Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...

Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...

Naona PASCO tatizo halisi la NYINYIEM siyo individuals ni tatizo la kimfumo ni tatizo la kitaasisi EL kama EL hata afanyaje hawezi kuubadili... aidha je, unajua alipoenda kwa TB Joshua Nigeria aliambiwa nini? Mtafute umuulize atakwambia.... IN short anajua HE IS NOT THE NEXT PRESIDA wa Tanzania.... na CCM wanajua wakimsimamisha... IMEKULA kwao! Na hawatamsimamisha take it from me! Sasa kinyume chake wakimsimamisha CDM ndio watachukua NCHI kama wananawa!
Mkuu Karikenye, hili bandiko lako limenikosesha kabisa amani!, nijuavyo mimi Mungu alishakisikia kilio cha Watanzania kwa muda mrefu, akamtia maneno ya unabii TB Joshua, kuwa amesikia kilio chetu, na ametupatia mkombozi!, ndipo TB Joshua akamtafuta EL na kumweleza maneno ya unabii ule ila alimwambia ni siri, na asiitoe mpaka utakapotimia huo unabii!.

Kiukweli maneno yako haya IN short anajua HE IS NOT THE NEXT PRESIDA wa Tanzania.... na CCM wanajua wakimsimamisha... IMEKULA kwao! Ni ya kukatisha kabisa tamaa, kwa sababu wengine ndio tunalipwa kupiga debe huku tukiwa tayari tumeisha ahidiwa nafasi tutakazopewa kama asante ya kazi nzuri, mfano mimi ndie napaswa kupewa ile posti ya Salva!, sasa kama unasema CCM haiwezi kumsimamisha EL, unamaanisha nini kwa maajaliwa yetu akina sisi na ahadi tulizo ahidiwa?.

Hata hivyo mimi bado sikuamini, nitapigana kufa na kupona mpaka EL awe ni yeye ili angalau na sisi iwe ni zamu yetu!, kwani nani hapendi kakibanda kama kale ka Mchungaji Mama Getrude Lwakatare?!, Nani hapendi S-Class 500 au Vogue etc?!, 2015 ni zamu yetu na EL ndie mtu wetu!.

Wanjf wenye kuitakia mema nchi hii, tuungane nami kwenye hili, tena matangazo yote ya serikali, pia yatapitia jf na tutalipwa vizuri!.
 
Pasco unatumia sabuni gani na brash gani na maji yenye kemikali hipi kusafisha hii kitu yenye kutu???Naomba jibu this is too late maana CCM wanajua kisasi alichonacho rohoni wamsimamishe apate uraisi awafanye kama Chiluba na Kenneth Kaunda??no way na haitakuja kuwa!!for your info!
Mkuu Kaka Kiiza, kwanza pole tena kwa msiba wa wife, nitakujibu baada ya msiba!.
 
CCM ikimsimamisha mgombea yoyote, atashinda tu kwa kanuni ya sasa ya mshindi ni mshindi. Unless kanuni hii inabadilishwa, vinginevyo CCM 50.1% dhidi ya Chadema 49.9%, mshindi atakuwa CCM. Utabiri wangu ni kwamba ushindi wa Chadema kama utatokea ni uwezekano wa kuunda serikali ya pamoja na CCM kutokana na ukaribu wa kura. Lakini hii itakuwa ngumu sana kiuamuzi kwa Chadema kwani tayari wameonyesha kutokubaliana na utaratibu huu, hasa pale wanapowaona CUF kama CCM 'B' baada ya uchaguzi wa Zanzibar 2010;

The bottom line hapa ni kwamba mgombea yoyote wa CCM akisimamishwa atashinda Urais; kwahiyo mbinde iliyopo kwa wagombea wote watakaojitokeza ni kuvuka kwana lile panga la kamati kuu ambalo kwa nyakati hizi ni arbitrary kwani itapendekeza majina yasiyozidi matano miongoni mwa maelfu yatakayojitokeza kuwania nafasi hiyo; na vigezo vitakavyotumika kubakisha majina yasiyozidi matano havitakuwa sawa na vile wakati wa Nyerere, na badala yake madudu mengi sana yatafanyika humo - fitina, uonevu, majungu n.k;

Mwisho wa siku, kwa yule atakayefanikiwa kuvuka kiunzi hiki cha awali na kuendelea mpaka mkutano mkuu wa taifa kuibuka mshindi ndiye atakayekuwa Rais wa tano wa Tanzania. Kwahiyo tusipoteze muda kujadiliana kwamba fulani ni more likely kushinda akipitishwa, fulani ni less likely kwani yeyote ambae atasimamishwa na CCM miongoni mwa majina haya yanayotajwa tajwa tayari, as long as CCM nzima itakuwa nyuma yake, huyo ndiye atakuwa Rais wa Tano wa JMT.

