema kama sio mkwewe Lowasa (Siyoi Sumari) basi ccm ingelipoteza Jimbo.

Kumbukumbu zangu kama dhaifu vile, kuwa huo wosia uliotolewa kwa ccm kumsimamisha mkwewe Lowasa haukuzingatiwa vile!

Ama kweli utamu upo wa aina nyingi, kwani hata pilipili ina utamu wake! Hongera Pasco kwa kukolewa na utamu!
 
Pasco na analysis zake nyepesi na zenye ufinyu wa kimtazamo hajambo. Umefungwa na nini kiasi kwamba you dont think of any other person except EL? amekupa nini? hebu jaribu kufikiria kama tunavyokufahamu. Achana na EL, sio mtaji mzuri. Utaukosa hata ukuu wa wilaya ukiendelea na tabia hii.
 
Pasco wa JF........Lowassa for president 2015.
Rais 2015 lazima atoke kaskazini.

:spy::spy::spy:

Mimi sikatai obsession ya Pasco kwa Lowassa, kila mtu anayo obsession yake at one point, it is natural. However, it become unnatural and a bit weird kama Mtu huyo anaelezewa kama man alone from a failed system. System ambayo haijaweza kufanya yale yaliyotarajiwa na wengi.

A system where, individuals ndani ya systems are biting each other, sabotaging each other, making deals with devils in and out of that same system.

An individual who was accused of getting across Procurement procedures, altering the process and causing a massive economical shake to the country, accepted the accusation as major and resigned - of-course while :A S cry:, who wouldn't.
Hata waziri wa uchukuzi wa Znz ali-resign juzi huku akinung'unika.

Ukikubali ku-resign, maana yake umekubali kosa. Issue ya kuthibitishwa mahakamani ni swala jingine kabisa. nani asiyejua kwamba kupelekwa mahakamani hapa Tz ni mapaka mkulu aamue?? Hata majizi yanaambiwa yarudishe fedha yazizokwiba.

Mkuu, huyu jamaa hasafishiki.....he has been around for a long long time.....amefanya nini?? usiongelee shule za kata kwasababu that is a disgrace to education system in Tanzania...what else?
 
Last edited by a moderator:
binafsi nimeona kma EL afya yake mgogoro kidogo, alikua anaongea kwa shda shda af design memory yke imekaa kushoto kdg........

reference nyingi za mambo aliyokua akijaribu kupambanua alikua hakumbuki...........

Kwa hiyo Pasco hakuiona hayo!!
 
Kwanza, Edward Lowassa si Waziri Mkuu mstaafu. Ni Waziri Mkuu wa zamani aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa Richmond. Mawaziri wakuu wastaafu walio hai ni kina Cleopa David Msuya, Salim Ahmed Salim, John Malecela, Joseph Warioba na Frederick Sumaye. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuwa "mstaafu" na yule "aliyejiuzulu" tena kwa kashfa ya ufisadi. Hivyo bora mumuite waziri mkuu wa zamani na si waziri mkuu mstaafu, kwani Lowassa hakuwahi kustaafu bali kalazimika kuachia madaraka.Kama walivyosema wenzangu, Watanzania tupo karibu milioni 50, hivi tumefilisika kiasi hiki mpaka tuendelee kung'ang'ania wanasiasa wenye kashfa za ufisadi na utajiri usioelezeka na wenye mashaka kama Lowassa? Jibu ni kuwa la hasha, kuna Watanzania na wanaCCM wengi sana waadilifu na wenye uwezo. Ila Lowassa anajulikana kuwa na uchu wa madaraka na kuwapanga watu humu JF na kwingineko kwa kuwapa pesa ili wampambe na wajaribu ku-brainwash Watanzania wasahau tuhuma za ufisadi na za ukosefu wa uadilifu dhidi ya Lowassa.Ni upumbavu mkubwa kujaribu kumtakasa fisadi. Mungu hapendi hilo na kamwe halitafanikiwa.
 
sasa mkuu Pasco, huyo Lowassa anashauri tu invest kwenye elimu kwanza wakati mali zetu zinaendelea kuibiwa, sasa mpaka tukija kuanza ku invest kwenye elimu na mali zetu zinaendelea kuibiwa hao wasomi watakuja kuitumia vipi elimu yao katika ustawi wa taifa letu, ishu kubwa hapa ni CCM ni adui wa maendeleo ya watanzania tumuondoe....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…