Kuelekea Kombe la CAFCC | Haya yafanyike kwa Simba SC dhidi ya USGN ili kuepusha ya Jwaneng Galaxy

Kuelekea Kombe la CAFCC | Haya yafanyike kwa Simba SC dhidi ya USGN ili kuepusha ya Jwaneng Galaxy

Zimebaki siku chache kabla ya Simba SC kushuka dimbani kuwavaa USGN kutoka Niger katika pambano la kuwania alama tatu muhimu ili kuweza kutinga hatua ya robo fainali Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Ili Simba SC iweze kushinda mchezo dhidi ya USGN mambo haya yafanyike haraka ili kuepusha yaliyotokea kwenye mchezo muhimu sana kwa kufungwa 3-1 na kuondoshwa kwenye Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy.

1. Simba SC waingie na mpango wa kuchagua kuwa direct kushambulia huku wakiwa na mbinu ya kuzuia kwanza eneo la USGN ili kuwanyima uhuru wa kuanzisha mashambulizi kutoka chini.

2. Simba SC wasikubali kufunguka kirahisi, na maamuzi yafanyike kwa haraka sana katika kuutoa mpira katika zone yao, USGN wakifanikiwa kuvunja mstari wa pili wa Simba wa wachezaji wanne ambao unazuia njia ya pasi, itakuwa ni hatari sana Simba SC.

3. Umakini uwe silaha muhimu kwa Simba SC pale wanapopoteza mpira wakati wa kutengeneza mashambulizi, yapasa kuzuia kwa shape ya 4-4-2 au 5-4-1 kuziba njia ya pasi za USGN na kufunga half spaces zote kwa kuwa na idadi kubwa ya wachezaji wanaozuia eneo la Simba SC.

Kwa maandalizi yote yanaendelea nina imani Simba SC kuibuka na ushindi ijapo kuwa mpira ni dakika 90, lakini bila shaka Viongozi, benchi la ufundi pamoja na wachezaji wote watatimiza majukumu yao kiweledi huku mchezaji wa 12 ambaye ni Shabiki akijitokeza kwa wingi kwenye Dimba la Benjamin Mkapa ili kuipasupport Simba SC wakipeperusha vema bendera ya Nchi ya Tanzania.

Kwako Mshabiki na Mdau wa Soka nini kifanyike kuepusha kufurushwa kwenye Kombe hili la pili kwa Ukubwa Barani Afrika... Karibu...!

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
Hii Game Simba Anapoteza.
KWA Matuta.

Kocha awafunde kupiga penalty la sivyo watapoteza

Sent from my TECNO RC6 using JamiiForums mobile app
 
Bila makandokando Simba hawezi shinda hii mechi!!!
 
Bila makandokando Simba hawezi shinda hii mechi!!!
Makandokando kama yapi unazungumzia kwenye mpira ambao unachezwa wazi uwanjani..?!
 
Sioni dalili yoyote ya Makolo kushin a hii mechi,wale wazee wamechoka
Sawa Wazee..Nyie wale Watoto wenu wamewafikisha wapi? Si mmepigwa Kombora moja tu mkapotea mpaka leo.
 
Huo uharaka wa timu inategemeana na flexibility,control,skills na dribbling ya mchezaji. Pale simba hakuna mchezaji mwenye sifa hizi ukiwatoa Sakho,Morison na Shabalala. Hivi Lwanga uzito aliokuwa nao kwenye kugeuka na kimbia ataweza fanya haya unayotaka Simba wafanye? Mkude mzito pia na hana wepesi,
Maneno ya kijinga yakitamkwa kwa kizungu yanaoneka ya maana sana!sijui nani alituroga!
 
Kikubwa Kocha Aweke Kikosi Cha Kazi

Nitashangaa Kama Morrison Hata Anza Hii Mechi. Nitashangaa Lwanga Asipo Anza
 
Amejichanganya tu huyo Jamaa, Nadhani hajafuatilia kwa undani hatua hii Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
HapanA, nilikuwa na haraka ya kuandika.
Ni kwamba, ushindi wa Simba utakuwa ndani ya penati.
Kocha ajitahidi kuwanoa vijana wake katika kupiga penati.

Wanaweza kupata penati na wakakosa, jambo ambalo linaweza tamatisha safari yao.

Sent from my TECNO RC6 using JamiiForums mobile app
 
HapanA, nilikuwa na haraka ya kuandika.
Ni kwamba, ushindi wa Simba utakuwa ndani ya penati.
Kocha ajitahidi kuwanoa vijana wake katika kupiga penati.

Wanaweza kupata penati na wakakosa, jambo ambalo linaweza tamatisha safari yao.

Sent from my TECNO RC6 using JamiiForums mobile app
Okay...Kumbe ndo kusudio lako...!
 
Back
Top Bottom