Iwapo CCM itatafuta mgombea mgeni na mpya kabisa masikioni mwa watu, hilo litakuwa ndio anguko la CCM 2015 kwani hapatakuwa na muda wa kumnadi mgombea mpya. Nyerere mwenyewe alipata shida sana na Mkapa 1995 ambapo aliumbuliwa asilimia in the lowe sixties, na huyo alikuwa mwalimu kazini. Mgombea wa CCM ni muhimu atokane na hawa hawa tunaowasikia sasahivi kwani hiyo ndio salama ya CCM 2015;
 
You really need help Pasco
seriously

Wapo watu waliamini kwa asilimia 100 kuwa Rais aliefaa mwaka 1995 na 2005 alikuwa
Salim A Salim
Watu hao ni pamoja na Mwalimu Nyerere

lakini hawakuwahi kuwa 'this crazy over one person'....

Nahofia coming 2016 na Rais sio huyu unaemtaka
unaweza usi recover mentally kwa kweli......You need help now
Mkuu the Big Boss, ni kweli, matarajio na mategemeo yangu yote, nimeyaweka kwa EL, na ni kweli, asipokuwa nitaishia kucolapse tuu, kwa sababu mpaka nyumba ipi nitahamia na kuuziwa nimesha ichagua na aina ya gari nitakaloendeshwa na baada ya miaka 2 nitauziwa kwa bei ya bure pia nilisha chagua, The only help I need for now ni kunisupport on this right cause ya ukombozi wa pili wa nchi yetu!.
 
CCM ikimsimamisha mgombea yoyote, atashinda tu kwa kanuni ya sasa ya mshindi ni mshindi. Unless kanuni hii inabadilishwa, vinginevyo CCM 50.1% dhidi ya Chadema 49.9%, mshindi atakuwa CCM. Utabiri wangu ni kwamba ushindi wa Chadema kama utatokea ni uwezekano wa kuunda serikali ya pamoja na CCM kutokana na ukaribu wa kura. Lakini hii itakuwa ngumu sana kiuamuzi kwa Chadema kwani tayari wameonyesha kutokubaliana na utaratibu huu, hasa pale wanapowaona CUF kama CCM 'B' baada ya uchaguzi wa Zanzibar 2010; The bottom line hapa ni kwamba mgombea yoyote wa CCM akisimamishwa atashinda Urais; kwahiyo mbinde iliyopo kwa wagombea wote watakaojitokeza ni kuvuka kwana lile panga la kamati kuu ambalo kwa nyakati hizi ni arbitrary kwani itapendekeza majina yasiyozidi matano miongoni mwa maelfu yatakayojitokeza kuwania nafasi hiyo; na vigezo vitakavyotumika kubakisha majina yasiyozidi matano havitakuwa sana na vile wakati wa Nyerere, madala yake madudu mengi sana yatafanyika humo - fitina, uonevu, majungu n.k;

Mwisho wa siku, kwa yule atakayefanikiwa kuvuka kiunzi hiki cha awali na kuendelea mpaka mkutano mkuu wa taifa kuibuak mshindi ndiye atakayekuwa Rais wa tano wa Tanzania. Kwahiyo tusipoteze muda kujadiliana kwamba fulani ni more likely kushinda akipitishwa, fulani ni less likely kwani yeyote ambae atasimamishwa na CCM miongoni mwa majina haya yanayotajwa tajwa tayari, as long as CCM nzima itakuwa nyuma yake, huyo ndiye atakuwa Rais wa Tano wa JMT.

Iwapo CCM itatafuta mgombea mgeni na mpya kabisa masikioni mwa watu, hilo litakuwa ndio anguko la CCM 2015 kwani hapatakuwa na muda wa kumnadi mgombea mpya. Nyerere mwenyewe alipata shida sana na Mkapa 1995 ambapo aliumbuliwa asilimia in the lowe sixties, na huyo alikuwa mwalimu kazini. Mgombea wa CCM ni muhimu atokane na hawa hawa tunaowasikia sasahivi kwani hiyo ndio salama ya CCM 2015;
Mkuu Mchambuzi, huu ni ukweli mchungu, ambao wanabody wengi humu wanapaswa kuuelewa na kuukubali, na kwa upande wangu, nakuaminia sana wewe Mchambuzi kwa uchambuzi wako mahiri, nakuomba sana endelea kubaeleza mpaka baelewe!.

`Nina ka swali kamoja kadogo kwako, please be honest, "jee ndani ya CCM kuna zaidi ya EL?",
 
Mkuu Mchambuzi, huu ni ukweli mchungu, ambao wanabody wengi humu wanapaswa kuuelewa na kuukubali, na kwa upande wangu, nakuaminia sana wewe Mchambuzi kwa uchambuzi wako mahiri, nakuomba sana endelea kubaeleza mpaka baelewe!.

`Nina ka swali kamoja kadogo kwako, please be honest, "jee ndani ya CCM kuna zaidi ya EL?",

Ndani ya CCM hakuna zaidi ya Lowassa, na naomba niazime dhana yako hiyo hiyo kwamba huu nao ndio ukweli mchungu. Wale wote wanaojipanga kumkabili Lowassa, success yao itakuwa highly determined na kuukubali ukweli huu (hata kwa shingo upande) kwamba ndani ya CCM hakuna zaidi ya Lowassa. Short of that, harakati zao hazitafanikiwa; Baada ya kusema haya, naomba niseme tu kwamba mimi binafsi bado sina mgombea, bado ninawa scrutinize kwa jinsi wanavyojitokeza na kujiuza kwenye soko la siasa; Lakini so far Lowassa yupo kwenye tano bora yangu, but not top three yet. Hii ni kwa sababu nina vigezo vyangu at least vitano vya kuangalia wagombea na sijavimalizia kazi miongoni mwa wanaotajwa tajwa;
 
Ndani ya CCM hakuna zaidi ya Lowassa, na naomba niazime dhana yako hiyo hiyo kwamba huu nao ndio ukweli mchungu. Wale wote wanaojipanga kumkabili Lowassa, success yao itakuwa highly determined na kuukubali ukweli huu (hata kwa shingo upande) kwamba ndani ya CCM hakuna zaidi ya Lowassa. Short of that, harakati zao hazitafanikiwa; Baada ya kusema haya, naomba niseme tu kwamba mimi binafsi bado sina mgombea, bado ninawa scrutinize kwa jinsi wanavyojitokeza na kujiuza kwenye soko la siasa; Lakini so far Lowassa yupo kwenye tano bora yangu, but not top three yet. Hii ni kwa sababu nina vigezo vyangu at least vitano vya kuangalia wagombea na sijavimalizia kazi miongoni mwa wanaotajwa tajwa;
Mkuu Mchambuzi, umemaliza kila kitu, hata nikilala leo, nitalala kwa amani!. Asante sana!.
 
Ndoto

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Mkuu Daudi Mchambuzi, kwa vile mida hii ni usiku, ndoto ndio mwake kabisa!, ingekuwa ni ndoto ya mchana, hapo ungesema, lakini kwa usiku, ndoto ndio mida yake!.

Vumbuzi nyingi duniani zilianzia kwenye ndoto ndio maana hata Membe anasubiria aoteshwe!.
Kama nafasi ya urais inaonekana ni kubwa sana kwa EL, usiwe na wasiwasi kwa sababu, hata lile limti la Mbuyu, ulianza kama mchicha!.
 
Siku hizi watu mnatumia hata keyboard kuharisha, mnadhani Tz tutaendelea kuwa wajinga wa kuikabidhi nchi mikononi mwa mafisadi wasiyokuwa na hata chembe ya huruma na hili taifa
 
Hauko serious. Lowasa u-billionea wake ule unafikiri kapatia Richmond? Au unafikiri ni ali-save mshahara wake akawa bilionea wa kutisha? Uliza watu alifanya nini alipokuwa waziri pale wizara ya Ardhi. Kumbuka Nyerere alimkataa Lowasa kwamba hana ethics za uongozi KABLA ya hiyo Richmond. Kumbuka wahindi waliomwambia Lowasa ananuka rushwa KABLA ya hiyo Richmond. Yes, anajua sana kuongea na kupanga hoja, lakini hivi unamjua Lowasa wewe?
Mkuu Synthesizer, niko very serious, in "between two devils, choose the lesser"!, CCM ni devil, ni zimwi, na ndani ya CCM, rushwa is the order of the day, hakuna msafi, kati ya hao wachafu wote, mwenye afadhali he is honest, genuine na besides all ni mtendaji!, kwa taarifa yako hao wengine ni wachafu zaidi kwa kumiliki mali kupitia watoto wao, wake zao mpaka vimada wao!. Zimwi likujualo, halikuli likakwisha, lazima litakubakisha tuu, EL ndilo zimwi letu likujualo!.
 
Siku hizi watu mnatumia hata keyboard kuharisha, mnadhani Tz tutaendelea kuwa wajinga wa kuikabidhi nchi mikononi mwa mafisadi wasiyokuwa na hata chembe ya huruma na hili taifa
Mkuu Shine, unamaanisha hii thread ni uha..?. Nakuomba sana ujiangalie kwa makini, 2015 utaha..sha kweli wewe utakaposikia ni EL!.
 
Kama kweli jamaa alikuwa msafi na anauchungu na wa TZ angewataja wa husika wa richmond ili wamuamini ni mtendaji na mtetezi. Bt jamaa kiukweli bila kuficha hafai tena hafai coz hakuona shida kuwasulubu wezi bali akabeba msalaba huo ambao hatautua kutoka mioyo ya watu up to the death. Namshauri ndoto hizo za mchana asiote tena. Wa TZ si maiti tena.
Mkuu Change is Must, tukikaribia darajani, mizigo tutaitua, wenye mizigo yao mtawajua!.
 
Pasco unataka kutuaminisha kuwa tatizo kuu la nchi yetu ni kukosa kiongozi mmoja bora wa kutuongoza, hivyo Lowassa ni mtu bora wa kipekee wakuja kutuongoza vema!!

Umechelewa sana, hakuna namna ambayo unayoweza kuwashawishi wanatanzania wa leo ambao wanaendelea kuelimishwa na CHADEMA kwa kasi ya ajabu warudi nyuma wakakueelewa, labda baadhi ya WanaCCM mazezeta ndio watakuelewa.

Kama unabisha muulize vizuri Lowassa ni kwa nini ndugu zake wameru kule Arumeru mashariki waliamua kuikataa CCM mbele ya macho yake pamoja na kupewa hongo za kila namna?
Mkuu Concrete, sio kutaka kuwaaminisha, bali ukweli ndio huuu na 2015, utashuhudia jinsi Watanzania tulivyo mazezeta japo wewe umesema baadhi ya wanaCCM mazezeta, kiukweli mtu akishachaguliwa, hata kama amechaguliwa na wana ccm, hao waliomchagua ni wananchi na atakuwa ni rais wa waliomchagua na wasio mchagua hivyo wote tutaishia kuwa mazezeta!.
 
Huyu Lowassa atatuumizia akili za kaka yetu Pasco.

Lowassa, he will never be a President of this Republic hata akigombea na Jiwe ni uhakika kuwa Jiwe litashinda. Lowassa ni mmoja waliomo kwenye list of Shame, alitajwa na rais wetu Dr Slaa kuwa ni fisadi kama Kikwete alivyo, still no difference mwizi ni mwzi tu hata ukimpa manyoya ya kuku bado ataiba hata mavi ya kuku.

Pasco you real need help ASAP
Mkuu Mzalendo80, sio atatuumizia, mimi ni tayari nimeshagua kambi, kwa maneno mengine, kama kuumia tayari nimeshaumia, ila kwa sifa za EL, hiki ndicho Watanzania tunachokitaka, kwani ukimuondoa Nyerere, waliobaki wote si ni majizi matupu?!.

Hatua hii ya kuwatangazia kuwa 2015 ni CCM tena, ni hatua nzuri ya kuwaandaa kisaikolojia kukubali matokeo na huku tukiidumisha upendo, amani, utulivu na mshikamamo wetu!. Watu wamehamika sana na mageuzi hivyo wana great expectations na mabadiliko, wakiyakosa, wanaweza ku despair na hata kuingia mitaani, hivyo ni vizuri kuwaanda kisaikolojia kuwa endapo CCM itamsimamisha EL, 2015 ni CCM tena!.
 
Hakuna kazi ngumu kama kumkampenia EL, Pasco you are on MISSION IMPOSSIBLE
Mkuu Kakalende, mimi simkampenii mtu, hapa si ninatoa tuu maelezo ya utangulizi!, kama huu utangulizi tuu, wewe unaouona ni kampeni, jee kampeni ikianza utasemaje?!.Kwa taarifa tuu, ndani ya CCM, hakuna mtu rahisi kumkampenia kama EL, kwa sababu yeye tayari ni iconic presidential figure!, anajulikana na kwa uwezo wake ni "chema chajiuza", CCM ikimteua mwingine yoyote, itabidi ifanye kazi ya ziada kumuuza kwa wananchi, kwa kuzingatia jinsi CCM ilivyopoteza mvuto, na hii kasi ya ajabu ya M4C, then muokozi pekee wa CCM 2015 ni one and only, EL!.
 
Last edited by a moderator:
Pasco, umejitahidi kufanya analysis yenye ushawishi, lakini kuna baadhi ya mambo ambayo naona haukuyatilia maanani (sijui kwa ushabiki au ni oversight tu). Kwanza, kwa ujumla, shida ya tanzania sasa hivi sidhani kama ni mtu mzuri wa kuongoza. tatizo kubwa linbaloikabili Tanzania hivi sasa ni mifumoya kiongozi ambayo haifanyikazi vile inavyotakiwa. Labda suala hili ndilo linalotutias giza na kuanza kuwajadili watu badala ya issues kwa sababu lenyewe linahusiana na personality pia.
Mkuu Mpitanjia, haya usemayo ni kweli tupu, mimi sikuyatilia maani sio kwa oversight wala sio kwa ushabiki, bali kwa uhalisia, hili la shida halisi ya Watanzania sip pesonalities, ni mifumo, huu ndio ukweli halisi, ila wenye kuujua ukweli huu ni the elite group ambao hata kura sidhani kama huwa wanabiga!. Watanzania wote waliobaki ambao ni waliowengi, huwa hawachagui sera, wala hawachagui chama bali wanachagua mtu!. Nenda kwenye data Alaysis ya uchaguzi wa 2010, utashangaa watu wa Vunjo wamemchagua Lyatonga kwa kura nyingi kwenye ubunge, na watu hao hao wakamchagua JK kwenye urais!. EL akisimama na yoyote, hakuna yoyote mwingine wa kushindana naye, watu waangalia sura tuu na hivi nywele zake ni nyeupe kama za Nyerere ndio kabisa, vizee vyote vitamchagua as if Nyerere amerudi!.
Lowassa au mtu mwingine anaweza kuonyesha quality za kiongozi mzuri lakini uongozi ni teamwork ambayo inapaswa kusaidiwa na mdumo mzuri. hapo yanaweza kuibuka matatizo mawili makubwa ambayo yanaweza kumfanya Lowassa ashindwe akishinda. Lwanza atakuwa na tiumu ya watu kutoka CCM ambako tayari kuna madonda makubwa na kpiga vita kwa hatari sana. Pili, huku akiwa na tiumu ambayo inatafunana ndani kwa ndani, atakumbana na mfumo ambao umegota kuanya kazi. Kwa kiasi kikubwa hata Kikwete ameshindwa kutokana na sababu hizimbili kuu.
Tanzania ilipofikia, haihitaji uongozi wa team work, inahitaji uongozi wa kijeshi type, you must do your job or fall out!, Kagame type, watu sasa they don't need a leader to show them the way, they need a ruler to rule, kunyoosha kwanza mambo nchi hii itoke kwenye mess we are in ndipo baadaye tutafute leaders!. JK ameshindwa simply because ni "dhaifu" period!. EL sio dhaifu!, he will rule with iron hand just to put things right on the track back again, ndipo tuendelee kubembelezana!.
Kwa hali ilivyohivi sasa CCMinapaswa kufa na kuzaliwa upya, na izaliwe mpya kweli, ikiachana na ya kale yote. Hili ni jambo ambalosidhani kama linaweza kutokea lenyewe na sioni uwezo wa Lowassa kulifanyahili litokee.Lakini pia kwa kiasi fulani Lowassa ameonyesha dalili za kuendeleza malumbano ya kutafunana kwa sababu ajalikana kuwa nimtu wa visasi.Mbaya zaidi, wakati wakiendelea kutafunana ndaniya CCM, huko nje Chadema, CUF na ADC nazo zitakuwa zikiendelea kuwatafuna. Unadhani Lowassa anaweza kweli kukabiliana na hali hii hasa ukizingatia wasi wasi wakokuwa afya yake inaweza kuwa na mushkeli?
EL is the man for that, kwa vile yeye ni CCM, na ni CCM imemtenda, he is the one and only, anayeweza kuinyoosha CCM na kushikisha adabu!, kwanza ataifumua yote na kuvunjilia mbali mitandao yote dhalimu!. Watu kama Six, Mwakiembe na wale waliojiita makamanda, kuna wengine watafuta pa kukimbilia na for sure kuna watakao ozea Segerea stating with Six na Mwaki, unless waikimbie nchi!.Kwenye chaguzi zote za nyuma, CCM was the determinant factor, ilikuwa inajiamulia, inataka kumsimamisha nani, Uchaguzi wa 2015, CCM sio determinant tena, kwa sasa determinant factor ni Chadema, its the one that ai calling the shots na CCM inapelekwa pelekwa kama inavyokimbizwa sasa, hata sina uhakika kama watu kama kina Nape wanalala usingizi!.Kufuatia kasi ya M4C, hakuna ubishi CCM imekalia kuti kavu na iko mkao wa kifo, hivyo kuelekea 2015, juhudi za CCM sio kutafuta kiongozi bora, bali kuangalia jinsi ya kijuokoa au kujinasua na kifo kilichoko mbele yake ambacho ni dhahiri!. Mkombozi pekee anayeweza kuinusuru CCM na kifo cha mende, is one and only EL!, hivyo CCM is left with no options, to live or let die!. Ikichagua kuishi, lazima imchague EL, vingenevyo 2015 ni bye bye CCM!.
 
Last edited by a moderator:
kama naiona Chadema itakavyopeta 2015. Mnamweka mwizi ndo awe rais? Wewe pasco na wasiwasi na thinking capacity yako!
 
Pasco na analysis zake nyepesi na zenye ufinyu wa kimtazamo hajambo. Umefungwa na nini kiasi kwamba you dont think of any other person except EL? amekupa nini? hebu jaribu kufikiria kama tunavyokufahamu. Achana na EL, sio mtaji mzuri. Utaukosa hata ukuu wa wilaya ukiendelea na tabia hii.
Mkuu Afwe, kwanza nakiri hizi analysis zangu ni nyepesi nyepesi na finyu ila ndizo la level ya chini kabisa ya mpiga kura!. Hivi kwa kelele zangu zote humu, bado kuna mnao amini ukk wa mkoa ni dili kubwa kwangu?!. EL ni mtaji mkubwa wa ukweli, nimeshaeleza huko nyuma, what does it mean for me and jf in general, iwapo EL atasimamishwa kugombea CCM!.
 
Tanzania ilipofikia, haihitaji uongozi wa team work, inahitaji uongozi wa kijeshi type, you must do your job or fall out!, Kagame type, watu sasa they don't need a leader to show them the way, they need a ruler to rule, kunyoosha kwanza mambo nchi hii itoke kwenye mess we are in ndipo baadaye tutafute leaders!. JK ameshindwa simply because ni "dhaifu" period!. EL sio dhaifu!, he will rule with iron hand just to put things right on the track back again, ndipo tuendelee kubembelezana!.
Nakubaliana na maneno yako Pasco, lakini yamenifanya nianze kuwaza jingine... the fall out kati ya JK na Lowassa. JK anafahamika kama mtu anayependa popularity na Lowassa 'dikteta' anayependa kusukuma mambo yaende. Hivi hii ndiyo sababu iliyowakosanisha?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom